CAG Prof. Mussa Assad amjibu Spika Ndugai, Asema Katiba ya JMT haina kifungu kinachomtaka ajieleze

africansongs

Member
Jan 5, 2018
83
225
CAG ameamua kumjibu mheshimiwa spika baada ya press conference ya jana ambayo spika amemtaka ajiuzulu.

Katika majibu hayo CAG amebainisha vizuri akitumia vipengele vya Katiba kuainisha wajibu wake bila kutetereka.

Hii ngoma ni kali kweli kweli, maana hapa kuna msomi vs mwanasiasa.

Sijui mshindi ataibuka nani.

======

Mara baada ya mkutano huo wa Spika Ndugai, Mwananchi lilizungumza na Profesa Assad ambaye alijibu kwa ujumbe wa maandishi akisema, Katiba haina kifungu cha kujieleza.

“Soma Katiba 143 ina disciplinary arrangements (mpangilio wa hatua za nidhamu), kujieleza haimo,” alisema Profesa Assad.

Ibara ya 143 (6) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, inasema “Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali, lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo hayataizuia Mahakama nayo kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ametekeleza”.

Ibara ya 144(3) inasema “iwapo Rais anaona kwamba suala la kumuondoa kazini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kwa mujibu wa masharti ya ibara hii lahitaji kuchunguzwa” atateua Tume Maalum ambayo itakuwa na mwenyekiti na Wajumbe wengine wasiopungua wawili.

Sehemu hiyo inasema mwenyekiti na angalau nusu ya wajumbe wengine wa tume hiyo itabidi wawe watu ambao ni majaji au watu waliopata kuwa majaji wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufani.

Awali katika maelezo yake, Ndugai alimsifu Profesa Assad kwa ujasiri wake huku akiufananisha na ujasiri wa mbwa kumtukana mtu anayemlisha.

Aliendelea kusema pia kuwa hana chuki binafsi na Assad bali tatizo ni lugha tu.

“Unatukana hadi mkono unaokulisha, inahitaji ujasiri
 
Hizo hoja za CAG ziko wapi hapo?

Anyway, Ndugai hajui maana ya Separation of power, asijaribu kuuingiza mhimili wa serikali katika hili suala.
CAG hakusema Rais ni dhaifu alisema "Bunge lina udhaifu" na wala hakusema bunge ni dhaifu.

Ndugai apambane na hali yake!. Asitafute huruma ya Magufuli.
 
Serikali na Bunge ni vitu viwili tofauti...hivyo Ndugai aache uongo. Rais hawezi kuwa sehemu ya Bunge hata kama anasaini yanayopitishwa na Bunge.

Mihimili ipo mitatu. Spika Ndugai aache chuki binafsi na CAG, kwanza CAG hakusema bunge ni dhaifu ila alisema "kama mapendekezo ya CAG kuhusu upotevu wa pesa hatua hazitachukulia haitakuwa suala lake bali litakuwa ni udhaifu wa bunge" hapo amejibu swali kutokana na jinsi alivyoulizwa.

Hapa linaloendelea kutokea ni kuwa kuna ubadhirifu mkubwa sana wa fedha za umma kwa hiyo wanaona jinsi ya kulificha hili tatizo ni kumtibua CAG na kumsemea uongo ili afukuzwe.

Hakuna asiyejua nia ya ndugai na Magufuli....kumfukuza CAG na kumuweka mtu wa aina ya Doto James ili waendelee kuchukua fedha zisizo idhinishwa.
 
Hizo hoja za CAG ziko wapi hapo?

Anyway, Ndugai hajui maana ya Separation of power, asijaribu kuuingiza mhimili wa serikali katika hili suala.
CAG hakusema Rais ni dhaifu alisema "Bunge lina udhaifu" na wala hakusema bunge ni dhaifu.

Ndugai apambane na hali yake!. Asitafute huruma ya Magufuli.
Yale mashavu kuumuka vile ni afya kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa ninawashangaa sana wale wanaoamini mzee wetu ni mtetez wa wanyonge
Usimuhusishe mpendwa wetu katika hili, hawezi kuingilia jambo dogo kama hili hawezi kuingia mtego wa kubishania neno dhaifu tena katika nchi ya watu maskini na wanyonge. Yuko busy tuletea maendeleo wananchi.
Tukutane 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo hoja za CAG ziko wapi hapo?

Anyway, Ndugai hajui maana ya Separation of power, asijaribu kuuingiza mhimili wa serikali katika hili suala.
CAG hakusema Rais ni dhaifu alisema "Bunge lina udhaifu" na wala hakusema bunge ni dhaifu.

Ndugai apambane na hali yake!. Asitafute huruma ya Magufuli.
Anasema kikatiba hakuna mtu wa kumwambia ajielezee kwa mtu mwingine iwe rais au nani. Kama Ndugai anavotaka akajieleze kwa rais.

Zaidi iundwe tume ya kuchunguza.

Ngoma nzito hii. Ndugai ataumbuka
 
Kwa jicho pana Rais yupo nyuma ya Spika.

Mwaka jana alipokea Live ripoti ya CAG na kuichambua madudu kadhaa yaliyoainishwa.

Mwaka huu ni kama hajui kuna ripoti ipo, aliipokea kimya kimya na sekeseke linaloendelea ni kama hasikii.

Siku zote Rais tulie nae kitu anachopinga huwa hanyamazi maana hana kariba ya kujizuia. Ila kwa hili kanyamaza. Ipo sababu.

Hapa ndipo tunasema kwa jicho pana magufuli anamsapoti ndugai, maana madudu yote ni ya uongozi wake, 1.5 trilion, zisizofahamika matumizi ni awamu yake.

Manunuzi yasiofata sheria, zabuni na kadhalika, magufuli apendi kusemwa, anaamini yeye anajua kila kitu. Na ana uwezo wa kila kitu ilimradi tu yeye ni Rais. Kauli zake nyingi huthibitisha hilo.

Sasa anasaka kichwa cha CAG na uwezo wa kukipata hana. Sasa anamtumia yule dhaifu bungeni kufikia lengo.

Rudia kauli ya dhaifu jana. "Eti" CAG akajisalimishe kwa Rais. Na ajiuzuru. Hii ndio nia ya Dhati ya Magufuli, Assad aondoke maana ni kikwazo kwake

Magufuli hapendi kukosolewa wote mnajua ya Lissu, wote mnajua ya Wapinzani leo, wote mnajua kilichompata msajili wa hazina alipotoa maoni ya wazi clouds 360 kuwa kuweka fedha za umma bank kuu kutapunguza mzunguko wa fedha na si kosa kisheria kuweka katika mabenki ya kawaida, aliliwa kichwa.
Dumelang
 
65 Reactions
Reply
Back
Top Bottom