Butiama wananyang'anywa sufuria, jembe kisa michango ya elimu. Shinyanga wanagawiwa ID za ujasiriamali kwa mtutu na askari. Tutafika?

Wabunifu sera wa serikali ya magu na ccm wamefika mwisho wao wa kufikiri. Hawana jipya la kufanya zaidi ya kuzidisha mateso kwa wale wanaowaita wanyonge. Hadi siku mnyonge atakapotambua kuwa ananyongwa ndipo tutapata ukombozi wa kweli.
Kwa kawaida kodi za wananchi na ada mbalimbali ndizo michango yao ya "lazima" kwa serilali iliyoko kisheria. Hivi ndivyo vyanzo vikuu vya mapato ya serikali ambayo yanayowezesha uendeshaji wake: kugharamia matumizi ya kawaida (recurrent expenditure) na kuwaletea maendeleo (development expenditure).
Mamlaka zenye dhamana ya kukusanya mapato ya serikali katika kutekeleza majukumu yao zinapaswa kuzingatia hali halisi za uchumi wa wananchi.
Ipo wizara ya mipango na fedha, na taasisi ya takwimu (Tanzania Bureau of Statistics). Wizara na Takwimu kama wanafanya kazi zao barabara ikiwemo maoteo (projections), habari ya " watoto wengi zaidi ya ilivyotarajiwa wameandikishwa mashuleni kwa sababu ya elimu ya bure" haipaswi kuwepo.
Aidha, utekelezaji wa kibajeti uni hauzingatiwi! Serikali haina vipaumbele katika miradi ya maendeleo kwa maana ya kuwa mirandi ya maendeleo inayotekelezwa kwa wakati mmoja imekuwa mingi mno na inazidia mapato yetu ikitiliwa maanani kuwa wafadhili/washirika wetu wa maendeleo wamepunguza ufadhili wao kwa sababu mbalimbali. Ndiyo sababu za kubuniwa na kunaibuliwa vitambulisho vya wajasiriamali na michango ya ujenzi wa shule za sekondari.
Fikiria viuzwe jumla ya vitambulisho mil. 5, tu @ 20,000/-. Tsh mil. 100 zinaweza kupatikana. Na wastani wa Tsh elfu 30 @ kaya, kwa kaya milioni 20, wananchi watakamuliwa bila huruma bil 600 nje ya bajeti ya serikali. Si haba. Mtanzania wa kaeaida anapatwa wasiwasi na uendeshwaji na hali ya uchumi wa nchi. Kampuni na mtu binafsi hufilisika kwa kukosa ukwasi na kushindwa kugharamia na kulipa madeni.
 
Kwa kawaida kodi za wananchi na ada mbalimbali ndizo michango yao ya "lazima" kwa serilali iliyoko kisheria. Hivi ndivyo vyanzo vikuu vya mapato ya serikali ambayo yanayowezesha uendeshaji wake: kugharamia matumizi ya kawaida (recurrent expenditure) na kuwaletea maendeleo (development expenditure).
Mamlaka zenye dhamana ya kukusanya mapato ya serikali katika kutekeleza majukumu yao zinapaswa kuzingatia hali halisi za uchumi wa wananchi.
Ipo wizara ya mipango na fedha, na taasisi ya takwimu (Tanzania Bureau of Statistics). Wizara na Takwimu kama wanafanya kazi zao barabara ikiwemo maoteo (projections), habari ya " watoto wengi zaidi ya ilivyotarajiwa wameandikishwa mashuleni kwa sababu ya elimu ya bure" haipaswi kuwepo.
Aidha, utekelezaji wa kibajeti uni hauzingatiwi! Serikali haina vipaumbele katika miradi ya maendeleo kwa maana ya kuwa mirandi ya maendeleo inayotekelezwa kwa wakati mmoja imekuwa mingi mno na inazidia mapato yetu ikitiliwa maanani kuwa wafadhili/washirika wetu wa maendeleo wamepunguza ufadhili wao kwa sababu mbalimbali. Ndiyo sababu za kubuniwa na kunaibuliwa vitambulisho vya wajasiriamali na michango ya ujenzi wa shule za sekondari.
Fikiria viuzwe jumla ya vitambulisho mil. 5, tu @ 20,000/-. Tsh mil. 100 zinaweza kupatikana. Na wastani wa Tsh elfu 30 @ kaya, kwa kaya milioni 20, wananchi watakamuliwa bila huruma bil 600 nje ya bajeti ya serikali. Si haba. Mtanzania wa kaeaida anapatwa wasiwasi na uendeshwaji na hali ya uchumi wa nchi. Kampuni na mtu binafsi hufilisika kwa kukosa ukwasi na kushindwa kugharamia na kulipa madeni.
Umesema kweli. Lakini kwa nn serikali hii haina projections ya mahitaji ya kijamii?!
"Tunanunua ndege na hela tunazo", unamficha nani
 
Habari mwana JF..

