Camera ya cannon type ipi iko vizuri kwa picha?

Entrepreneur na mwanafunzi wa chuo kimoja Dar ninampango wa kununua camera kwa ajili ya kufanyia biashara ya upigaji picha kwa matukio kadhaa sitakua na studio kwa sababu biashara hii ni ndogo.

Nahitaji kufahamu camera ipi ni nzuri kwa mawazo yangu ninampango wa kununua cannon lakini sijajua cannon model gani ndo itakua suitable.
[HASHTAG]#msaada[/HASHTAG] tafadhali
a4663277d34f72b34e728849d4ab17c3.jpg


Hujasema ni picha za mnato na video au? Any way Kwa kuanzia Canon 600D itakufaa.. inapiga both video na mnato
 
WAKUU,

NINA KAMERA YANGU NDOGO AINA YA NIKON.

TATIZO NI KWAMBA NINAPOIWASHA ILI NIPIGE PICHA LENS HAICHOMOKI,
NA INAONESHA UJUMBE
UNAOSOMEKA
"Lens Error".

KUNA MWENYE UJUZI WA KULI_FIX HILO TATIZO.
 
Tafuta canon 700D au 750D hio 700D Dec 2015 niliinunua 1,240,000 freedom communications samora bila risiti, ila mtaa huo huo wa samora karibu na askari monument niliona wanaziuza 1,389,000 sasa hivi navyo type kariakoo 700D wanauza 1,900,000 kariakoo, ila milioni 1-900,000 utazipata kama bado unahitaji
Nna 600D Canon kamera nzuri sana
 
Za muda huu,

Mtoa mada na wengineo..!

Naomba nitoe ushauri kidogo juu ya hili bandiko; Vitu vya kuzingatia unapotafuta camera especially DSLR camera
1. Kwa kuanzia hakikisha camera unayonunua ina kianzio cha 16 Megapixel
2. Wekeza zaidi kwenye lens achana na kuhangaika kununua camera kubwa wakati unaanza business,uzuri wa DSLR camera ukitaka ku-advance basi unabadili tu Body maana lens utakuwa nazo
NOTE: Epuka kuanza na camera kubwa kama zilizotajwa na wadau hapo juu Eg. canon EOS 5D Mark 3,2 7D au Nikon D7100, D7200 ni aghali sana hivyo kama huna hela ya kutosha achana nazo, badala yake tafuta camera za kuanzia Eg Canon 1300,Canon 77D, Canon 80D, Canon 750D, Canon EOS 800D, Canon EOS 200D/300D, Canon EOS 700D
au Ukipenda Niko basi Nikon D3200, D3300 au D5600 (pia Nikon D3100 ila tafuta Prime Lens/ Lens Kubwa)

Hizo camera ambazo nimekutajia ni camera nzuri kwa kuanzia na bei zake si mbaya zingonga still na Video kiwango cha 1080p (yaan full HD. Kama una Link marekani Kuna Amazon wanauza hizo camera with full Package( Camera body,lens,wide angle lens, tripod, Flash and 32GB memory card. Kwa Amazon ivyo vitu unavipata betwen $350-400.

Ambapo ukinunua tanzania, huwa hupewi package ya namna hiyo, watakupa tu Camera peke yake tena wakati mwingine Bila Lens so cost ya kuanza kutafuta vitu vingine inakuwa Kubwa.

Personally mimi ni Mfanyakazi nimeajiriwa, ila nafanya business ya photographing and Videographing, nilianza na Nikon D300 for still na D3100 for Video, ni camera ndogo kiasi kwamba wakati mwingine wapiga picha wengine wakiona picha zangu wanashangaa nikiwaambia kuwa zimepigwa kwa Nikon D300, ila nimewekeza kwenye Lens kubwa baasi, tena huwa sifanyi Editing kabisa editing yangu ni from my camera setting tu baasi baada ya hapo nahamisha picha kwenye computer na kuzichambua na kupeleka studio kwa kusafisha, mambo ya Photoshop sijui huwa napiga kwa picha za advert tu (mitandao ya kijamii etc)

MTAZAMO wangu Camera kubwa sio ishu as long as camera ni dslr, una lens za kutosha 18mm-55 and 55-200, pixel from 16 na kuendelea nakuhakikishia utafanya kazi nzuri sana, kitu nilicho note kwa Wapiga picha wengi hawataki kuwekeza kwenye knowledge ya kazi yao, dslr zina setting nyingi sana kiasi kwamba ukiwa unatafuta elimu kuhusu matumizi ya hiyo camera yako unajikuta unafanya kazi nzuri hadi watu watashangaa.
Perfect!
 
Kuna mtu anataka kuniuzia nikon 700D iko complete lens mbili bag cleaning tools 1.3m hii bei ni fair kweli na. Camera katumia 8months .

Au
Nikanunue k.koo nikon 3300D. Lens moja ile mwisho 55
 
Kuna mtu anataka kuniuzia nikon 700D iko complete lens mbili bag cleaning tools 1.3m hii bei ni fair kweli na. Camera katumia 8months .

Au
Nikanunue k.koo nikon 3300D. Lens moja ile mwisho 55

Bajeti yako ingekua ipo vizuri ningekuuzia kitu cha 5d markIII kipya full set utambe hapa mjini
 
Kama upo serious na hiyo kazi, una customers base njoo inbox nitakukabidhi vifaa vya kisasa ikiwemo canon new model ( 5D mark 3)..njoo na wazo tufanye kazi..sharti ni moja tu uje na idea ya namna gani tutapata pesa na idea iwe realistic
mkuu vip umeshapataga mtu? mm nilikuwa na aidea nzuri tu jinsi ya kutengeneza pesa na camera
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom