"Bwana Yule" Na Alivyovunja Record Karibu Zote 2016

Msherwa

JF-Expert Member
Aug 4, 2012
1,335
1,225
Katika Mwaka unaoisha leo 2016, Ifuatayo ni list ya Record zilizovunjwa na "Bwana Yule".
Zote zilizopo hapa ni RECORD MPYA ZILIZOVUNJWA (yaani new, weird and UNBELIEVABLE!!)

1. Kwa mara ya kwanza Bwana Yule mpenda maskini akabomoa nyumba za maskini bila hata kifuta machozi.

2. Walioomba Panadol wakaletewa Pangaboi

3. Walioomba mikopo wakapewa makopo

4. Waliotaka kuona bahari wakalazimika kulijua jangwa la Idodomya KWA LAZIMA

5. Mnyama mwenye jina akaipiku thamani ya kila kitu Tanzania. Watu wakasahau vyote wakamfuata hadi ahera alikolala ili wamuulize kama kweli amekufa au karudi South Africa

6. Sheria Thabiti za kuzuia matawi ya maendeleo yaani sekta ya habari na mawasiliano zikatungwa, huku mahakama ya mafisadi ikikosa watuhumiwa kutokana na sheria zenye matundu!

7. Eti akirudi twajificha uvunguni? (Ndio heshima ya baba nyumbani iheshimiwe!)

8. Dangote akatinga magogoni bila hiyana (hanaga mwakilishi yule?)

9. Namba zikarudiwa toka vidudu mpaka chuo kikuu. Wote wakasoma namba kwa sauti!

10. Ondokeni ....... Nimesema Ondokeni ....!! No, No No.... Rudini.. Rudini mitaani machinga!! Nyie ndo wapiga kura!

11. Sitaki kumuona tena Melo na limtandao lake ...!!! (sorry Melo)

Hebu tufunge mwaka kwa kukumbushana tulipofikia ili tupate mwanga wa wapi tutaanzia 2017. Mimi bado naamini TUNAWEZA kwa sababu TULIANZA!!

Religion Must Be Respected It is a Real Father of Most Of US!!

Happy New Year JF!!
 
2016 ni wa aina yake tangu tupate Uhuru!

Huku Tumepigwa Biti tusizungumzie issue ya Faru John wakati wao ndio wametujulisha kupotea kwake na huku kwa Watani wanatupiga Biti tusiongelee la Kupotea kwa Ben Saanane eti atauawa wakati ni wao ndio walitujulisha kupotea kwake!

Inawezekana Faru John alikuwa Mzima amefichwa lakin tulipoanza kuzungumzia Issue yake ndo waliomteka Wakaamua kumuua kabisa ndo sababu na Kamanda wa Anga
Akatupa ushauri ule Muhimu kuhusu Kamanda Ben!!
 
aisee hyo ya sitaki kumwona melo na limtandao lake sijaisikia kabisa,,ilisemwa lini???
 
2016 ni wa aina yake tangu tupate Uhuru!

Huku Tumepigwa Biti tusizungumzie issue ya Faru John wakati wao ndio wametujulisha kupotea kwake na huku kwa Watani wanatupiga Biti tusiongelee la Kupotea kwa Ben Saanane eti atauawa wakati ni wao ndio walitujulisha kupotea kwake!

Inawezekana Faru John alikuwa Mzima amefichwa lakin tulipoanza kuzungumzia Issue yake ndo waliomteka Wakaamua kumuua kabisa ndo sababu na Kamanda wa Anga
Akatupa ushauri ule Muhimu kuhusu Kamanda Ben!!
Hahaha heshima yako kiongozi moja ya watu nawakubali sana hapa jukwaani
 
Watumishi Tanzania wamelipwa malimbikizo yao tena na annual increments zao vizuri sana.

2020 unakuja,
Dai tume huru ewe mtanzania
 
Daaaa kiukwelii nambaa nimeisomaa mwakaa huu eeeeeeeeeeh mungu mwakaa 2017 naombaa usiwee kamaa 2016 maana nitakufaaaa ......................
 
walipoanza kukusanya hela kwa ajiri ya uchaguzi tu!
hela ikaanza kuadimika tangu mwezi wa nane,
mi nilianuka akiwa na miezi mi2 tu
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom