Captain Mbwana Samatta nakuomba tusamehe Watanzania, Taifa Stars ikifungwa mbaya Wewe ila ikishinda Sifa wanapewa Wengine

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,073
107,565
Najua unavyoumia Mdogo wangu ila GENTAMYCINE nasema Watanzania tutakutusi, kukashifu na kukuona huna lolote ila hapo hapo ulipo tambua kuwa Wewe ndiyo Shujaa yetu namba Moja ndani ya Kikosi cha Timu ya Taifa Tanzania ya Taifa Stars.

Najua kuwa Taifa Stars ikifungwa basi Sisi Waswahili tunakutupia lawama zote Wewe ila ikishinda tu kwa Unafiki wetu wa Kutukuka tunakusahau ghafla na kwa muda kisha tunaanza Kuwasifia wengine wanaofunga Magoli ya Kawaida sana ( japo yanasifiwa kuwa ni mazuri ) wakati Wewe umeyafunga hayo sana tu ukiwa TP Mazembe, Genk na Aston Villa na wala hukuwa Mshamba ( Mbwiga ) Kuyashangilia mno kwani una Kipaji na Uwezo pia.

Nakuhakikishia Captain Mbwana Samatta wacha Wanafiki na Waswahili tukuseme sana na tukuone huna Faida wala Msaada wowote kwa Taifa Stars ila nina uhakika kuwa Mguu wako pekee ama Kichwa chako vitatupeleka rasmi na kwa mara ya Kwanza Kombe la Dunia huko QATAR na hapo ndiyo unaenda Kutufunga kabisa Midomo na tutabaki na Aibu zetu huku tukihaha kutaka kuja Kukuomba Radhi ( Msamaha ) kwa yote.

Tuvumilie tu Captain Wetu na tuzoee!!!!
 
Najua unavyoumia Mdogo wangu ila GENTAMYCINE nasema Watanzania tutakutusi, kukashifu na kukuona huna lolote ila hapo hapo ulipo tambua kuwa Wewe ndiyo Shujaa yetu namba Moja ndani ya Kikosi cha Timu ya Taifa Tanzania ya Taifa Stars...
Na hasa wewe unakimdomo Sana kazi kila ck kichonga chonga tu

Unabadiri daily na I'd mpya mpya tu



Asipocheza mzamiru kuanzia mechi Ile tutashinda Ila akicheza Tu imekula kwetu


Naomba msamaha

Mie mswahili
 
Kuna watu Kama wamekariru, uwepo wa Samatta uwanjani Kuna vitu inaongeza Kwanza mabeki wanahofia kupanda ila kwa sababu quality ya wachezaji wetu ni ndogo tunaishia kumlaumu
 
Umenena kweli Ila penye kubeba lawma anapokosa nafasi za wazi hakuepukiki siyo kwake Tu team nzima bila kumsahau bocco na msuva
 
Game iliyopita dhidi ya goli la Msuva,mimi nilimuona huyo Samata akiwa mchoyo kwa wafungaji kwa kujipigia mipira golini wakati tayari kwenye box kuna watu wa kufunga.Tulikuwa na uwezo wa kufunga zaidi ya goli lile moja,aache uchoyo.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom