Ng`wanantogwa
Member
- Aug 14, 2009
- 14
- 5
Kuna tetesi kwamba Bw. Ludovick Utoh amepoteza uwezo na ujasiri wa kuibua ubadhilifu wa fedha za serilkali na kuchunguza usahihi wa matumizi ya fedha za serilkali na mashirika ya umma kwa sababu tayari alishamaliza muda wake na kuongezewa muda mara mbili.
Kwa nafasi ya Bw. Utoh ni mtu anayepaswa kufanya kazi kwa uzalendo mkubwa sana maana watanzania wamempa dhamana kubwa, sijui kama mnafahamu kuna nyazifa kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Rais ana uwezo wa kuteua tu lakini hana uwezo wa kuachisha yeye kama yeye bali itakuwa hivyo kupitia jopo la majaji kadhaa wakiwemo wengine kutoka nchi za jumuiya ya madola? nyazifa hizo ni pamoja na CAG na JAJI MKUU.
Kinachofanyika sasa Bw Utoh anataka kumsaidia na kumfurahisha Mhe, Rais Kikwete na serikali yake isiendelee kupata wakati mgumu lakini vile vile kuongezewa tena muda mwingine pengine amalize kabisa awamu hii ya pili ya JK. Lakini pia tetesi zinasema Bw. Jairo na mhe Rais ni maswahiba wa siku nyingi tangu bwana Jairo akifanyia kazi ikulu pale magogoni.
Ndugu zangu, ikiwa hizi ni tetesi najua fika humu ndani kuna Great thinkers na kuna watu wenye first hand information nitafurahi kusikia zaidi.Nawasilisha.
Kwa nafasi ya Bw. Utoh ni mtu anayepaswa kufanya kazi kwa uzalendo mkubwa sana maana watanzania wamempa dhamana kubwa, sijui kama mnafahamu kuna nyazifa kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Rais ana uwezo wa kuteua tu lakini hana uwezo wa kuachisha yeye kama yeye bali itakuwa hivyo kupitia jopo la majaji kadhaa wakiwemo wengine kutoka nchi za jumuiya ya madola? nyazifa hizo ni pamoja na CAG na JAJI MKUU.
Kinachofanyika sasa Bw Utoh anataka kumsaidia na kumfurahisha Mhe, Rais Kikwete na serikali yake isiendelee kupata wakati mgumu lakini vile vile kuongezewa tena muda mwingine pengine amalize kabisa awamu hii ya pili ya JK. Lakini pia tetesi zinasema Bw. Jairo na mhe Rais ni maswahiba wa siku nyingi tangu bwana Jairo akifanyia kazi ikulu pale magogoni.
Ndugu zangu, ikiwa hizi ni tetesi najua fika humu ndani kuna Great thinkers na kuna watu wenye first hand information nitafurahi kusikia zaidi.Nawasilisha.