Deogratias Mutungi
Senior Member
- Oct 1, 2019
- 136
- 178
Salaam Wana JF.
Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.
Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.
Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.
Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.
Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?
Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?
Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?
Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.
Deogratias Mutungi
Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.
Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.
Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.
Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.
Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?
Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?
Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?
Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.
Deogratias Mutungi