Mbu JF-Expert Member Jan 11, 2007 12,753 7,844 Dec 30, 2008 #1 ...kwaheri 2008 if i could change back the hands of time,... ningetumia muda kuwa karibu zaidi na rafiki yangu aliotangulia mbele ya haki... wewe je?
...kwaheri 2008 if i could change back the hands of time,... ningetumia muda kuwa karibu zaidi na rafiki yangu aliotangulia mbele ya haki... wewe je?
Kibunango Platinum Member Aug 29, 2006 8,420 2,271 Dec 30, 2008 #2 Attachments Friends-kingdom_04.jpg 38.5 KB · Views: 103
K Kjnne46 Member Dec 4, 2006 69 2 Dec 31, 2008 #3 TATHMINI MWAKA MPYA 1430 HIJRIAH Mwaka mpya umeingia Moja Nne Tatu Sifuri Hijriah Waumini Yatupasa Kuzingatia Nguzo za Uislamu Nitakutajia! Shahada ni Egemeo la Kuanzia Kisha Swala na Zakati Kufuatia Swaumu ya Ramadhani Inapotujia Mwezi Mmoja Kufunga Imefaradhia! Nayo Hijja Faradhi mara moja pia Kwa Muislamu mwenye uwezo na nia Uwezo Kiafya na Pesa za Kusafiria Na Familia Mahitaji Tosha Kuwaachia! Makkah kwanza na Minah Kuhirimia Arafah na Muzdalifah nazo Kupitia Jamaraat Shetani Mawe Kumtupia Nae Mnyama Kuchinja Hijja Kumalizia! Muharram Mwezi Mosi Ikiwadia Tukae Misikitini Vikundi kufikiria Mwaka Jana Mambo gani Tuliazimia Tuchuje mafanikio na Yale Yaliyosalia! Hijriah Mjo Wake Unakumbushia Kurejea Madhambi Tuliyotenda Kutorudia Kwa Dhati ya Moyo Ima Kutubia Ibilisi Mwaka Mpya budi Kumkimbia! Maendeleo ya Uislamu Mikakati Kuipangia Awali ni ELIMU ya Dini na Dunia Vyuo Vikuu Watoto Fursa Kuzitumia Ummah wetu Kunufaika Wakihitimia! Turatibu Taaluma kwa Zote Jinsia Kilimo na Mali Asili Kuvikazania Mazao ya Biashara Viwe Ndio Njia Ya Waislamu Maendeleo Kuwafikia! Ya-Rabi Tunakuomba Kutujaalia Tuendako Tuweze Maisha Kupalilia Tushikamane TAQWa Peponi Kujitayarishia Waja Wako Dua Maridhawa Takabalia! A A M I I N! A A M I I N!! ___________________________________
TATHMINI MWAKA MPYA 1430 HIJRIAH Mwaka mpya umeingia Moja Nne Tatu Sifuri Hijriah Waumini Yatupasa Kuzingatia Nguzo za Uislamu Nitakutajia! Shahada ni Egemeo la Kuanzia Kisha Swala na Zakati Kufuatia Swaumu ya Ramadhani Inapotujia Mwezi Mmoja Kufunga Imefaradhia! Nayo Hijja Faradhi mara moja pia Kwa Muislamu mwenye uwezo na nia Uwezo Kiafya na Pesa za Kusafiria Na Familia Mahitaji Tosha Kuwaachia! Makkah kwanza na Minah Kuhirimia Arafah na Muzdalifah nazo Kupitia Jamaraat Shetani Mawe Kumtupia Nae Mnyama Kuchinja Hijja Kumalizia! Muharram Mwezi Mosi Ikiwadia Tukae Misikitini Vikundi kufikiria Mwaka Jana Mambo gani Tuliazimia Tuchuje mafanikio na Yale Yaliyosalia! Hijriah Mjo Wake Unakumbushia Kurejea Madhambi Tuliyotenda Kutorudia Kwa Dhati ya Moyo Ima Kutubia Ibilisi Mwaka Mpya budi Kumkimbia! Maendeleo ya Uislamu Mikakati Kuipangia Awali ni ELIMU ya Dini na Dunia Vyuo Vikuu Watoto Fursa Kuzitumia Ummah wetu Kunufaika Wakihitimia! Turatibu Taaluma kwa Zote Jinsia Kilimo na Mali Asili Kuvikazania Mazao ya Biashara Viwe Ndio Njia Ya Waislamu Maendeleo Kuwafikia! Ya-Rabi Tunakuomba Kutujaalia Tuendako Tuweze Maisha Kupalilia Tushikamane TAQWa Peponi Kujitayarishia Waja Wako Dua Maridhawa Takabalia! A A M I I N! A A M I I N!! ___________________________________