Cag apewe na wananchi tujue taarifa za wabunge wanakaa siku ngapi majimboni

Zing

JF-Expert Member
Jun 24, 2009
1,767
470
Kuna haja ofisi ya CAG kuwa na wajibu
  • kuwa na register kujua wabunge walizitumia ofisi zao wilayani na mkoni kwa siku ngapi katika mwaka

Ukioadoa wale wabunge wa mijini na Dar Hivi katika siku 365 za mwaka kuna mbunge hata mmoja amabye anatumia japo siku 60 kuwa kwenye wilaya ya jimbo lake?
 
Labda tuanzie hapa, kisheria au kikanuni, mbunge anatakiwa kukaa jimboni kwake kwa siku ngapi kwa mwaka? Vinginevyo hili liko nje ya mikono ya CAG na mamlaka nyingine.
 
Elimu kwa umma ndio suluhisho la hili tatizo. Wapiga kura waelimishwe kwamba Mbunge wao kazi yake ni kuwawakilisha na hivyo anapaswa kuwa nao karibu na kuwatembelea mara kwa mara na kujua shida zao ili aziwakilishe bungeni. Kama Mbunge hataonekana mara kwa mara jimboni hadi siku karibia na uchaguzi basi wanapiga kura wampige chini. Kwa sasa kuna tatizo la wabunge kutokaa jimboni na wengi maisha yao ni Dar!
 
Hakuna sheria, kanuni wala taratibu zinazomlamisha mbunge kukaa jimboni siku 365.
 
CAG nae ni walewale sasa unadhani nini kitatokea? Yemwenyewe CAG anastahili hati chafu kwani serikali huwa inamwingilia kazi zake mara kibao na kuforce matokeo ya ukaguzi.
 
Moderator wana sababu gani kuhamisha hii thread kutoka kwenye siasa?
 
Elimu kwa umma ndio suluhisho la hili tatizo. Wapiga kura waelimishwe kwamba Mbunge wao kazi yake ni kuwawakilisha na hivyo anapaswa kuwa nao karibu na kuwatembelea mara kwa mara na kujua shida zao ili aziwakilishe bungeni. Kama Mbunge hataonekana mara kwa mara jimboni hadi siku karibia na uchaguzi basi wanapiga kura wampige chini. Kwa sasa kuna tatizo la wabunge kutokaa jimboni na wengi maisha yao ni Dar!

Lakini kumpiga chini haisadii kuondoa la matumizi mabaya ya pesa za walipa kodi kuna wabunge kama kina Sitta ofisi zao zimetumia mamilini kukarabati. e walizingatia ni siku ngapi watatumia ofisi hizo?

Wabunge wengine ndio hivyo ofisi zao hata samani zimeagizwa kutoka china wakati ni majimbo yana mbao na mfundi seremala na wabunge hao wanajuwa wazi watakuwa busy na kamati za bunge kuliko kuwa busy kwenye ofisi za majimbo.
 
Back
Top Bottom