CAG: Mkandarasi alichukua tenda kwa 104b akaiuza kwa 40b akapiga cha juu 64b

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,180
103,672
Namnukuu CAG Kichere

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari iliingia mkataba na “Mkandarasi Mkuu” wa shilingi bilioni 172.36 tarehe 3 Agosti 2019 wa muda wa mwaka mmoja hadi kufikia mwezi Agosti 2020 kwa ajili ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia meli katika bandari ya Tanga, kufanya tathmini ya athari za kimazingira, na kununua vifaa kwa ajili ya shughuli za bandari. Kwa kulingana na mkataba, gharama ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia meli katika Bandari ya Tanga ilikuwa ni shilingi bilioni 104.92 (asilimia 60 ya bei yote ya mkataba).

Hata hivyo, mnamo tarehe 1 Agosti 2019, “Mkandarasi Mkuu” iliingia makubaliano na “Mkandarasi Mbia” kwa ajili ya kazi ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia Meli kwa bei ya mkataba dola
za marekani milioni 18.15 sawa na shilingi bilioni 40.46 kwa kipindi cha miezi 11 bila kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari. Pia “Mkandarasi Mkuu” aliingia mkataba na “Mkandarasi Mbia” hata kabla ya kusaini mkataba wake na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Kuingia mkataba bila kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Bandari ilikuwa ni kinyume na Kifungu Kidogo cha 4.4 cha Masharti ya Jumla ya Mkataba kati ya Mamlaka ya Bandari na Mkandarasi Mkuu ambacho
kinaizuia Mkandarasi Mkuu kutoa sehemu ya kazi kwa Mkandarasi mwingine, na ikiwa kunauhitaji wa kutoa kazi kwa Kampuni nyingine kutekeleza kazi zilizoko kwenye mkataba, Mkandarasi Mkuu anapaswa kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Bandari siku 28 kabla ya kutoa kazi hiyo.

Aidha, nilibaini jumla ya malipo yaliyolipwa kwa kazi ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia Meli yalikuwa dola za
marekeni milioni 18.22 sawa na shilingi bilioni 40.62, kiasi hiki, pia, kinajumuisha malipo ya dola za marekani 73,824 sawa na shilingi milioni 164.55 kwa huduma za wakala wa meli kwa “Mkandarasi mbia”. Ulinganifu wa kiasi kilichotozwa na Mkandarasi Mkuu shillingi bilioni 104.92 na kiasi alicholipwa na “Mkandarasi mbia”
shilingi bilioni 40.62 inaonesha Kiasi kilichotozwa na Mkandarasi Mkuu kimezidi kiasi halisi kilichotumika kufanya malipo ya kazi hiyo kwa shilingi bilioni 64.30.

My Take
Msimamo wangu ni uleule,kwa mwendo huu ni bora nchi ikauzwa kila mtu achukue chake ajue anafanya nini. Inatia uchungu sana
 
Namnukuu CAG Kichere

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari iliingia mkataba na “Mkandarasi Mkuu” wa shilingi bilioni 172.36 tarehe 3 Agosti 2019 wa muda wa mwaka mmoja hadi kufikia mwezi Agosti 2020 kwa ajili ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia meli katika bandari ya Tanga, kufanya tathmini ya athari za kimazingira, na kununua vifaa kwa ajili ya shughuli za bandari. Kwa kulingana na mkataba, gharama ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia meli katika Bandari ya Tanga ilikuwa ni shilingi bilioni 104.92 (asilimia 60 ya bei yote ya mkataba).

