CAG: Hali ya Magereza ni mbaya, wafungwa wanalala vyumba vya mabati, nyumba za maofisa nazo zimechoka

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,458
Wafungwa.JPG
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere amesema ukaguzi ulihakiki majengo ya makazi ya magereza na kubaini kuwa mengi ni chakavu na yanahitaji ukarabati mkubwa.

“Hali mbaya zaidi ilibainika katika magereza ya kilimo ambapo wafungwa walikuwa wakilala katika vyumba zilivyojengwa kwa mabati. Hali hii ilibainika katika Magereza ya Kilimo ya Ushora na Kingurungundwa,” - CAG.

Bweni la wafungwa la Kilimo ya Ushora lilipigwa picha na kuonekana likiwa limezungushiwa mabati yanatoonekana kuchoka.

Ameongeza kuwa: “Nyumba nyingi za wafanyakazi wa magereza zilizotembelewa zilikuwa katika hali mbaya kwa sababu ya ukosefu wa matengenezo na ukarabati. Nyumba za watumishi wa magereza zilikosa maji safi na ya kutosha.

“Mifumo ya majitaka ilikuwa chakavu na mingi ilikuwa ikivuja. Hali hii ilibainika katika magereza sita ambayo ni magereza makuu ya Keko na Butimba; Magereza ya Wilaya za Kilwa, Manyoni, na Ukerewe; na Magereza ya kilimo ya Kingurungundwa na Kwa Mngumi.

“Jeshi la Magereza halikuwa na mipango ya matengenezo ili kusaidia shughuli zake za ukarabati wa majengo na hakukuwa na bajeti iliyotengwa kwa madhumuni ya ukarabati na matengenezo.

“Kutokana na ukarabati na matengenezo hayo ya miundombinu ya magereza kukosa bajeti, shughuli hizo ziliachwa kwa magereza husika ambapo ukarabati ulifanyika kwa kutumia vyanzo vya fedha vya ndani ya magereza husika.

“Pia, kutokana na ufinyu wa fedha, ukaguzi ulibaini kuwa kwa magereza yote 15 yaliyotembelewa, kiasi cha shilingi milioni 38 kilipelekwa kwa magereza husika kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za askari isipokuwa Wilaya ya Ukerewe iliyopokea shilingi milioni 76 kutokana na hali ya nyumba za maofisa wa magereza kuwa mbaya zaidi.

“Imeelezwa kuwa, fedha zilizotolewa zilitoka katika vyanzo mbalimbali kama vile faida iliyotokana na miradi ya uwekezaji inayotekelezwa na Jeshi la Magereza nchi nzima.”
 
Wengi wa wafungwa hawatakiwi kuwa humo, waanze kuwapunguza, na kwa utaratibu mzuri bila kuwatumia wafungwa vibaya au kuwaonea magereza wanaweza kuwa wazalishaji wakubwa sana wakiamua na itaweza kusaidia budget zao kama kutakuwa na guidelines nzuri za matumizi ya pesa zitakazo patikana
 
Halafu %kubwa ya wafungwa wako gerezani Kwa kuonewa tu.
Lakini anaye waonea ni nani kama sisi kwa sisi binadamu tumekuwa wabaya sana mtu unamsingizia mtu kakufanyia kitu anafungwa sijui unajisikiaje na hasa akishindwa kujitetea kuwa hajafanya kosa ndiyo basi tena
 
Wengi wa wafungwa hawatakiwi kuwa humo, waanze kuwapunguza, na kwa utaratibu mzuri bila kuwatumia wafungwa vibaya au kuwaonea magereza wanaweza kuwa wazalishaji wakubwa sana wakiamua na itaweza kusaidia budget zao kama kutakuwa na guidelines nzuri za matumizi ya pesa zitakazo patikana
kipindi Cha magufuli kulikuwa na ongezeko kubwa la wafungwa,kiasi haijawai kutokea tangu tupate Uhuru,

Yule mzee nadhani alitaka watu wote wawe jela,uraini abakie yeye tu na kina bashite,huyu mama amejitaidi Sana kupunguza wafungwa na mahabusu
 
..kama askari magereza wanaishi ktk mazingira mabaya namna hiyo kwanini jeshi la magereza linajenga makao makuu mapya ya kifahari mjini Dodoma?
 
Ndo viongoz wasilaaniwe kweli? Kumbuka wanaoteseka wengine walisingiziwa tu mule
 
Halafu askari magereza nao ifikie kipindi wajitambue hivi mnaishi maisha ya hovyo namna hiyo halafu unakuta mnakuwa wanoko na mna waonea sana wafungwa hizo roho mbaya kwanini msitumie kui force serikali iboreshe maisha yenu huko mlipo???acheni kuonea wafungwa.
 
Back
Top Bottom