Car alarm systems si salama sana, kuna siku nilikua nafungua gari kwa remote, gari nyingine nayo ikafunguka

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,052
40,715
Ilikuwa ni sehemu ya parking ya magari mengi sana, nilishangaa kila nikifumgua gari kwa remote , kuna gari nyingine kama mita 10 toka nilipo nayo ikawa inatoa mlio kama inafunguka, nikifunga kwa remote na yenyewe inatoa mlio kwamba inafunga sambamba na ile inayolengwa. Nikarudia hilo zoezi la kufunga na kufungua kama mara 10 ili kujiridhisha.

Sasa naomba kujua, inawezekanaje remote ya alarm system ya gari moja inakuwaje inaweza kufungua na kufunga alarm system ya gari nyingine?

Ina maana kama yule mwenye gari nyingine angekuja kufungua gari yake, na yangu pia ingefunguka, na kama si muaminifu lolote linaweza kutokea
 
Sio ya kiwandani, ni zile wanaita Octopus wanazofunga hawa watu wa Music sound nk.
Nilikuwa na wasiwasi kuwa ndio izo izo za kuunganishiwa hapa hapa. Nafikiri izo huwa mara nyingi ni kama remote ya TV tu ufanyaji kazi wake. Zile za kiwandani funguo huwa zinakuwa coded, ili hizi za pweza badala ya kutumia coded key, itakuwa inatumia mionzi tu pekee direct.

Hatari kweli kweli. Mana apo kama umeweka kwenye parking wewe umo ndani kwenye mall mtu anapekura vizuri tu na mlinzi anamtizama mana anajua ni ya kwake hana wasi.
 
Ilikuwa ni sehemu ya parking ya magari mengi sana, nilishangaa kila nikifumgua gari kwa remote , kuna gari nyingine kama mita 10 toka nilipo nayo ikawa inatoa mlio kama inafunguka, nikifunga kwa remote na yenyewe inatoa mlio kwamba inafunga sambamba na ile inayolengwa. Nikarudia hilo zoezi la kufunga na kufungua kama mara 10 ili kujiridhisha...
Kwa mchina kawaida tu Jombaa,

Hujawahi kuona ufunguo wa Chumbani unafungua na Stoo?
 
Kwa Car Security nzuri wafuate Multi lock Tanzania wapo mkabala na Maktaba.Wana security alarm system za magari.

Hawa zamani walikuwa na lock ya kufunga kwenye gear level na milango hii mpaka mwizi aibe basi itambidi abebe gari kwa breakdown au winch.
 
Ilikuwa ni sehemu ya parking ya magari mengi sana, nilishangaa kila nikifumgua gari kwa remote , kuna gari nyingine kama mita 10 toka nilipo nayo ikawa inatoa mlio kama inafunguka, nikifunga kwa remote na yenyewe inatoa mlio kwamba inafunga sambamba na ile inayolengwa. Nikarudia hilo zoezi la kufunga na kufungua kama mara 10 ili kujiridhisha..
Hilo ndiyo tatizo la after market security features.

Si unajua tena wachina na mambo yao. Yaani mimi hizi alarm za kununua huku bongo, naziona zipo kama sub woofer za kichina tu...remoti moja inaingia kwenye sub woofer nyiingi
 
Na wafungaji wengi wa hizi alarms si professionals....ndiyo maana magari mengi ya watu yanawaka moto hovyo na kuteketea.

Kuna documentary moja nilikuwa naangalia namna ya ufungaji wa hizo security alarms, kwa kweli hapa bongo watu wengi wanaunga unga tu bora ilie.

Nikikumbuka jina la ile site nitashare link hapa..
 
Na wafungaji wengi wa hizi alarms si professionals....ndiyo maana magari mengi ya watu yanawaka moto hovyo na kuteketea.

Kuna documentary moja nilikuwa naangalia namna ya ufungaji wa hizo security alarms, kwa kweli hapa bongo watu wengi wanaunga unga tu bora ilie.

Nikikumbuka jina la ile site nitashare link hapa..

Kwa hiyo wewe security system ya kwenye gari yako umeweka kutoka wapi. Ni ile kutoka kiwandan ilokuja na gari? Ama hujaweka kabisa.
 
Kwa Car Security nzuri wafuate Multi lock Tanzania wapo mkabala na Maktaba.Wana security alarm system za magari.

Hawa zamani walikuwa na lock ya kufunga kwenye gear level na milango hii mpaka mwizi aibe basi itambidi abebe gari kwa breakdown au winch.

Wazee wa T lock tulikua tunafunga gear kwenye Reverse dah😂😂. Siku nyingi sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom