Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,793
- 12,238
Bunge letu limeishapitisha muswada wa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya.
Ndugu wadau naomba tuangalie jambo hili kwa kifupi; kipi tulitakiwa kuanza nacho:
Narudisha hoja hii baada ya M.M. Mwanakijiji kuweka ufafanuzi mzuri kama ilivyoandikwa na Tanzania Daima leo tarehe 11/04/2012 kama ifuatavyo:
Ndugu wadau naomba tuangalie jambo hili kwa kifupi; kipi tulitakiwa kuanza nacho:
- Kujadili muundo wa muungano, au
- Kujadili katiba mpya?
Narudisha hoja hii baada ya M.M. Mwanakijiji kuweka ufafanuzi mzuri kama ilivyoandikwa na Tanzania Daima leo tarehe 11/04/2012 kama ifuatavyo:
Kitu cha tatu ambacho mzee Mtei amekigusia kwa kupitia ni kuwa Zanzibar inaonekana hawataki Muungano.Sasa, kama tayari kuna mwamko wa kupinga Muungano na tumeona hata juzi Jussa akipigia debe sheria ya ubaguzi dhidi ya watu wa bara (ambao anawaita wageni) lakini mchakato umepangwa kana kwamba watu wote wanaheshimu Muungano huu? Kwanini kwa mfano, kabla ya kuanza kuandika Katiba Mpya ya "Muungano" watu wa Zanzibar wapewe nafasi ya kuamua kama wanataka kubakia kwenye Muungano au la? Baadhi yetu tunaamini kuwa kabla ya kuandika Katiba Mpya ni vizuri suala la Muungano likaamuliwa peke yake kwanza.Kama Wazanzibar watasema wanataka kutoka kwenye Muungano basi watoke ili Bara waandike katiba yao mpya na hivyo kuwa na mahusiano ya nchi mbili ndugu. Kimsingi mzee Mtei amedodosa tu kwa mbali kuwa mchakato hauheshimu hisia za Wazanzibari wanaotaka Muungano uvunjwe kwa sababu "wanakandamizwa na kuonewa" na "mkoloni" Bara!
Naomba tujadili bila jazba kwa maslahi ya Tanzania/Tanganyika
Naomba tujadili bila jazba kwa maslahi ya Tanzania/Tanganyika