Hata hivyo, mnamo tarehe 1 Agosti 2019, “Mkandarasi Mkuu” iliingia makubaliano na “Mkandarasi Mbia” kwa ajili ya kazi ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia Meli kwa bei ya mkataba dola
za marekani milioni 18.15 sawa na shilingi bilioni 40.46 kwa kipindi cha miezi 11 bila kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari. Pia “Mkandarasi Mkuu” aliingia mkataba na “Mkandarasi Mbia” hata kabla ya kusaini mkataba wake na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).
Kuingia mkataba bila kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Bandari ilikuwa ni kinyume na Kifungu Kidogo cha 4.4 cha Masharti ya Jumla ya Mkataba kati ya Mamlaka ya Bandari na Mkandarasi Mkuu ambacho
kinaizuia Mkandarasi Mkuu kutoa sehemu ya kazi kwa Mkandarasi mwingine, na ikiwa kunauhitaji wa kutoa kazi kwa Kampuni nyingine kutekeleza kazi zilizoko kwenye mkataba, Mkandarasi Mkuu anapaswa kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Bandari siku 28 kabla ya kutoa kazi hiyo.
Aidha, nilibaini jumla ya malipo yaliyolipwa kwa kazi ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia Meli yalikuwa dola za
marekeni milioni 18.22 sawa na shilingi bilioni 40.62, kiasi hiki, pia, kinajumuisha malipo ya dola za marekani 73,824 sawa na shilingi milioni 164.55 kwa huduma za wakala wa meli kwa “Mkandarasi mbia”. Ulinganifu wa kiasi kilichotozwa na Mkandarasi Mkuu shillingi bilioni 104.92 na kiasi alicholipwa na “Mkandarasi mbia”
shilingi bilioni 40.62 inaonesha Kiasi kilichotozwa na Mkandarasi Mkuu kimezidi kiasi halisi kilichotumika kufanya malipo ya kazi hiyo kwa shilingi bilioni 64.30.

My Take
Msimamo wangu ni uleule,kwa mwendo huu ni bora nchi ikauzwa kila mtu achukue chake ajue anafanya nini. Inatia uchungu sana
Mbaya zaidi wewe masikini unajikunja na kibiashara chako ili siku moja uinuke lakini unakumbana na tozo na kodi kibao huku hao wanaokutoza huo mlolongo wa kodi ndiyo hawa. Wanaiba wanajenga ma-lodge na majumba ya kutisha wanakuja kutamba mtaani. Inaumiza na kutia uchungu sana...na hawafanywi cho chote japo wanajulikana...

Swali ni je; tutafanyeje kama taifa kupambana na hali hii wakati jamii yenyewe inaabudu hawa mafisadi wenye pesa? Kuna matumaini?
 
Mbaya zaidi wewe masikini unajikunja na kibiashara chako ili siku moja uinuke lakini unakumbana na tozo na kodi kibao huku hao wanaokutoza huo mlolongo wa kodi ndiyo hawa. Wanaiba wanajenga ma-lodge na majumba ya kutisha wanakuja kutamba mtaani. Inaumiza na kutia uchungu sana...na hawafanywi cho chote japo wanajulikana...

Swali ni je; tutafanyeje kama taifa kupambana na hali hii wakati jamii yenyewe inaabudu hawa mafisadi wenye pesa? Kuna matumaini?
Wanasiasa ni mchwa hatari sana kutafuna keki ya Taifa kuliko taasisi zote za serikalini.

Ila wanavyonifurahishaga hapa wale wanaolipwa kuchafua TRA, POLICE, BANDARI n.k huwa sina mbavu kabisa
 
Namnukuu CAG Kichere

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari iliingia mkataba na “Mkandarasi Mkuu” wa shilingi bilioni 172.36 tarehe 3 Agosti 2019 wa muda wa mwaka mmoja hadi kufikia mwezi Agosti 2020 kwa ajili ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia meli katika bandari ya Tanga, kufanya tathmini ya athari za kimazingira, na kununua vifaa kwa ajili ya shughuli za bandari. Kwa kulingana na mkataba, gharama ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia meli katika Bandari ya Tanga ilikuwa ni shilingi bilioni 104.92 (asilimia 60 ya bei yote ya mkataba).

