Burundi yakataliwa kujiunga SADC

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275

Burundi imekwama kujiunga na Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kuelezwa kuwa imeshindwa kutimiza vigezo vya kuwa mwanachama.

Kupitia taarifa ya Mwenyekiti wa SADC, Rais wa Namibia, Hage Geingob (pichani) iliyotolewa hivi karibuni, Burundi haijakidhi vigezo.

Taarifa hiyo imesema wataalamu wa masuala ya diplomasia waliopewa jukumu la kuyafanyia tathimini maombi ya Burundi wamejiridhisha kuwa bado taifa hilo la Afrika Mashariki halijapata baraka za kujiunga SADC.

Imesema hali ya uhusiano na nchi jirani ikiwemo Rwanda ni miongoni mwa dosari za kutokamilika kwa vigezo vya kujiunga SADC. Tathmini ya mwisho ya Burundi ilifanyika kati ya Mei 18 na 25, mwaka huu.

Kama ingekubaliwa, Burundi ingekuwa mwanachama wa pili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kujiunga SADC. Tanzania ndiye mwanachama pekee wa EAC katika SADC.
 
Hizi jumuiya ni za kukaa na kunywa pombe na mademu tu hakuna cha maana
Waafrika huwa hatujifunzi Warundi wanaona kuwa Tanzania ambayo imo kwenye jumuiya mbili kwa mpigo na bado ni maskini na wao wanataka kujiunga na hizi jumuiya za porojo.
Hakuna la maana huku..bakini tu kivyenu
Mmeropoka (samahi kama nimewaudhi)...

Burundi anafanya hivi ili kutafuta ulinzi kwasababu Rwanda anamuonea sana,..

Kama unakumbuka Second Congo War (kabila) aliokolewa na SADC.

Pia kwa m23 ,Congo iliokolewa na SADC, Rwanda anafanya chokochoko kwa mwenzie ili amuweke mtutsi pale Burundi, na hata ukiangalia sababu ya Burundi kukataliwa ni 'mahusiano mabaya na Rwanda'...

Hata haya matokeo usikute yapo influenced na Kagame kama mnavyomjua alivyo master mind, anajua fika Burundi akijiunga SADC hatoweza kumgusa wala kumletea vurugu tena.......
 
Mmeropoka (samahi kama nimewaudhi)...

Burundi anafanya hivi ili kutafuta ulinzi kwasababu Rwanda anamuonea sana,..

Kama unakumbuka Second Congo War (kabila) aliokolewa na SADC.

Pia kwa m23 ,Congo iliokolewa na SADC, Rwanda anafanya chokochoko kwa mwenzie ili amuweke mtutsi pale Burundi, na hata ukiangalia sababu ya Burundi kukataliwa ni 'mahusiano mabaya na Rwanda'...

Hata haya matokeo usikute yapo influenced na Kagame kama mnavyomjua alivyo master mind, anajua fika Burundi akijiunga SADC hatoweza kumgusa wala kumletea vurugu tena.......
Hizo ni akili za kitwana mbona Burundi inashindwa kusimama pekee yake mbele ya Rwanda.

Nchi zenyewe ziko karibia sawa kwa idadi ya watu na nguvu.
 
Mmeropoka (samahi kama nimewaudhi)...

Burundi anafanya hivi ili kutafuta ulinzi kwasababu Rwanda anamuonea sana,..

Kama unakumbuka Second Congo War (kabila) aliokolewa na SADC.

Pia kwa m23 ,Congo iliokolewa na SADC, Rwanda anafanya chokochoko kwa mwenzie ili amuweke mtutsi pale Burundi, na hata ukiangalia sababu ya Burundi kukataliwa ni 'mahusiano mabaya na Rwanda'...

Hata haya matokeo usikute yapo influenced na Kagame kama mnavyomjua alivyo master mind, anajua fika Burundi akijiunga SADC hatoweza kumgusa wala kumletea vurugu tena.......

So hiyo ni jumuiya ya kivita!
 
UMOJA WOWOTE AFRICA HAUNA NGUVU ,NI KAMA NZI WANAOJIKUSANYA PAMOJA UKICHUKUA JIWE NA KUWARUSHIA WANATAWANYIKA KILA MTU KIVYAKE....:D:D
cc AU>>>>>libya
nilitamani sana AFRICA-1,318,377,648 iwe nchi moja tuwe na population kubwa kama USA-328,973,782 na tutashindana kiuchumi vizuri.CHINA--1,419,805,194
 
Kwani Ecomog walivyoenda kumtoa Yahya Jammeh, ni jumuiya ya kivita.???

Soma Uzi nilioquote, kasema Burundi inasaka kinga ya kunyanyaswa na Rwanda. Yaani ndio hasa cha msingi Burundi inachosaka huko SADC.
 

Burundi imekwama kujiunga na Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kuelezwa kuwa imeshindwa kutimiza vigezo vya kuwa mwanachama.

Kupitia taarifa ya Mwenyekiti wa SADC, Rais wa Namibia, Hage Geingob (pichani) iliyotolewa hivi karibuni, Burundi haijakidhi vigezo.

Taarifa hiyo imesema wataalamu wa masuala ya diplomasia waliopewa jukumu la kuyafanyia tathimini maombi ya Burundi wamejiridhisha kuwa bado taifa hilo la Afrika Mashariki halijapata baraka za kujiunga SADC.

Imesema hali ya uhusiano na nchi jirani ikiwemo Rwanda ni miongoni mwa dosari za kutokamilika kwa vigezo vya kujiunga SADC. Tathmini ya mwisho ya Burundi ilifanyika kati ya Mei 18 na 25, mwaka huu.

Kama ingekubaliwa, Burundi ingekuwa mwanachama wa pili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kujiunga SADC. Tanzania ndiye mwanachama pekee wa EAC katika SADC.
Acha uongo.....Kenya pia yupo SADC
 
Acha uongo.....Kenya pia yupo SADC
SADC ya Tandahimba labda

SADC (Southern African Development Community) is a regional organisation consisting of 14 Member Countries (Angola, Botswana, Congo (DR), Lesotho,Malawi, Mauritius, Mozambique, Namibia, Seychelles, South Africa, Swaziland,Tanzania, Zambia and Zimbabwe). Seychelles is still in the process of ratifying the SADC Treaty.
 
Back
Top Bottom