ABC ZA 2025
JF-Expert Member
- May 2, 2018
- 1,160
- 706
Kazi iendelee | Soka liendelee,
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka kwa niaba ya CCM na kwaniaba ya Mkt wa CCM Taifa ambae pia Rais wa JMT Mhe Samia Suluhu Hassan.
Wamezitakia heri na baraka timu nne zitakazopeperusha bendera ya Tanzania kwenye mashindano ya Kombe la Shirikisho na baadae Club-Bingwa Africa hapo mwakani.
CCM ndio chama pekee kilichobeba agenda ya michezo na wanamichezo kisawasawa hili Tanzania inajua na dunia inajua, kwani CCM inaamini michezo ni ajira, michezo ni kazi kama kazi zingine na nia ya CCM nikufikia kazi|ajira 8M ifikapo mwaka 2025 hivyo huwezi kuitenga CCM na michezo kama chanzo cha ajira hasa kwa Vijana wa Kitanzania.
Tanzania ni miongoni mwanchi 12 tu zitakazopeleka timu nne kwa pamoja kwenye mashindano hayo ya CAF ambapo timu mbili zitacheza kombe la Shirikisho na timu mbili zitacheza Club Bingwa Africa huku Simba SC wao wakiwatayari wamefuzu hii ni kazi ya CCM na nimatokeo ya Uongozi mahiri na imara wa Rais Samia Suluhu Hassan.
View attachment 1944275
Rais Samia atoa wastani wa madarasa manne na madawati 120 katika kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima | Hakika awamu ya Sita Tanzania lazima iwe Tanzania.
" Hakuna kama Samaia "
Baada ya janga la Covid-19 kuvuruga Uchumi wa dunia na sisi tukiwemo, Shirika la fedha duniani ( IMF) pamoja na benki ya dunia ( WB) wameanza kuzisaidia nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania mikopo yenye masharti nafuu ili pesa hizo zitumike kama Economic Stimulus & Relief Fund na hapa muelewe vizuri Tanzania tunapokea mikopo na misaada ila "HATUITEGEMEI " ndio maana hata kwenye bajeti yetu hii ya FY2021|22 katia ya Tshs 36.33trl zilizotengwa pesa zetu ni 91.9% huku misaada na mikopo ikiwa ni 8.1% tu,
IMF tayari imeisaidia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu kiasi cha Tshs 1.3trl kwaajili ya kusisimua Uchumi wake uliodorora kwasababu ya covod-19 kwani niukweli usiopingika Tanzania tumeumizwa zaidi kwenye Sekta za Utalii,biashara na Usafirishaji,
Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutumia pesa hizo na baada ya kutoa madarasa ya kisasa elfu 15 sawa na wastani wa madarasa manne kwenye kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima huku kipaumbele kikiwa ni shule zenye upungufu wa madarasa lakini furaha iliyoje Rais wetu ametoa tena jumla ya madawati 462,795 ambayo ni sawa na Wastani wa madawati 120 kwenye kila Shule ya Sekondari nchi nzima ambazo jumla ya shule hizo ni 3,863.
Sababu za Rais Samia Suluhu Hassan kutoa madarasa mapya manne ya kisasa na madawati mapya 120 katika kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima ni kuhakikisha wazazi wa watoto watakaojiunga na kidato cha kwanza mwakani katika mwaka wa masomo 2021|2025 hawalipi hata Shilingia mia moja kwani Rais wetu mnyenyekevu ameshalipa pia ada za watoto wote 1M wanaotakiwa kuanza shule siku moja nchi nzima yaani trh 06|01|2022,hii haijawahi kutokea katika historia ya nchi yetu,
VIVA SAMIA VIVA || VIVA TANZANIA VIVA
View attachment 1971181
Anawezaje haya yote huyu mama?
SGR TZS 10.2T ni Yeye,
SG TZS 6.55T ni Yeye
Madarasa mapya manne kila sekondari nchi nzima,
Madawati 120 kila sekondari nchi nzima