Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,378
Waliofariki kutokana na ajali hiyo katika maeneo mawili ya jimbo, Magharibi ya Marekani imefikia 42 hivyo kuweka rekodi mpya ya vifo kutokana na moto katika jimbo hilo
Waliofariki walikutwa kwenye magari baada ya kukumbwa na moto mkubwa uliokuwa unasambaa kwa kasi, wengine walifariki wakiwa majumbani mwao
Takribani watu 228 hawajulikani walipo, Majengo zaidi ya 7,200 yameharibiwa huku mengine 15,500 yakiwa hatarini kuharibiwa. Watu 250,000 walazimika kukimbia makazi yao
Moto huo mkali uliopewa jina la Camp Fires ulianza Kaskazini ya jimbo hilo na kuteketeza kabisa mji wa Paradise
Gavana wa Jimbo, Jerry Brown amesema 'Hatujui sababu za moto huo ila Mji wa Paradaise ulijitayarisha vya kutosha kukabiliana na hali mbaya ya hewa ya ukame na upepo mkali
UPDATES
Idadi ya Watu waliofariki kutokana na ajali ya moto unaochoma msitu nchini Marekani imefikia 71 huku zaidi ya watu 1,011 hawajulikani walipo, Askari Kory Honea amesema hayo jana Novemba 16
Zimamoto wamejikuta wakipambana na aina mbili za moto katika msitu huo ambapo awali walikuwa walipambana na moto uliopewa jina la 'Camp Fire' uliopo katika Kaunti ya Butt lakini sasa umeibuka mwingine katika Kaunti ya Ventura uliopewa jina la 'Woolsey Fire'
Wameeleza kuwa Mvua ingezaidia kuuzima moto huo lakini ingeleta ugumu katika kuwatafuta waliopotea na kupoteza maisha kutokana na kwamba wamekuwa wakikutana na mifupa tu au vipande vya mifupa ya watu
Camp Fire umeharibu nyumba 9,700 na majengo 144 na hadi kufikia jana ulikuwa umezimwa kwa 45% na sehemu iliyobaki haihatarishi maeneo yenye watu wengi
Aidha, Kusini mwa California watu zaidi wamekuwa wakiruhusiwa kurudi majumbani kwao baada ya asilimia 69 ya Woolsey Fire kuzimwa hadi kufikia jana usiku, moto huo umeteketeza nyumba 600
Waliofariki walikutwa kwenye magari baada ya kukumbwa na moto mkubwa uliokuwa unasambaa kwa kasi, wengine walifariki wakiwa majumbani mwao
Takribani watu 228 hawajulikani walipo, Majengo zaidi ya 7,200 yameharibiwa huku mengine 15,500 yakiwa hatarini kuharibiwa. Watu 250,000 walazimika kukimbia makazi yao
Moto huo mkali uliopewa jina la Camp Fires ulianza Kaskazini ya jimbo hilo na kuteketeza kabisa mji wa Paradise
Gavana wa Jimbo, Jerry Brown amesema 'Hatujui sababu za moto huo ila Mji wa Paradaise ulijitayarisha vya kutosha kukabiliana na hali mbaya ya hewa ya ukame na upepo mkali
UPDATES
Idadi ya Watu waliofariki kutokana na ajali ya moto unaochoma msitu nchini Marekani imefikia 71 huku zaidi ya watu 1,011 hawajulikani walipo, Askari Kory Honea amesema hayo jana Novemba 16
Zimamoto wamejikuta wakipambana na aina mbili za moto katika msitu huo ambapo awali walikuwa walipambana na moto uliopewa jina la 'Camp Fire' uliopo katika Kaunti ya Butt lakini sasa umeibuka mwingine katika Kaunti ya Ventura uliopewa jina la 'Woolsey Fire'
Wameeleza kuwa Mvua ingezaidia kuuzima moto huo lakini ingeleta ugumu katika kuwatafuta waliopotea na kupoteza maisha kutokana na kwamba wamekuwa wakikutana na mifupa tu au vipande vya mifupa ya watu
Camp Fire umeharibu nyumba 9,700 na majengo 144 na hadi kufikia jana ulikuwa umezimwa kwa 45% na sehemu iliyobaki haihatarishi maeneo yenye watu wengi
Aidha, Kusini mwa California watu zaidi wamekuwa wakiruhusiwa kurudi majumbani kwao baada ya asilimia 69 ya Woolsey Fire kuzimwa hadi kufikia jana usiku, moto huo umeteketeza nyumba 600