CAG azungumzia kukaguliwa na Bunge la Tanzania, bajeti ya 2019/20

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Dar es Salaam. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Profesa Mussa Assad amesema siyo jambo jipya ofisi yake kufanyiwa ukaguzi, akisema hatua hiyo hufanyika kila mwaka na taarifa kuwasilishwa Kamati ya Bunge la Hesabu za Serikali (PAC).

Profesa Assad alisema hayo jana Jumanne Juni 13, 2019 wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha Azam.

Alisema baada ya kukamilika kwa ripoti hiyo ya ukaguzi, huwasilishwa kwa kamati hiyo kabla ya kusomwa bungeni.

“Tunakaguliwa kila mwaka na mkaguzi wetu kama kawaida atateuliwa na PAC ya Bunge atafanya kazi yake, akimaliza atatoa ripoti na kuitazama sisi na kusainiwa na audit committee halafu hesabu hizo zitapelekwa kwa mwenyekiti wa PAC ili kusoma bungeni.”

“Hayo ni mambo ya kawaida kabisa katika utendaji wa taasisi yetu na siyo jambo jipya, ni matakwa ya kisheria,” alisema Profesa Assad.

Mei 16, 2019, Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai alitoa taarifa bungeni kwamba kwa mujibu wa sheria ya ukaguzi wa umma, hesabu za ofisi ya CAG zinakaguliwa na Bunge kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).
 
Dar es Salaam. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Profesa Mussa Assad amesema siyo jambo jipya ofisi yake kufanyiwa ukaguzi, akisema hatua hiyo hufanyika kila mwaka na taarifa kuwasilishwa Kamati ya Bunge la Hesabu za Serikali (PAC).

Profesa Assad alisema hayo jana Jumanne Juni 13, 2019 wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha Azam.

Alisema baada ya kukamilika kwa ripoti hiyo ya ukaguzi, huwasilishwa kwa kamati hiyo kabla ya kusomwa bungeni.

“Tunakaguliwa kila mwaka na mkaguzi wetu kama kawaida atateuliwa na PAC ya Bunge atafanya kazi yake, akimaliza atatoa ripoti na kuitazama sisi na kusainiwa na audit committee halafu hesabu hizo zitapelekwa kwa mwenyekiti wa PAC ili kusoma bungeni.”

“Hayo ni mambo ya kawaida kabisa katika utendaji wa taasisi yetu na siyo jambo jipya, ni matakwa ya kisheria,” alisema Profesa Assad.

Mei 16, 2019, Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai alitoa taarifa bungeni kwamba kwa mujibu wa sheria ya ukaguzi wa umma, hesabu za ofisi ya CAG zinakaguliwa na Bunge kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).
Sasa Mbona Bw. Nduu aliongea akasema CAG hakaguliwagi ndo wameanza now?
 
Sasa Mbona Bw. Nduu aliongea akasema CAG hakaguliwagi ndo wameanza now?
... siasa tu hizo Mkuu! Kwenye mambo ya kitaalamu na kisheria wanaletaga siasa na mizaha isiyo na maana. Ona jinsi Prof Assad alivyolizungmzia kumbe ni kitu cha kawaida na kinafanyika kila mwaka.
 
Hapo kwenye ukaguzi ndio mtego ulipo wa kumchomoa kutoka kwenye kiti. Assad hutakiwi kwa sababu sio mnafki na hutaki kutumika kisiasa, pia kuonesha ufisadi wa chama tawal na sirikali kuu bila kupepesa imewakera, mfano ni ile 1.5 T.
 
Tutamkumbuka huyu CAG, msemakweli ni mpenzi wa Mungu kumbe kwa jiwe msemakweli ni adui wa CCM
 
Spika alitaka kutuaminisha kuwa CAG hakaguliwi ....!!

Au alitaka kutusahaulisha ile 1.5 Trillion, ambayo inadaiwa inazidi kuongezeka ..........!!
 
Ripoti ya ukaguzi alikuwa anaitengeneza CAG mwenyewe pasipokukagauliwa, Mungu mbariki Ndugai!
We ni kilaza tu...kama hata baada ya kutumia lugha nyepesi hujamuelewa Prof Assad wewe ni hasara.
Hata hivyo Prof Assad sio level yako wewe wala Ndugai...Mungu ambariki huyu mzee
 
Niko huku nyumbani kwa Mh. Heche hakuna choo, wanakunya vichakani na ndiyo utamaduni, kuchimba choo ni mkosi kwenye familia kama vile mtoto kutanguliza miguu au makalio!
 
Back
Top Bottom