Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
Edward Manyangu (41) mkazi wa kijiji cha Ijitu Wilaya ya Busega mkoani Simiyu anadaiwa kumuua mkewe, Dalali Maunga (41) kwa kumpiga na kitu kizito kichwani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Richard Abwao akizungumza leo Jumanne Mei 11, 2021 amesema tukio hilo lilitokea jana Mei 10, 2021 baada ya wanandoa hao kuingia kwenye mvutano kutokana na mwanaume kumtuhumu mkewe kuwa na uhusiano nje ya ndoa.
“Baada ya kutekeleza mauaji hayo, Manyangu naye alijiua kwa kujinyonga kwa kamba aliyofunga juu ya mti ulioko nje ya nyumba yao,” amesema Kamanda Abwao
Amebainisha kuwa kwa mujibu wa ujumbe wa maandishi unaoaminika kuandikwa na kuchwa na Manyangu, alikuwa akimthumu mkewe kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine.
Kamanda Abwao amesema baada ya uchunguzi wa kitabibu, miili ilikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Mwananchi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Richard Abwao akizungumza leo Jumanne Mei 11, 2021 amesema tukio hilo lilitokea jana Mei 10, 2021 baada ya wanandoa hao kuingia kwenye mvutano kutokana na mwanaume kumtuhumu mkewe kuwa na uhusiano nje ya ndoa.
“Baada ya kutekeleza mauaji hayo, Manyangu naye alijiua kwa kujinyonga kwa kamba aliyofunga juu ya mti ulioko nje ya nyumba yao,” amesema Kamanda Abwao
Amebainisha kuwa kwa mujibu wa ujumbe wa maandishi unaoaminika kuandikwa na kuchwa na Manyangu, alikuwa akimthumu mkewe kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine.
Kamanda Abwao amesema baada ya uchunguzi wa kitabibu, miili ilikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Mwananchi