Bwana harusi apigwa stop kanisani

TIQO

JF-Expert Member
Jan 8, 2011
13,787
2,078
Bwana harusi Chrispin Saadani (34) aliyekuwa akisherekea kufunga ndoa na mchumba ake usiku mwa tar.24 Disemba alijikuta anazuiwa kufunga ndoa na mchumba ake baada ya wanawake wawili alio zaa nao kuibuka gafla kanisa katoliki Jimbo la Sumbawanga huku haamini kilicho tokea.
 
hao wanawake wamekurupuka tu!! Kisheria kama hauna cheti cha ndoa ww co mke wala mume..kama kazaa nao tu hawana haki ya kuzuia ndoa..
Hila huyo jamaa nae duu...alishindwa kuweka mambo sawa kabla ya kuoa..mbona aibu hyo ss
 
Bwana harusi Chrispin Saadani (34) aliyekuwa akisherekea kufunga ndoa na mchumba ake usiku mwa tar.24 Disemba alijikuta anazuiwa kufunga ndoa na mchumba ake baada ya wanawake wawili alio zaa nao kuibuka gafla kanisa katoliki Jimbo la Sumbawanga huku haamini kilicho tokea.

Yasijekuwa yale yale ya kutafuta assurance kama alivyotiririka lara 1. Ninachokijua zuio hilo ni la muda tu kwani ikithibitika kuwa hajawahi kufunga ndoa hakuna anayeweza kumzuia kufunga ndoa na anayemtaka.
 
Last edited by a moderator:
taarifa huyu jamaa alikuwa na wake watatu na wote wanafamiana kati yao wawili walishazaa naye na ndio waliopeleka pingamizi baada kujua anafunga ndoa na bi mdogo wakihoji atawatunzaje hawo watoto
 
Hilo nalo linategemea uthabiti wa Padre aliyekuwa anafungisha ndoa. Kabla ndoa haijafungwa huwa inatangazwa jumapili 3 mfululizo ili kama kuna mwenye pingamizi na aliwasilishe mapema.

Kuruhusu mambo ya namna hii kunawapa nafasi watu kufanya mambo ya kukomoana kwani yawezekana wamefanya hivyo kumkomoa wakijua ameshatumia gharama kufanya maandalizi. Lingine linalonishangaza, siku hizi ukitaka kufunga ndoa, lazima serikali ya mtaa ulioishi kwa miaka mi3 iliyopita itoe uthibitisho kwamba inakufahamu kuwa hujaoa
 
Nilisikia kwenye redio kipindi cha uchambuzi wa magazeti leo asubuhi, duh! Noma sana! lakini wale wanawake walidai walitaka kumkomoa na kutaka kujua hatima ya watoto wao ambapo bwana Chrispin baada ya tukio hilo amehaidi kuwapa mtaji wa laki moja kila mmoja mpka April 25 mwakani,pia ametakiwa kurudisha vitu alivyokuwa amechukua kwa mwanamke mmojawapo aliyetoa kipingamizi.
 
PakaJimmy umeua..
mwenzako alikuwa akifanya siri, na alienda kuolea huko Sumbawanga akijua kuwa mjini kuna wanga wengi, akasahau kuwa SUMBAWANGA NI MWISHO WA MATATIZO.
Ni Krispin gani huyo?
Sio Asprin kweli huyo?
Maana hadi sasa ni kweli anao wake 4, gfsonwin, cacico, Kongosho na Madame B.

Sasa alitaka kumwoa nani mpya tena?
Bahati nzuri hajapita Arusha siku nyingi, hilo shuzi lingetuhusu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom