OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 48,772
- 102,128
Bomoa Bomoa iliyofanyika Kindondoni. Ilidaiwa kuwa ilifanywa kwa mujibu wa Tamko Na. 6.6.1 la Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995
Rais ameonekana kupongezwa kwa kutumia busara kuwarudishwa wamachinga walitimuliwa katikati ya mji wa Mwanza na kuwarudisha wachimbaji wadogowadogo mkoani Shinyanga. Rais alisikika akitoa amri hiyo kwamba hata kama ni sharia lazima wapiga kura wake walindwe wasibughudhiwe
Ikumbukwe kuwa wakati wa bomoa bomoa Dar es Salaam tulipiga kelele kuwa huu ni unyama tukimuomba rais aamuru utu uzingatiwe. Ikatamkwa kuwa hiyo ni kwa mujibu wa Tamko Na. 6.6.1 la Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995.
Je, busara hizi zina msimu na maeneo spesheli? Je wamachinga waliondolewa Dar na Mbeya wao sio masikini? Wao rais wao ni yupi?