Burundi: Spika ataiongoza nchi baada ya kifo cha Rais Pierre Nkurunziza

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Burundi yatangaza siku saba za kuomboleza kifo cha Rais Nkurunziza

Serikali ya Burundi imetangaza maombolezo ya kitaifa ya siku 7 kufuatia kifo cha rais wake Pierre Nkurunziza, aliyeaga dunia Jumatatu akiwa na umri wa miaka 55 kutokana na mshituko wa moyo.

Präsident Burundis Pierre Nkurunziza (Reuters/E. Ngendakumana)

Tangazo la serikali kwenye Redio na Televisheni ya taifa lililosomwa na msemaji wake Prosper Ntahorwamiye ambaye pia ni Katibu mkuu wa serikali lilisema Nkurunziza alifariki dunia kutokana na mshituko wa moyo katika hospitali ya mkoani Karuzi.

Kulingana na katiba ya Burundi spika wa Bunge Pascal Nyabenda ndiye atakayeshika hatamu za uongozi kwa kipindi cha miezi miwili hadi atakapotawazwa Evariste Ndayishimiye aliyeibuka na ushindi kwenye uchaguzi wa rais wa Mei 20 mwaka huu.

Hata hivyo taarifa nyingine zinasema muhula wa bunge ulimalizika tangu April 27 ilipozinduliwa kampeni ya uchaguzi hivyo ni makamu wa rais atakayeshika hatamu.

Nkurunziza aliiongoza Burundi kwa kipindi cha miaka 15.

DW

Pia Soma: News Alert: - Serikali ya Burundi yatangaza kifo cha Rais Pierre Nkurunziza
 
Sasa Kama RAIS mteule yupo.... Kwa nini wanaongelea kipindi cha mpito cha miezi 2!?

Kwa nini Wasingefanya haraka wakamwapisha RAIS mteule.....!

Wanajifanya wamekua Nchi za Ulaya kwamba Democracy imetamalaki....
Nchi yenyewe ile Kila mtu anataka kuwa RAIS.
Hahaha

Mkuu utaratibu uloekwa nahisi ndio unafuatwa ila nahisi walitakiwa waweke kamati yamaridhiano kuuvunja utaratibu uliokuwepo kwadharura maadam RAIS alikua tayari yupo

Siasa za Afrika zilivyo zakipumbavu mara jamaa anagoma kutoka katika kiti ukifika wakati wake

Mungu awavushe hapa hawa jamaa maana wanakipengele kigumu sana
 
Kwa siasa za Africa huyo Gaston Sindimwo aliyepewa mamlaka kuongoza kipindi cha mpito anaweza kung'ang'ania madaraka jumla ukizingatia anatoka UPRONA na si chama tawala CNDD-FDD!

Ngoja tuone!
 
Kuna mgogoro hapo?

Ni Spika ama Makamu wa Rais anayechukua nafasi hiyo?

Ila yasije kutokea ya Ntibantunganya!!
 
Agaton Rwasa ni naibu spika eh? na ndio mshindi wa pili kwenye uchaguzi uliopita
 
Upande uleee daah haya ya Mungu mengi, huenda mabadiliko makubwa mno yakatokea mmmh daah ngoja ninyamaze nimechoka safari ndefu nitaongea nikioga
 
Kwa siasa za Africa huyo Makamu wa kwanza wa Rais aliyepewa mamlaka kuongoza kipindi cha mpito anaweza kung'ang'ania madaraka ukizingatia hatoki chama tawala.

Ngoja tuone!
Hhata mie natabiri haya MKUU.....
 
Back
Top Bottom