Je tumekosa dira au tumeamua kwa makusudi kuwaumiza watu wetu?!

Hivyo ndivyo navyoweza kuuliza kwa hali tuliyofikia sasa.

Sasa hivi tunavyozungumza huko Butiama ktk baadhi ya vijiji kama Buturu, michango ya ujenzi wa sekondari inalazimishwa hata kwa asiye na uwezo. Buturu wanachangishwa sh. 40,000/= (awamu ya 1). Juzi wenyekiti wa vijiji wameanza oparesheni kukamata kuku, jembe, sufuria n.k kwa yeyote ambaye mpaka sasa hajachanga.

Ikumbukwe sasa hivi kaya nyingi ndio zipo ktk kilimo, ni msimu wa kupanda ila kwa umaskini wa kaya zile hata mbegu ya kilimo ni shida. Mbolea ndio hawanunui kabisaa..! Ni maskini wa kutupwa. Hizo 40,000/= watatoa wapi?!

Hiyo mnayosema ni serikali sikivu, ni ipi?! Hii inayo engineer unyonyaji mkubwa hivi?!

Sasa huku Shinyanga ndio nimeshangaa.
Waponda mawe ya mgodini, kina mama wauza mchicha n.k wamelazimishwa kuuziwa vitambulisho vya ujasiriamali.

Ktk taarifa ya habari ya ITV usiku wa saa 2, tarehe 15 march 2019, ameonekana mkuu wa wilaya ya shinyanga akitimka mbio na askari wake kuwakimbia waganga njaa wa mgodini ambao waliandamana kwenda kulalamika kulazimishwa chini ya ulinzi mkali na bunduki kununua vitambulisho hivyo.

Wamehoji kuwa wao sio wajasiriamali! Mama mmoja akahoji yeye anauza mchicha na mtaji wake ni sh. Elfu 3. Anatoa wapi 20,000/-???!

Ni wapi tunafeli. Inakuwaje project za JPM zinageuka mateso kwa mwananchi?

Au ukitembelea VX unisahau uhalisia wa maisha ya wananchi wako?!

Cc: barafu , technically , magongwa mtambuka, UCD . Wakudadavuwa
Mliipenda wenyewe na nderemo mkapiga sasa mnaisoma namba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM hoyeeeeeeeeeee. Tuliwataka wenyewe, tulipiga kura wenyewe sasaaa. Mtuache tunasubiri khanga, kofia na t shirt 2020. Mtajiju.
 
Watu mnawazungumzia wapewa vitambulisho tu vya ujasiliamali lakini hamchunguzi gharama za miamala ya kifedha kupanda na pengine makato yasiyoeleweka kwenye mishahara,mambo ni mengi mda ni mchache kila mtu atafikiwa kwa namna yake hadi kibubu kijae
 
.
Kuhusu hizo kadi zilizotolewa na Mhe. Rais Magufuli nadhani kuna maagiza ambayo yanapaswa kuongezeka kutoka kwake.

Nilimsikia akisema kuwa vitambulisho hivyo ni kwa watu wenye mtaji usiozidi milioni nne.

Sijasikia akitoa maelekezo kuhusu kima cha chini cha mtaji.

Tangu yule mbunge Sugu alipopata msukosuko, Maafisa wetu kutoka secret service walipaswa kuwa wameona tatizo lililoibuliwa na kushauri ipasavyo.

Wamefanya hivyo?

Kama tayari, Mhe. Rais anapaswa kuchukua hatua sasa.

Kama bado hawajafanya hivyo, waharakishe kuweka sawa jambo hili.

Usalama wa nchi ni pamoja na usalama wa kiuchumi katika kaya hizi za watu maskini.

Nimesikia huko Kaskazini wanasema hii ni sawa na kodi ya kichwa.

Kuna jambo halijakaa sawa.

Usipate shida kuhusu vitambulisho na mwendelezo wake bali ukitaka kujua undani na siri isiyowekwa wazi ya vitambulisho hivyo basi inabidi uwe kipenzi cha kumwangalia Agrey Mwanri kwenye youtube...huyu kwenye mikutano yake huweka wazi na hadharani kwa kila kitu ambacho wengine hawathubutu kukisema
 
Usipate shida kuhusu vitambulisho na mwendelezo wake bali ukitaka kujua undani na siri isiyowekwa wazi ya vitambulisho hivyo basi inabidi uwe kipenzi cha kumwangalia Agrey Mwanri kwenye youtube...huyu kwenye mikutano yake huweka wazi na hadharani kwa kila kitu ambacho wengine hawathubutu kukisema
Mh Aggrey Mwanri anasemaje mkuu
 
Wabunifu sera wa serikali ya magu na ccm wamefika mwisho wao wa kufikiri. Hawana jipya la kufanya zaidi ya kuzidisha mateso kwa wale wanaowaita wanyonge. Hadi siku mnyonge atakapotambua kuwa ananyongwa ndipo tutapata ukombozi wa kweli.
Naomba inaposadikika umechangia kuua uchumi unapunguziwa 75% ya mshahara wako anayezorotesha uchumi hana tofauti na mhujumu uchumi!
 
Habari mwana JF..

Je tumekosa dira au tumeamua kwa makusudi kuwaumiza watu wetu?!

Hivyo ndivyo navyoweza kuuliza kwa hali tuliyofikia sasa.

Sasa hivi tunavyozungumza huko Butiama ktk baadhi ya vijiji kama Buturu, michango ya ujenzi wa sekondari inalazimishwa hata kwa asiye na uwezo. Buturu wanachangishwa sh. 40,000/= (awamu ya 1). Juzi wenyekiti wa vijiji wameanza oparesheni kukamata kuku, jembe, sufuria n.k kwa yeyote ambaye mpaka sasa hajachanga.

Ikumbukwe sasa hivi kaya nyingi ndio zipo ktk kilimo, ni msimu wa kupanda ila kwa umaskini wa kaya zile hata mbegu ya kilimo ni shida. Mbolea ndio hawanunui kabisaa..! Ni maskini wa kutupwa. Hizo 40,000/= watatoa wapi?!

Hiyo mnayosema ni serikali sikivu, ni ipi?! Hii inayo engineer unyonyaji mkubwa hivi?!

Sasa huku Shinyanga ndio nimeshangaa.
Waponda mawe ya mgodini, kina mama wauza mchicha n.k wamelazimishwa kuuziwa vitambulisho vya ujasiriamali.

Ktk taarifa ya habari ya ITV usiku wa saa 2, tarehe 15 march 2019, ameonekana mkuu wa wilaya ya shinyanga akitimka mbio na askari wake kuwakimbia waganga njaa wa mgodini ambao waliandamana kwenda kulalamika kulazimishwa chini ya ulinzi mkali na bunduki kununua vitambulisho hivyo.

Wamehoji kuwa wao sio wajasiriamali! Mama mmoja akahoji yeye anauza mchicha na mtaji wake ni sh. Elfu 3. Anatoa wapi 20,000/-???!

Ni wapi tunafeli. Inakuwaje project za JPM zinageuka mateso kwa mwananchi?

Au ukitembelea VX unisahau uhalisia wa maisha ya wananchi wako?!

Cc: barafu , technically , magongwa mtambuka, UCD . Wakudadavuwa

Safi kabisa,

Lazima watu wote walipe Kodi ili uchaguzi ukifika mtu asikubali Tena kurubuniwa kwa vitenge na mafulana ya wagombea was vyama.

Sasa watakuwa na akili,
 
Watu mnawazungumzia wapewa vitambulisho tu vya ujasiliamali lakini hamchunguzi gharama za miamala ya kifedha kupanda na pengine makato yasiyoeleweka kwenye mishahara,mambo ni mengi mda ni mchache kila mtu atafikiwa kwa namna yake hadi kibubu kijae
Si alisema hela anazo nyingi!!
 
Back
Top Bottom