Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Burundi imekwama kujiunga na Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kuelezwa kuwa imeshindwa kutimiza vigezo vya kuwa mwanachama.
Kupitia taarifa ya Mwenyekiti wa SADC, Rais wa Namibia, Hage Geingob (pichani) iliyotolewa hivi karibuni, Burundi haijakidhi vigezo.
Taarifa hiyo imesema wataalamu wa masuala ya diplomasia waliopewa jukumu la kuyafanyia tathimini maombi ya Burundi wamejiridhisha kuwa bado taifa hilo la Afrika Mashariki halijapata baraka za kujiunga SADC.
Imesema hali ya uhusiano na nchi jirani ikiwemo Rwanda ni miongoni mwa dosari za kutokamilika kwa vigezo vya kujiunga SADC. Tathmini ya mwisho ya Burundi ilifanyika kati ya Mei 18 na 25, mwaka huu.
Kama ingekubaliwa, Burundi ingekuwa mwanachama wa pili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kujiunga SADC. Tanzania ndiye mwanachama pekee wa EAC katika SADC.