CAG: Uwanja wa Ndege Chato ni mradi usio na faida

Mmawia

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
121,947
95,237
Tulisema tukaitwa wapinzani tuna wivu.

Sasa wenye mamlaka wa kusema wamesema.

--
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere amesema gharama za ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Chato mkoani Geita zilizidi bajeti iliyotengwa kwa sababu ulifanyika bila upembuzi yakinifu.

CAG alisema kutofanyika kwa upembuzi yakinifu kunaongeza hatari kwa Serikali kuwekeza katika mradi usio na tija na uwezekano wa kuwapo gharama zisizodhibitiwa na ongezeko la muda katika utekelezaji wake.

“Mpatio yangu yalibaini Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) hawakufanya upembuzi yakinifu kabla ya kuanz aujenzi,” amesema Kichere.

CAG Kichere amesema Sh3.62 bilioni za mradi huo zilitolewa kwenye miradi mingine kwa matarajio kwamba zingerejeshwa baada ya Hazina kutoa fedha zake, jambo ambalo halikutekelezwa kwa wakati hivyo kusimamisha miradi mingine iiliyopangwa.
 
Ilikuwa ni Serikali ya kifisadi pia🐒🐒🐒
MiT7A.jpeg
 
Tulisema tukaitwa wapinzani tuna wivu.

Sasa wenye mamlaka wa kusema wamesema.

.https://www.instagram.com/p/CcUyVOhtBIe/?igshid=YmMyMTA2M2Y=
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo uwanja wa Chato ulikuwa na umuhimu gani kujengwa chato wakati kuna uwanja wa Mwanza na pale Bukoba?
 
Tulisema tukaitwa wapinzani tuna wivu.

Sasa wenye mamlaka wa kusema wamesema.

.https://www.instagram.com/p/CcUyVOhtBIe/?igshid=YmMyMTA2M2Y=
Hata mobutu seseseko kuku wa zebanga alijenga uwanja MKUBWA wa ndege kijijini kwao lakini baada ya kifo chake kiwanja hicho kimekuwa uwanja wa kuchungia mbuzi.....
Afrika siasa Ni ngumu kuliko fizikia..
 
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
Tofauti ni kuwa viwanja vya Musoma na Mtwara vimejengwa miji mikuu ya mikoa sehemu ambazo kuna watu na biashara nyingi wakati uwanja wa Chato umejengwa kijijini kwenye watu wachache ni biashara chache!
 
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
Una tofauti kubwa ndugu yangu. Ukitaka kujua jaribu kufikiri uwanja wenye hadhi ya Chato ujengwe chalinze au Mwanga. Ungeona ni sawa?
 
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
Kulikuwa na uharaka gani wa kujenga uwanja Chato wa runway ya kimataifa bila idhini ya bunge?? Hivyo viwanja vingine viko kwenye mpango kazi wa TAA

Mkuu Mpinzire hebu shirikisha ubongo wako japo kwa dakika 5
 
Hivi uwanja wa ndege wa Chato unatofauti gani na Uwanja wa Ndege wa Musoma unaojengwa? Au wa Mtwara? Hizo faida anazotaka CAG ni zipi? Zionekane baada ya mda fani? Maana nina hakika ata ujenzi wa terminal 3 Mwaimu Nyerere bado hatujaanza kupata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
Badala ya kulilia legasi ni vema ukatueleza ni lini tutapata faida na itatokana na nini
 
Back
Top Bottom