Hata hivyo, mnamo tarehe 1 Agosti 2019, “Mkandarasi Mkuu” iliingia makubaliano na “Mkandarasi Mbia” kwa ajili ya kazi ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia Meli kwa bei ya mkataba dola
za marekani milioni 18.15 sawa na shilingi bilioni 40.46 kwa kipindi cha miezi 11 bila kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari. Pia “Mkandarasi Mkuu” aliingia mkataba na “Mkandarasi Mbia” hata kabla ya kusaini mkataba wake na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).
Kuingia mkataba bila kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Bandari ilikuwa ni kinyume na Kifungu Kidogo cha 4.4 cha Masharti ya Jumla ya Mkataba kati ya Mamlaka ya Bandari na Mkandarasi Mkuu ambacho
kinaizuia Mkandarasi Mkuu kutoa sehemu ya kazi kwa Mkandarasi mwingine, na ikiwa kunauhitaji wa kutoa kazi kwa Kampuni nyingine kutekeleza kazi zilizoko kwenye mkataba, Mkandarasi Mkuu anapaswa kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Bandari siku 28 kabla ya kutoa kazi hiyo.
Aidha, nilibaini jumla ya malipo yaliyolipwa kwa kazi ya kuongeza kina cha lango na sehemu ya kugeuzia Meli yalikuwa dola za
marekeni milioni 18.22 sawa na shilingi bilioni 40.62, kiasi hiki, pia, kinajumuisha malipo ya dola za marekani 73,824 sawa na shilingi milioni 164.55 kwa huduma za wakala wa meli kwa “Mkandarasi mbia”. Ulinganifu wa kiasi kilichotozwa na Mkandarasi Mkuu shillingi bilioni 104.92 na kiasi alicholipwa na “Mkandarasi mbia”
shilingi bilioni 40.62 inaonesha Kiasi kilichotozwa na Mkandarasi Mkuu kimezidi kiasi halisi kilichotumika kufanya malipo ya kazi hiyo kwa shilingi bilioni 64.30.

My Take
Msimamo wangu ni uleule,kwa mwendo huu ni bora nchi ikauzwa kila mtu achukue chake ajue anafanya nini. Inatia uchungu sana
Inawezekaneje mkandarasi akalipwa hela yote hata kabla hajaanza wala kumaliza kazi?

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwenye katiba mpya kuwekwe kifungu kitakacho sema wazi na kueleweka ni mazingira gani ya kufuru ya kiutendji wa serikali iliyopo madarakani ambayo yakifikiwa na uongozi wa nchi wa kiraia wa vyama vya kisiasa basi nchi iongozwe na Military Junta angalau kwa miaka miwili kama kipindi cha mpito. Wakati huo wa kipindi hiki cha mpito vyama vya kisiasa vifanyiwe overhaul ya kutosha.

Hii demokrasia ya vyama vya siasa ilipofikia lazima ifungiwe speed gavana.
 
Halafu Kuna mbuzi zinasema JPM aliondoa upigaji, awamu ya JPM ilikuwa na upigaji ambao haijawahi kutokea tangu Tanzania ianze, alikuwa anahadaa watanzania kwa kutembea akitukana mabarabarani as if anapambana na ufisadi, aliowatumbua wote ni wale "waliomruka" kwenye mipango, mkuu wa mamlaka ya bandari alikuja kutimuliwa na mama Samia, JPM alimtunza
 
Mbaya zaidi wewe masikini unajikunja na kibiashara chako ili siku moja uinuke lakini unakumbana na tozo na kodi kibao huku hao wanaokutoza huo mlolongo wa kodi ndiyo hawa. Wanaiba wanajenga ma-lodge na majumba ya kutisha wanakuja kutamba mtaani. Inaumiza na kutia uchungu sana...na hawafanywi cho chote japo wanajulikana...

Swali ni je; tutafanyeje kama taifa kupambana na hali hii wakati jamii yenyewe inaabudu hawa mafisadi wenye pesa? Kuna matumaini?
Wanakula mbususu tuu pale alafu wanakwambia kijana tafuta hela🤣🤣🤣🤣
 
C&P kutoka hapa hapa JF


Mafisadi wenzie. Hakuna sheria nchini kwamba wezi wanaporudisha kile walichoiba basi hawafunguliwi mashtaka lakini Mkwere hakuwapandisha wezi wa $133 million za EPA kwa kudai kuwa pesa zile asilimia kubwa wamezirudisha pamoja na kuwa hakutoa uthibitisho wowote wa kurudishwa kwa pesa zile.


