Buzwagi kuna makubwa, inasikitisha

Mfwatiliaji

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
1,323
67
Wananchi sasa waibana Buzwagi



Na Patrick Mabula, Kahama

SAKATA la baadhi ya wanakijiji wenye mali wakiwamo wachimbaji wadogo katika mgodi wa Buzwagi ambao walishagoma kupokea fidia kutoka kampuni ya Barrick kwa madai kuwa wanapunjwa na kwenda mahakamani, wamegoma kuondoa shauri hilo baada ya kutakiwa kufanya hivyo na Serikali.

Wananchi hao wapatao 30 walisema juzi kuwa wamegoma kulitoa shauri hilo kortini, baada ya kuombwa kufanya hivyo ili waelewane nje ya Mahakama na mwekezaji huyo.

Wasimamizi wa madai hayo mahakamani, Bw.Omary Sekerume, Bw. Lameck Makoye na Bw. Issa bin Issa walisema katika kikao na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Brigedia Jenerali Yohana Balele aliwataka kulitoa shauri hilo mahakamani.

Walisema baada ya kuombwa na Mkuu wa Mkoa katika kikao hicho, kuondoa shauri la madai ya fidia walilopeleka mahakamani, baada ya kutoridhishwa na fidia inayotolewa na Barrick kupitia kampuni ya Pangea Minerals, walikataa.

Aliyevumbua dhahabu katika eneo la Buzwagi, Bw.Yahya Bundala, ambaye ni mmoja wa waliokataa kupokea fidia hiyo, alisema waliamua kwenda mahakamani baada ya kutoridhishwa na fidia katika mali zao yakiwamo mashimo ya dhahabu waliyokuwa wanachimba, mashamba, miti, nyumba na makaburi ya ndugu zao.

Bw. Sekelume alisema hawakubali fidia ya sh. 200,000 kwa kila shimo walilokuwa wakichimba dhahabu na sh. 120 kwa meta moja ya mraba ya kila ardhi ya mashamba yao zikiwamo mali mbalimbali.

Alisema wao wanataka Pangea iwalipe fidia ya kila shimo kiasi cha sh. milioni 25 sehemu za maosheo walipokuwa wakikamulia dhahabu, sh. milioni 40 na kila meta moja eneo ya mashamba yao iwe kiasi cha sh. 4,941.

Katika barua iliyotoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama aliyowaandikia yenye kumbukumbu namba cb 75/143/01/3 ya Julai 13 mwaka huu, aliwataka wananchi hao kusaini barua za makubaliano ya fidia ya mali zao na kupisha eneo la Buzwagi kitu ambacho walikipinga.

Aidha, kwenye eneo la mgodi wa Buzwagi zaidi ya watu 538 wanatakiwa kulipwa fidia katika mradi huo, ambapo kati yao tayari wameshalipwa kiasi cha sh. milioni 72.8 ingawa bado kundi la wakijiji na wachimbaji wadogo wapatao 30 bado wamegoma na kuamua kwenda mahakamani.

Awali, Meneja Mtendaji Mkuu wa Barrick Gold Tanzania, Bw. Deo Mwanyika katika taarifa yake aliyoitoa hivi karibuni kwa Rais Jakaya Kikwete alipotembelea Buzwagi, alisema mgogoro na watu hao upo kwa waliokataa kupokea fidia.
 
Kumbe compansation ya ardhi ni TZS 120 per sq. meter na shimo la dhahabu hata kwa waliogundua ni laki mbili tu
 
Muziki bado mnene na kamam hawatalipa basi Mahakamani ni mahala pao ila swali ni je watashinda na kupata haki huko ? Maana Serikali ya JK na wawekezaji hata wakimuua mama yako bado hawataguswa .I predict this to be another Zimbambwe ama Soweto
 
Wananchi sasa waibana Buzwagi
Na Patrick Mabula, Kahama

SAKATA la baadhi ya wanakijiji wenye mali wakiwamo wachimbaji wadogo katika mgodi wa Buzwagi ambao walishagoma kupokea fidia kutoka kampuni ya Barrick kwa madai kuwa wanapunjwa na kwenda mahakamani, wamegoma kuondoa shauri hilo baada ya kutakiwa kufanya hivyo na Serikali.

Wananchi hao wapatao 30 walisema juzi kuwa wamegoma kulitoa shauri hilo kortini, baada ya kuombwa kufanya hivyo ili waelewane nje ya Mahakama na mwekezaji huyo.

Wasimamizi wa madai hayo mahakamani, Bw.Omary Sekerume, Bw. Lameck Makoye na Bw. Issa bin Issa walisema katika kikao na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Brigedia Jenerali Yohana Balele
aliwataka kulitoa shauri hilo mahakamani.

Walisema baada ya kuombwa na Mkuu wa Mkoa katika kikao hicho, kuondoa shauri la madai ya fidia walilopeleka mahakamani, baada ya kutoridhishwa na fidia inayotolewa na Barrick kupitia kampuni ya Pangea Minerals, walikataa. Aliyevumbua dhahabu katika eneo la Buzwagi, Bw.Yahya Bundala, ambaye ni mmoja wa waliokataa kupokea fidia hiyo, alisema waliamua kwenda mahakamani baada ya kutoridhishwa na fidia katika mali zao yakiwamo mashimo ya dhahabu waliyokuwa wanachimba, mashamba, miti, nyumba na makaburi ya ndugu zao.

Bw. Sekelume alisema hawakubali fidia ya sh. 200,000 kwa kila shimo walilokuwa wakichimba dhahabu na sh. 120 kwa meta moja ya mraba ya kila ardhi ya mashamba yao zikiwamo mali mbalimbali.

Alisema wao wanataka Pangea iwalipe fidia ya kila shimo kiasi cha sh. milioni 25 sehemu za maosheo walipokuwa wakikamulia dhahabu, sh. milioni 40 na kila meta moja eneo ya mashamba yao iwe kiasi cha sh. 4,941.

Katika barua iliyotoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama aliyowaandikia yenye kumbukumbu namba cb 75/143/01/3 ya Julai 13 mwaka huu, aliwataka wananchi hao kusaini barua za makubaliano ya fidia ya mali zao na kupisha eneo la Buzwagi kitu ambacho walikipinga.

Aidha, kwenye eneo la mgodi wa Buzwagi zaidi ya watu 538 wanatakiwa kulipwa fidia katika mradi huo, ambapo kati yao tayari wameshalipwa kiasi cha sh. milioni 72.8 ingawa bado kundi la wakijiji na wachimbaji wadogo wapatao 30 bado wamegoma na kuamua kwenda mahakamani.

Awali, Meneja Mtendaji Mkuu wa Barrick Gold Tanzania, Bw. Deo Mwanyika katika taarifa yake aliyoitoa hivi karibuni kwa Rais Jakaya Kikwete alipotembelea Buzwagi, alisema mgogoro na watu hao upo kwa waliokataa kupokea fidia.

Shimo la dhahabu laki mbili wakati bei ya ounce moja $700 ambayo ni kama zaidi ya mara tatu ya fidia. Uwi uwi uwi hii serikali inanuka. Hesabu za wapi hizi jamani waliosoma uchumi na JK pengine wanafahamu syllabus ya uchumi wakati huo. Hii serikali iko upande wa mafedhuli na mafisadi.
 
Ni kutega mabomu tu, hadi wakimbie wenyewe. kwani wenyewe si tutayachimba pole pole haraka ya nini.
 
Wananchi sasa waibana Buzwagi

....

Sekelume alisema hawakubali fidia ya sh. 200,000 kwa kila shimo walilokuwa wakichimba dhahabu na sh. 120 kwa meta moja ya mraba ya kila ardhi ya mashamba yao zikiwamo mali mbalimbali.

Fidia ya shilingi laki mbili kwa shimo? dola 180? na sh 120 kwa meta ya mraba?

Huu ni utani au ni kweli?
 
Kwa mtaji huu kuna mtu yeyote atakayesonga mbele jamani. Baada ya hawa ndugu kupata hivyo vilaki kadhaa what next, wamenyanganywa kipato chao cha kila siku maana huu ni unyanganyi, waende wapi si ndio umaskini unazidi kupiga hatua. Halafu mtu anaweza kusema hadharani kwamba haelewi kwa nini tanzania bado ni maskini.

Kuna haja yakufikiri wakati majibu yako waziwazi kabisa kila kona yanasikika. God bless thia country and all its people.
 
Hivi kweli tunayo serikali kwa ajili ya watu au kwa ajili ya wazungu na viongozi wachache?.Hivi hiyo dhahabu itakayochimbwa nayo itauzwa kwa Tsh 200,000? Ninani aliyepanga hayo malipo? Kama kuna mtu anafahamu huyo mtu tafadhali muwekeni hadharani mara moja.
Kwa kifupi huu ni wizi na uonezi mkubwa! na wakati umefika kwa wananchi kuchukua silaha na kupigania haki zao.Maana serikali haiwajali hivyo wekeni mabomu kama alivyosema ndugu yangu hapo juu au tumieni silaha yoyote ile mpaka kieleweke.
Hawa wazungu na wanyampara wao wanadhani Tz ni nchi ya kunyonya halafu wanatucheka ati kuwa sisi ni masikini.
Wembe.
 
mikataba ni siri,sasa sijui ndio vipi tena.wananchi hawajui mkataba unasema nini kwa hiyo hawajui kama kulikuwa na malipo au hapana.hivi kwa nini tunyanyasike kwenye aridhi yetu
 
laki 2 kwa shimo?cant believe.....,kuna ulazima wa kuwapima viongozi magonjwa ya akili kabla ya kuingia madarakani,halafu JK anadai hajui kwa nini nchi ni maskini,coz yeye mwenyewe akili yake ni maskini,fool.
 
Badala ya serikali kuwasaidia wananchi wasidhulumiwe yenyewe ilikuwa upande wa mwekezaji, hongera Lissu kwa kujitolea kuwatetea bure.
 
Enzi hizo thread wala hazichangiwi sana.

Hii serikali hii. CCM ndio chanzo kikuu cha matatizo nchi hii.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom