Vigogo Wamshutumu Rais kwa Kukosa Kuchukua Hatua Dhidi ya Rushwa, Ubadhirifu na Ufisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Serikali kitanzini

na Mwandishi Wetu
Tanzania daima

VIGOGO kadhaa waliyatumia maadhimisho ya miaka minane tangu kufariki kwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, kuinyooshea kidole serikali, wakiituhumu kwa kufanya mchezo na vita dhidi ya rushwa, ubadhirifu na ufisadi.

Aliyeonekana kutoa maneno makali kuliko wote, ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, ambaye akizungumza wakati wa kufunga kongamano la kumkumbuka Nyerere huko Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alibainisha kuwa rushwa inazungumzwa sana hivi sasa lakini hakuna mtu anayethubutu kuchukua hatua.

Alisema yanayotokea sasa ni tofauti ya yaliyotokea miaka kadhaa iliyopita, akikumbusha kuwa katika miaka ya 1990, wakati serikali ilipokabiliwa na tuhuma nzito kuhusu rushwa, rais wa wakati huo, Ali Hassan mwinyi, aliamua kulivunja Baraza la Mawaziri.

Alisema kuwa alipoliunda upya, rais Mwinyi alibakisha mawaziri wa zamani saba tu, jambo ambalo lilimwezesha; kuanza upya' kuisuka serikali yake ifanye kile kilichokuwa kikipendekezwa na watu wengi.

Alisema hali hiyo ilibadilika baada ya Mwinyi kuondoka madarakani, kwani rais aliyemfuatia, Benjamin Mkapa, licha ya kuunda Tume ya Warioba, kuchunguza masuala ya rushwa, matokeo ya tume hiyo yamesababisha zaidi ugomvi badala ya kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa.

Ingawa hakufafanua kuhusu kauli yake hiyo, lakini uzoefu unaonyesha kuwa hakuna hatua madhubuti zilizochukuliwa kutokana na mapendekezo yaliyokuwamo katika ripoti ya tume hiyo.

Akizidi kumchambua Mkapa, Butiku alisema kuwa hivi sasa rais huyo, ambaye katika harakati za kuwania nafasi hiyo alijulikana kama; Bwana Msafi' (Mr Clean), anakabiliwa na tuhuma nzito za kufanya biashara akiwa Ikulu, lakini inashangaza kuona kuwa ameamua kukaa kimya.

Hii ni mara ya kwanza kwa kiongozi wa aina ya Butiku, kujitokeza hadharani na kutaka rais huyo mstaafu ajitokeze kujibu tuhuma hizo. Butiku alitoa kauli hiyo, akiijenga chini ya msingi kuwa kimya kinachoonyeshwa na Mkapa, kinaweza kutumiwa na viongozi wengine kujenga utamaduni wa umangimeza.

Akionekana kuiweka serikali ya sasa kitanzini, Butiku alibainisha kuwa rushwa inazungumzwa sana hivi sasa lakini inashangaza kuona kuwa hakuna mtu au taasisi inayochukua hatua za dhati kukabiliana na hali hiyo.

Alisema kuwa kuna viongozi ambao wanatajwa kwa tuhuma za ufisadi na inashangaza kuwa badala ya tuhuma hizo kufanyiwa kazi, serikali inakuja na kauli zinazojikanganya kwa kugonganisha maneno.

"Baba wa Taifa aliwahi kusema kuwa nchi inanuka rushwa, alikuwa CHADEMA? Hivi sasa tunashuhudia tuhuma nzito dhidi ya viongozi; serikali ichukue hatua na kutoa majibu sahihi. Masuala ya rushwa si ya vyama," alisema Butiku.

Butiku alikwenda mbali zaidi na kuzidi kuibana Serikali ya Awamu ya Nne kwa kubainisha kuwa uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 2005 ulitawaliwa na rushwa.

"(Makamu Mkuu wa UDSM) Profesa Mukandala ulikuwepo. Hukuona rushwa? Katika dakika za mwisho Mwalimu alisema rushwa ni donda ndugu, mimi nasema ni unfinished business (jambo ambalo halijamalizwa)," alisema.

Akikumbusha hatua zilizochukuliwa na rais Mwinyi, Butiku aliihimiza serikali kuchukua hatua akisisitiza kuwa katika masuala ya rushwa ambayo imefikia viwango vilivyopo nchini, mtu ahitaji ushahidi ili kuchukua hatua zinazopaswa.

Alisema kuwa amemwandikia barua Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na masuala hayo, ingawa hakueleza hadharani ni nini hasa kilichomo ndani ya barua hiyo.

Butiku ametoa kauli hiyo huku serikali ikionekana kana kwamba inafanya mchezo wa kuigiza kuhusiana na tuhuma zilizotolewa dhidi ya viongozi wake, wakituhumiwa kwa ufisadi.

Tuhuma hizo zilizotolewa na wapinzani, zimesababisha viongozi kadhaa wa serikali na CCM, kujitokeza hadharani kwa kile wanachodai kuwa ni kuzijibu, huku wakitoa kauli ambazo si tu zinatofautiana, bali zinakinzana katika masuala kadhaa.

Kiongozi mmoja aliwahi kunukuliwa akisema kuwa serikali haitajihangaisha kuzunguka mikoani kujibu tuhuma hizo kama walivyofanya wapinzani kuzunguka mikoani kuwaelezea wananchi kuhusiana na madai ya ubadhirifu.

Lakini siku moja baadaye, kiongozi mwingine aliibuka na kudai kuwa viongozi wa CCM watajipanga na kuanza ziara katika mikoa yote ili kujibu tuhuma hizo za wapinzani.

Mpango huo wa CCM ulidakwa na serikali, ambayo iliwatuma mawaziri wake katika makundi mikoani, wakiungana na makada kadhaa wa CCM wakijibu tuhuma dhidi ya viongozi wa serikali na chama.

Aliporejea kutoka ziara yake ya wiki tatu nchini Marekani, Rais Kikwete, akihutubia katika mkusanyiko wa kidini huko Arusha, alisema kuwa serikali inachunguza kila tuhuma inayotolewa, na kuleta mkanganyiko zaidi, hasa ukizingatia kauli za awali za viongozi wengine zilizolenga kuonyesha kuwa madai hayo ya wapinzani ni upuuzi.
 
Akizidi kumchambua Mkapa, Butiku alisema kuwa hivi sasa rais huyo, ambaye katika harakati za kuwania nafasi hiyo alijulikana kama ‘Bwana Msafi’ (Mr Clean), anakabiliwa na tuhuma nzito za kufanya biashara akiwa Ikulu, lakini inashangaza kuona kuwa ameamua kukaa kimya.

Haya sasa, sisiemu wambishie na Butiku, maana wao kazi yao ni kubisha hata ukweli!
 
hapo tunasema kuwa kidonda kimepata doctor wake maana walizoea tuu akina Zitto na sijui nani vile kuwa ndo wanasema tuu na huyu nae sijui hapo watasemaje
 
Raisi kaziba masikio. Ni jana tu alikandia tuhuma hizo anazoziita za wapinzani kuwa zinaweza kusababisha vurugu kwa hiyo anaammini wanatafuta madaraka kupitia mafuta ambayo ni damu za watu! Hotuba ya Jana mliipata? Mi simuelewi huyu presida wetu!
 
Haya Babu mh Kikongwe la kule mbali mwiluuu!!!!!!! zee la propaganda, ki-gagula la sisi-mmh!!!!! Tafadhali tumia uwezo wako, mvute kwenye karai na u-mwadabishe huyo Batik anaejidai kuwa-sitiri wadanganyika pleeeeeeeeeeese!!!!!!!

PIPA LAKUVUJA HALIZIBIKI KWA BIG GEE
 
bado anakusanya data na baada ya muda utaambiwa kuwa bank kuu taarifa ni safi hakuna rushwa na taarifa zoet za mahesabu ziko ok hivyo bwana baaa haliji yuko safi kuendelea kuwa gavana wa BOt kazi ipo
 
Watasema hawa, Butiku, mwinyi wote wamesema. itafika wananchi wataamua wenyewe, kwani hawaoni. wanasubiri mkuu achukue hatua, ole wake ashindwe kuchukua atalijua jiji.
 
Jamani Wana Forum Wenzangu, Mie Nikisoma Habari Kama Hizi Huwa Presha Na Hasira Zinapanda. Hivi Jamani Huyu Rais Wetu Anaumwa Ugonjwa Gani? Hivi Jamani Ndio Ku-ignore Sauti Ya Jamii Wa Watanzania Kiasi Hiki? Si Ajibaraguze Basi Angalau Afanye Re-shufle Hiyo Cabinet Yake Basi, Tuone Kwamba Anafanya Kazi Kama Kiongozi Basi. Kazi Kusafiri Tu Kwenda Marekani Utafikiri Teenager!

Yaani Baba Wa Taifa Angekuwa Bado Yu Hai Nadhani Angewachapa Viboko Yeye Na Huyo Lowassa Ikulu!

Please Excuse My Language, But This Guy Is Full Of S_ _ _!!
 
Mimi nilidhani huko serikalini wote hawana akili!
Huyu mzee Butiku ameamua kumwaga mamnyanga chini na kung'oa mzizi wa Fitna.

Haya nyie makada wa SISIEMU jibuni swali.

Nyerere alikuwa Chadema aliposema nchi inanuka Rushwa?
 
Madilu, CCM watasema kuwa Butiku analalamikia kunyimwa ulaji, na yeye angekuwa kwenye mkao wa kula sijui kama angepiga kelele hivyo. Kuna baadhi ya watu wanadai kuwa yeye na Mkapa hawakuiva na Mkapa alimwonyesha mlango wa kutokea mapema Zaidi. Nasema CCM watasema hivyo kwa sababu wao huwa hawajibu hoja, wanawashambulia watoa hoja!
 
At last mwanaume toka CCM kasimama!

Nadhani watasimama wengi? tuwape muda,,, this is like a wave, you either go with it au unaachwa kabisa,,, CCM ni lazima waende na wimbi hili otherwise... mambo hayatakuwa upande wao...

Tatizo langu, hawa tunaowategemea sidhani kuna kitu wanafanya kujiandaa kuongoza taifa, naona nao wanapiga vigelegele tu, siku wakiambiwa haya uongozi huu watakuwa wang'aa macho...mambo yatakuwa mambo!!!
 
Wasi wasi wangu ni juu ya Mahusiani ya warioba na Butiku .Warioba kaamuwa kuwasaliti Wadanganyika na Butiku kashika msimamo na kusema ukweli . Butiku kaamua kumuezi Mwalimu vilivyo na Warioba kaomba usajili kwa mafisadi maana hata hivyo anahusika kwa njia moja ama nyingine so Butiku na Mwinyi karibuni . Mzee Mwinyi alikandiwa sana siku zile na sasa naye anasema ukweli sijui watamnyima mlinzi na magari ya misafara ?

Kazi iko hapo kwa CCM
 
Rais wetu mtalii,so hayamuingilii akilini?mnasubiri nini kumpuuza?

hatupendi kabisa?anapenda kusafiri na kula good time
 
Serikali kitanzini

na Mwandishi Wetu

VIGOGO kadhaa waliyatumia maadhimisho ya miaka minane tangu kufariki kwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, kuinyooshea kidole serikali, wakiituhumu kwa kufanya mchezo na vita dhidi ya rushwa, ubadhirifu na ufisadi.

Aliyeonekana kutoa maneno makali kuliko wote, ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, ambaye akizungumza wakati wa kufunga kongamano la kumkumbuka Nyerere huko Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alibainisha kuwa rushwa inazungumzwa sana hivi sasa lakini hakuna mtu anayethubutu kuchukua hatua.

Alisema yanayotokea sasa ni tofauti ya yaliyotokea miaka kadhaa iliyopita, akikumbusha kuwa katika miaka ya 1990, wakati serikali ilipokabiliwa na tuhuma nzito kuhusu rushwa, rais wa wakati huo, Ali Hassan mwinyi, aliamua kulivunja Baraza la Mawaziri.

Alisema kuwa alipoliunda upya, rais Mwinyi alibakisha mawaziri wa zamani saba tu, jambo ambalo lilimwezesha ‘kuanza upya’ kuisuka serikali yake ifanye kile kilichokuwa kikipendekezwa na watu wengi.

Alisema hali hiyo ilibadilika baada ya Mwinyi kuondoka madarakani, kwani rais aliyemfuatia, Benjamin Mkapa, licha ya kuunda Tume ya Warioba, kuchunguza masuala ya rushwa, matokeo ya tume hiyo yamesababisha zaidi ugomvi badala ya kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa.

Ingawa hakufafanua kuhusu kauli yake hiyo, lakini uzoefu unaonyesha kuwa hakuna hatua madhubuti zilizochukuliwa kutokana na mapendekezo yaliyokuwamo katika ripoti ya tume hiyo.

Akizidi kumchambua Mkapa, Butiku alisema kuwa hivi sasa rais huyo, ambaye katika harakati za kuwania nafasi hiyo alijulikana kama ‘Bwana Msafi’ (Mr Clean), anakabiliwa na tuhuma nzito za kufanya biashara akiwa Ikulu, lakini inashangaza kuona kuwa ameamua kukaa kimya.

Hii ni mara ya kwanza kwa kiongozi wa aina ya Butiku, kujitokeza hadharani na kutaka rais huyo mstaafu ajitokeze kujibu tuhuma hizo. Butiku alitoa kauli hiyo, akiijenga chini ya msingi kuwa kimya kinachoonyeshwa na Mkapa, kinaweza kutumiwa na viongozi wengine kujenga utamaduni wa umangimeza.

Akionekana kuiweka serikali ya sasa kitanzini, Butiku alibainisha kuwa rushwa inazungumzwa sana hivi sasa lakini inashangaza kuona kuwa hakuna mtu au taasisi inayochukua hatua za dhati kukabiliana na hali hiyo.

Alisema kuwa kuna viongozi ambao wanatajwa kwa tuhuma za ufisadi na inashangaza kuwa badala ya tuhuma hizo kufanyiwa kazi, serikali inakuja na kauli zinazojikanganya kwa kugonganisha maneno.

“Baba wa Taifa aliwahi kusema kuwa nchi inanuka rushwa, alikuwa CHADEMA? Hivi sasa tunashuhudia tuhuma nzito dhidi ya viongozi… serikali ichukue hatua na kutoa majibu sahihi. Masuala ya rushwa si ya vyama,” alisema Butiku.

Butiku alikwenda mbali zaidi na kuzidi kuibana Serikali ya Awamu ya Nne kwa kubainisha kuwa uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 2005 ulitawaliwa na rushwa.

“(Makamu Mkuu wa UDSM) Profesa Mukandala ulikuwepo. Hukuona rushwa? Katika dakika za mwisho Mwalimu alisema rushwa ni donda ndugu, mimi nasema ni unfinished business (jambo ambalo halijamalizwa),” alisema.

Akikumbusha hatua zilizochukuliwa na rais Mwinyi, Butiku aliihimiza serikali kuchukua hatua akisisitiza kuwa katika masuala ya rushwa ambayo imefikia viwango vilivyopo nchini, mtu ahitaji ushahidi ili kuchukua hatua zinazopaswa.

Alisema kuwa amemwandikia barua Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na masuala hayo, ingawa hakueleza hadharani ni nini hasa kilichomo ndani ya barua hiyo.

Butiku ametoa kauli hiyo huku serikali ikionekana kana kwamba inafanya mchezo wa kuigiza kuhusiana na tuhuma zilizotolewa dhidi ya viongozi wake, wakituhumiwa kwa ufisadi.

Tuhuma hizo zilizotolewa na wapinzani, zimesababisha viongozi kadhaa wa serikali na CCM, kujitokeza hadharani kwa kile wanachodai kuwa ni kuzijibu, huku wakitoa kauli ambazo si tu zinatofautiana, bali zinakinzana katika masuala kadhaa.

Kiongozi mmoja aliwahi kunukuliwa akisema kuwa serikali haitajihangaisha kuzunguka mikoani kujibu tuhuma hizo kama walivyofanya wapinzani kuzunguka mikoani kuwaelezea wananchi kuhusiana na madai ya ubadhirifu.

Lakini siku moja baadaye, kiongozi mwingine aliibuka na kudai kuwa viongozi wa CCM watajipanga na kuanza ziara katika mikoa yote ili kujibu tuhuma hizo za wapinzani.

Mpango huo wa CCM ulidakwa na serikali, ambayo iliwatuma mawaziri wake katika makundi mikoani, wakiungana na makada kadhaa wa CCM wakijibu tuhuma dhidi ya viongozi wa serikali na chama.

Aliporejea kutoka ziara yake ya wiki tatu nchini Marekani, Rais Kikwete, akihutubia katika mkusanyiko wa kidini huko Arusha, alisema kuwa serikali inachunguza kila tuhuma inayotolewa, na kuleta mkanganyiko zaidi, hasa ukizingatia kauli za awali za viongozi wengine zilizolenga kuonyesha kuwa madai hayo ya wapinzani ni upuuzi.

Source:Tanzania Daima.

Mnaona mambo yanavyokua matamu sasa,moto uendelee kuwaka tu,hadi kieleweke.Soma signature yangu ipo simple lakini imebeba ujumbe,hata hilo Butiko kaliona.
 
Serikali kitanzini

na Mwandishi Wetu



Source:Tanzania Daima.

Mnaona mambo yanavyokua matamu sasa,moto uendelee kuwaka tu,hadi kieleweke.Soma signature yangu ipo simple lakini imebeba ujumbe,hata hilo Butiko kaliona.

ndiyo inabeba ujumbe hata mimi ninalikubali mzee
 
Bila shaka hawa wanaozungumzia huu ufisadi hawana uchungu wa kushindwa uchaguzi wa 2005, kama CHADEMA na vyama vingine wanavyotuhumiwa wakizungumzia ufisadi.
 
Back
Top Bottom