CallTanzania.Com

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
803
Kuna mtu yeyote ambaye ameishajaribu kutumia hizi card zilizo kwenye barners za hapa JF CallTanzania.Com?

Kama yupo naomba anisaidie yafuatayo, nataka kujua quality ya sauti na kama kweli rate hizo walizosema ziko sawa ama ni biashara ya kuvutia matangazo? Kuna kadi nyingine ukipiga baadhi ya mitandao connection inakuwa mbovu na credit inaliwa hata bila kuongea, je, hizi kazi zinatwanga mitandao yote ya Bongo?
 
Keil,
I am using CallingCardplus.com. Give them a try they have good rates for Tanzania.
 
Nisaidieni kidogo hizo ni kadi za namna gani na zinatumika kivipi? Ni kwa walio majuu tu?
 
Ehhhhh,
Usiingie Mkenge juu juu.
Hii quality ya sauti inategemea uko mbali kiasi gani kutoka STATION ya hawa jamaa au kama hapo ulipo kuna STATION ya hawa jamaa. Tuseme kama uko UK, ni poa sana kutumia SKYPE. Kama uko USA ni poa sana kutumia REBTEL nk. Sasa tuseme uko USA na unaunganisha SKYPE iliyopo UK, basi ujue kuna TIME delay hadi kufika UK na hapo ndipo uende kuunganishwa tuseme Kikuyu kwa Wagogo. Lakini unaweza kujaribu maana wengi hutoa dakika walau mbili uonje RAHA ya kuongea na wazee huko Mwanelumango au Mkomanzi... Hivi ndivyo nijuavyo mimi juu ya VoIP. Sijui kama imebadilika kwa sasa.
 
Kwa muda wa zaidi ya mwezi sasa hapa JF kumekuwa na matangazao ya CallTanzania.com yakiashiria kuwa bei ya simu kuita Tanzania (nadhani kutokea marekani) ni senti 13 tu kwa dakika. Swali langu siyo kuhusu huduma zenyewe bali wamiliki wa biashara ile; je ni watanzania?

Utafiti wa haraka haraka umeonyesha kuwa kampuni hii CallTanzania.com inamilikiwa na Miron Enterprises LLC, ambayo pia inamiliki keepCalling.com na PeruTel.com. Miron Enterprises LLC yenyewe inamilikiwa na mtu ajulikanaye kama Florin Miron, na imesajiliwa huko Americus, Georgia. Lakini CallTanzania.com, KeepCalling.com na PeruTel.com zote zinaendesha biashara zake kutokea address moja ya Bellingham, Washington State.

Kama kuna anayemjua huyu bwana Miron kwa zaidi namwomba anisaidie kujua kama jamaa huyo ni Mtanzania. Nina dukuduku tu kwa vile tangazo lake linayoonyesha utanzania sana. Nafahamau wakenya kadhaa ambao wana makampuni ya simu na wanafanya vizuri kwa sitashangaa kusikia kuwa kuna watanzania pia wameshaingia kwenye biashara hiyo ambayo inalipa sana.
 
Back
Top Bottom