Rada walikwapua $42 million na hakuna hata mmoja aliyepandishwa kizimbani. Yule mhindi aliyekuwa rumande aliachwa atoroke katika mazingira ya kutatanisha na wahusika wengine wote waliopata mgao hawakuguswa na mkono wa sheria mpaka leo wanapeta na pesa za wizi uraiani.

Mabilioni ya Uswiss uchunguzi bado unaendelea tangu June 2012 na Mkwere hajatia neno hata siku moja na si ajabu "uchunguzi" utaendelea hata baada ya awamu yake kwisha. Cha ajabu hizo bank accounts zote wenye nazo bado wanaendelea kutoa hizo pesa za wizi na mpaka sasa wameshatoa zaidi ya Tshs 40 billion.


Meremeta walichota $155 million na Kagoda pia walichota mapesa chungu nzima na kudai ni siri kubwa za Serikali hivyo wizi ule hauwezi kujadiliwa Bungeni.

Acheni kutaka kupindisha ukweli ili kuwatetea hawa wezi wakubwa na mafisadi waliojivisha ngozi ya uongozi ambao wanakwapua mapesa chungu nzima ya walipa kodi miaka nenda miaka rudi.
 
C&P kutoka hapa japa JF


Mafisadi wenzie. Hakuna sheria nchini kwamba wezi wanaporudisha kile walichoiba basi hawafunguliwi mashtaka lakini Mkwere hakuwapandisha wezi wa $133 million za EPA kwa kudai kuwa pesa zile asilimia kubwa wamezirudisha pamoja na kuwa hakutoa uthibitisho wowote wa kurudishwa kwa pesa zile.


Rada walikwapua $42 million na hakuna hata mmoja aliyepandishwa kizimbani. Yule mhindi aliyekuwa rumande aliachwa atoreke katika mazingira ya kutatanisha na wahusika wengine wote waliopata mgao hawakuguswa na mkono wa sheria mpaka leo wanapeta na pesa za wizi uraiani.

Mabilioni ya Uswiss uchunguzi bado unaendelea tangu June 2012 na Kikwete hajatia nenio hata siku moja na sia ajabu "uchunguzi" utaendelea hata baada ya awamu yake kwisha. Cha ajabu hizo bank accounts zote wenye nazo bado wanaendelea kutoa hizo pesa za wizi na mpaka sasa wameshatoa zaidi ya Tshs 40 billion.


Meremeta walichota $155 million na Kagoda pia walichota mapesa chungu nzima na kudai ni siri kubwa za Serikali hivyo wizi ule hauwezi kujadiliwa Bungeni.

Acheni kutaka kupindisha ukweli ili kuwatetea hawa wezi wakubwa na mafisadi waliojivisha ngozi ya uongozi ambao wanakwapua mapesa chungu nzima ya walipa kodi miaka nenda miaka rudi.
Hakuna mwenye afadhali kumtetea kiongozi yeyote wa ccm aliye hai au aliye kufa ni sawa na kupiga kofi upepo huo ubadhirifu imefanyika wakati wa mwendazake na kila aliyepita anayake na ajae pia anayake kwaiyo kumbukumbu nyingi hazisaidii zaidi ya kuwatoa ccm madarakani basi.
 
hapo kwenye malipo mbona kama mimi sijaelewa,tafadhali alieelewa anifafanulie mbona kama sioni kiasi chochote kilichozidi?
 
My Take
Msimamo wangu ni uleule,kwa mwendo huu ni bora nchi ikauzwa kila mtu achukue chake ajue anafanya nini. Inatia uchungu sana.


Nchi huwa inauzwa wapi mkuu, namaanisha soko lake liko wapi



YESU NI BWANA
Nchi haiuziki hii, chawa wengi sana. Halafu chawa wenyewe hawana lolote
 
Back
Top Bottom