Cameroon yashindwa kuqualify CAN 2012 licha ya ushindi

Sinkala

JF-Expert Member
Dec 22, 2008
1,773
683
Cameroon imeichapa DRC mabao 3-2 ugenini mjini Kinshasa, lakini haitaenda CAN 2012 kutokana na kuwa ya pili bila hata ya kujali matokeo ya pair nyingine ya mechi kati ya Mauritius na Senegal. Cameroon imemaliza mechi sita kwa kupata pointi 11 huku Senegal ina pointi 13 hata kabla haijaivaa Mauritius. Mechi hizi hazikuchezwa pamoja kwa kuwa hakukuwepo uwezekano wa kupanga matokeo.

Cameroon inasubiri miujiza kuingia katika kapu la washindi wa pili walio na matokeo bora (best run-up) lakini ni kama vile haupo uwezekano, kwani katika timu tatu za best run-up, tayari mmoja (Sudan) ameshaondoa matumaini hayo kwa kuwa wa pili kwa pointi 13. Timu nyingine zilizo za pili na mchezo mmoja mkononi kwenye makundi yao lakini zina pointi 11 sawa na Cameroon ni Libya na Tunisia, huku Nigeria na Angola zikishinda kwenye makundi yao zitafikisha point 12
 
Haha tanzania tutakwalifai na kuchukua hili kombe 2012 .usicheze na sisi kabisa
 
Kenya nao wamewabania uganda ambao ndio walikua na muelekeo wa kuwakilisha east africa huko CAN 2012 lakini wamewabania wametoka sare ya 0-0,na angola ameshnda 2-0,kwa matokeo hayo uganda amekosa nafasi,alitakiwa ashinde na amekosa magoli mengi sana waganda,sasa east africa tutaendelea kuwa waangaliaji na washangiliaji wa mataifa mengine.
 
Kenya nao wamewabania uganda ambao ndio walikua na muelekeo wa kuwakilisha east africa huko CAN 2012 lakini wamewabania wametoka sare ya 0-0,na angola ameshnda 2-0,kwa matokeo hayo uganda amekosa nafasi,alitakiwa ashinde na amekosa magoli mengi sana waganda,sasa east africa tutaendelea kuwa waangaliaji na washangiliaji wa mataifa mengine.

Sad news
 
KTK vigogo wa africa ambao hawakupata nafasi ya kushiri CAN hapo mwakani ni MISRI,CAMEROUN,NIGERIA,CONGO DRC,NA HATA SOUTH AFRICA ANA NAFASI FINYU SANA YAKWENDA,ILA KILichonisikitisha ni kenya kuwabania vilivyo uganda wakati kenya walikua hawana nafasi yoyote,ila uganda alihitaji goli 1 na point3 awe amefuzu,sasa amefuzu angola,east africa tunaendlea kuwa watazamaji bila mwakilishiwetu hata 1.
 
Tanzania tungeachana na mechi za kimataifa kwa muda kidogo tujipange na team za watoto under 17 na 20 baada 8yrs tuanze upya...
Kwa sasa tunapoteza pesa bure hao wazee wanacheza kkuangalia tv tu sio kufundishwa na makocha....hawafundishiki wakiwa wameshakomaa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom