Burundi imejitoa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,551
Burundi. Sasa ni rasmi kwamba Burundi imekuwa nchi ya kwanza mwanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kujiondoa ikiwa ni mwaka mmoja tangu ilipowasilisha maombi yake.


Oktoba 27, 2016, Burundi iliwasilisha barua kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Ban Ki-moon ikieleza kuhusu kusudio la kuanza mchakato wa mwaka mmoja kujiondoa. Burundi ilichukua uamuzi huo baada ya mahakama hiyo kuanzisha juhudi za kuchunguzi juu ya uwezekano wa kuwepo uhalifu wa kivita zilipoibuka vurugu mwaka 2015 wakati Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwania muhula wa tatu

Pia, Gambia chini ya mtawala wa zamani aliyeko uhamishoni sasa Yahya Jammeh alianzisha mchakato wa kujiondoa ICC akilalamikia upendeleo kwa kutofanya uchunguzi na hatimaye kushtaki uhalifu unaofanywa nan chi za magharibi badala yake mahakama hiyo imejikita Afrika tu.

Lakini rais mpya wa taifa hilo Adama Barrow alitengua noti ya kujitoa iliyowasilishwa na Jammeh.
Umoja wa Afrika (AU) ulihamasisha nchi zote za Afrika kujiondoa katika mkutano wa mwaka ukidai kwamba mahakama hiyo haitendi haki kwa kushughulikia uhalifu wa bara la Afrika tu. Uamuzi huo ambao haukuwa shuruti la kisheria kwa utekelezaji ulipingwa na Nigeria na Senegal.


Kenya na Uganda pia zilitishia kujiondoa ICC wakati Zambia ilianzisha mchakato wa kupata maoni nchi nzima ikiwa iamue kujiondoa au ibaki kuwa mwanachama. Asilimia 93.3 ya waliotoa ushauri wao wamesisitiza nchi ibaki kuwa mwanachama ICC.


Afrika Kusini ilianzisha mchakato rasmi wa kujitoa mwaka 2016, hivyo kuwa nchi ya pili kuomba kujiondoa kwenye Mkataba wa Roma uliounda mahakama hiyo.


Lakini Mahakam Kuu ya Afrika Kusini mwaka huu 2017 ilisema uamuzi wa serikali kujiondoa ICC ulikuwa kinyume cha katiba na batili.


Pamoja na Burundi kujitoa, bado ICC ina uwezo kuchunguza uhalifu uliotekelezwa wakati ilipokuwa mwanachama wa mahakama hiyo. Lakini haiwezi kuchunguza uhalifu wowote wa siku zijazo.
 
nchi gani itafuata?
Sasa hivi watu watashangilia kwa sababu ya unazi wa kisiasa lakini mbele ya safari kutakuwa na majuto makuu. Matokeo yake ndiyo mwanzo wa kuanzishwa vikundi cha ughaidi na watu viongozi wataua watu bila wasiwasi na watu watachoka wataanzisha vijeshi vyao. Sasa hivi wako makini kidogo kwasababu wanaogopa kesi.
Waafrika bila kuwepo chombo cha kutudhibiti na hatari nchi hazita tawalika
 
Burundi. Sasa ni rasmi kwamba Burundi imekuwa nchi ya kwanza mwanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kujiondoa ikiwa ni mwaka mmoja tangu ilipowasilisha maombi yake.


Oktoba 27, 2016, Burundi iliwasilisha barua kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Ban Ki-moon ikieleza kuhusu kusudio la kuanza mchakato wa mwaka mmoja kujiondoa. Burundi ilichukua uamuzi huo baada ya mahakama hiyo kuanzisha juhudi za kuchunguzi juu ya uwezekano wa kuwepo uhalifu wa kivita zilipoibuka vurugu mwaka 2015 wakati Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwania muhula wa tatu

Pia, Gambia chini ya mtawala wa zamani aliyeko uhamishoni sasa Yahya Jammeh alianzisha mchakato wa kujiondoa ICC akilalamikia upendeleo kwa kutofanya uchunguzi na hatimaye kushtaki uhalifu unaofanywa nan chi za magharibi badala yake mahakama hiyo imejikita Afrika tu.

Lakini rais mpya wa taifa hilo Adama Barrow alitengua noti ya kujitoa iliyowasilishwa na Jammeh.
Umoja wa Afrika (AU) ulihamasisha nchi zote za Afrika kujiondoa katika mkutano wa mwaka ukidai kwamba mahakama hiyo haitendi haki kwa kushughulikia uhalifu wa bara la Afrika tu. Uamuzi huo ambao haukuwa shuruti la kisheria kwa utekelezaji ulipingwa na Nigeria na Senegal.


Kenya na Uganda pia zilitishia kujiondoa ICC wakati Zambia ilianzisha mchakato wa kupata maoni nchi nzima ikiwa iamue kujiondoa au ibaki kuwa mwanachama. Asilimia 93.3 ya waliotoa ushauri wao wamesisitiza nchi ibaki kuwa mwanachama ICC.


Afrika Kusini ilianzisha mchakato rasmi wa kujitoa mwaka 2016, hivyo kuwa nchi ya pili kuomba kujiondoa kwenye Mkataba wa Roma uliounda mahakama hiyo.


Lakini Mahakam Kuu ya Afrika Kusini mwaka huu 2017 ilisema uamuzi wa serikali kujiondoa ICC ulikuwa kinyume cha katiba na batili.


Pamoja na Burundi kujitoa, bado ICC ina uwezo kuchunguza uhalifu uliotekelezwa wakati ilipokuwa mwanachama wa mahakama hiyo. Lakini haiwezi kuchunguza uhalifu wowote wa siku zijazo.
the bad thing on their side ni kwamba, ICC bado ina uwezo kushitaki warundi kama raia yeyote wa nchi iliyosaini mkataba wa Roma amekuwa persecuted akiwa Burundi, au Mrundi yeyote amefanya kosa linalodondokea kwenye ICC statute kwenye nchi iliyosaini mkataba wa Roma (Rome Statute of International Criminal Court). nchi zilizowazunguka Burundi hazijajitoa hivyo endapo mrundi atafanya kosa linalodondokea kwenye nchi hizo hata akikimbilia burundi atatakiwa kukamatwa, au endapo mtu toka nchi zilizosaini ataenda Burundi makosa yanayodondokea kwenye statute yafanyika juu ya huyo mtu, perpetrators hata kama ni warundi au rais, atatakiwa kukamatwa. hivyo hawajakwepa sana mkono wa ICC.

haimaanishi warundi wameshakuwa immune na ICC absolutely.
 
ICC is a second face of NEO- COLONIALSM
ni kwasababu tu haujaijua ICC mkuu. ukija kuijua, hautakaa uongee hivyo tena. viongozi wa africa kama hakuna hata mtu anayewatisha kidogo, wanaweza kufanya chochote wapendacho. siku uje utekwe na noah, siku uje ufanyiwe uonevu wa hali ya juu na serikali yako na hakuna hata pa kukimbila zaidi ya kushitaki kwa Mungu pekee...hapo utaelewa. utakuja kuelewa kumbe wakati mwingine Mungu anaweza kutumia kitu chochote hata kama ni kiovu ili kuokoa haki za baadhi ya watu. kipindi cha zamani Mungu alitumia hadi maadui wa israel ili kuwaadhibu waisrael wakae kwenye mstari. sio kila kitu kibaya machoni pako hakina matumizi.
 
ni kwasababu tu haujaijua ICC mkuu. ukija kuijua, hautakaa uongee hivyo tena. viongozi wa africa kama hakuna hata mtu anayewatisha kidogo, wanaweza kufanya chochote wapendacho. siku uje utekwe na noah, siku uje ufanyiwe uonevu wa hali ya juu na serikali yako na hakuna hata pa kukimbila zaidi ya kushitaki kwa Mungu pekee...hapo utaelewa. utakuja kuelewa kumbe wakati mwingine Mungu anaweza kutumia kitu chochote hata kama ni kiovu ili kuokoa haki za baadhi ya watu. kipindi cha zamani Mungu alitumia hadi maadui wa israel ili kuwaadhibu waisrael wakae kwenye mstari. sio kila kitu kibaya machoni pako hakina matumizi.
swali kubwa ni kwamba... kwanini ribo tatu ya watuhumiwa ktk mahakama ya ICC ni Waafrika?! kwani weupe wao hawana wahalifu wanaostahili kufikishwa ICC?!
 
swali kubwa ni kwamba... kwanini ribo tatu ya watuhumiwa ktk mahakama ya ICC ni Waafrika?! kwani weupe wao hawana wahalifu wanaostahili kufikishwa ICC?!
Asilimia za nchi zilizoendelea zinafuata sheria. Hata Tanzania ilikuwa mojawapo za nchi ambazo lilikuwa makini kwenye demokrasia na haki za raia wake ukilinganisha na nchi nyingi za waafrika.
Kwa hiyo ilikuwa ni ndoto kufikiria siku moja Tanzania itashitakiwa ICC. Ndiyo maana Kagame na Kikwete walikuwa mahasimu kwa sababu Kikwete hakuupenda mwenendo wa Kagame.
 
ni kwasababu tu haujaijua ICC mkuu. ukija kuijua, hautakaa uongee hivyo tena. viongozi wa africa kama hakuna hata mtu anayewatisha kidogo, wanaweza kufanya chochote wapendacho. siku uje utekwe na noah, siku uje ufanyiwe uonevu wa hali ya juu na serikali yako na hakuna hata pa kukimbila zaidi ya kushitaki kwa Mungu pekee...hapo utaelewa. utakuja kuelewa kumbe wakati mwingine Mungu anaweza kutumia kitu chochote hata kama ni kiovu ili kuokoa haki za baadhi ya watu. kipindi cha zamani Mungu alitumia hadi maadui wa israel ili kuwaadhibu waisrael wakae kwenye mstari. sio kila kitu kibaya machoni pako hakina matumizi.
Mbona nyerere hajapelekwa icc kwa uhalifu aliofanya kabla haja ng'atuka
 
Asilimia za nchi zilizoendelea zinafuata sheria. Hata Tanzania ilikuwa mojawapo za nchi ambazo lilikuwa makini kwenye demokrasia na haki za raia wake ukilinganisha na nchi nyingi za waafrika.
Kwa hiyo ilikuwa ni ndoto kufikiria siku moja Tanzania itashitakiwa ICC. Ndiyo maana Kagame na Kikwete walikuwa mahasimu kwa sababu Kikwete hakuupenda mwenendo wa Kagame.
Tony Blair alikiri hadharani kuwa alichofanya Iraq ni uhalifu wa kivita, kuna hata aliyenyanyua mdomo kuwa ashitakiwe hata akitokea ataonekana kituko.
Pamoja na matatizo yaliyopo Africa bado sioni uwepo wa hiyo mahakama kama umesaidia chochote , sana sana kibaraka wao wakishamchoka ndio wanamsukumia huko kama wakina Laurent gbabo na Charles Taylor .
Dunia ya unafki,samaki mkubwa amle mdogo ,mwenye nguvu mpishe aende zake.
 
swali kubwa ni kwamba... kwanini ribo tatu ya watuhumiwa ktk mahakama ya ICC ni Waafrika?! kwani weupe wao hawana wahalifu wanaostahili kufikishwa ICC?!
Huu huwa ni utetezi dhaifu sana. Kutokufanya makosa kwa wazungu au mabara mengine hakuhalalishi uovu wa Waafrika. Waafrika, hasa viongozi ni viumbe wa hovyohovyo mnoo. Sitoi mifano, wanafahamika.
 
Tujitoeni.
Kujitoa kwa Tanzania ni faida kwa wanasiasa haijalishi wa chama tawala au upinzani ila ni kilio kwa watawaliwa kwani kila kiongozi wa siasa atafanya juhudi zake kiharamia haijalishi nani ana kufa.
Kiongozi akiwa dikteta ndiyo anaweza hata kuua watu hadharani si kwa kificho maana hamna mtu wa kumfanya kitu dola iko chini yake.
Watu wakichoka wanaingia misituni kwa heri amani
 
Sawa tu,
Mbona USA siyo mwanachama wa ICC, USA kakataa makubaliano ya mabadiliko ya tabia ya nchi na juzi kati hapa kajitoa UNESCO.

Kwa hiyo, kila Taifa liishi lipendavyo siyo watu tushikiwe akili na nchi au mataifa mengine.
 
swali kubwa ni kwamba... kwanini ribo tatu ya watuhumiwa ktk mahakama ya ICC ni Waafrika?! kwani weupe wao hawana wahalifu wanaostahili kufikishwa ICC?!
Weupe hawafanyi mambo wanayoyafanya viongozi wa africa. mtaje mmoja tu walau unayemfahamu, na utakapotaja hakikisha unamtaja aliyefanya maovu kuanzia July, 1, 2002 wakati Rome Statute of International Criminal Court ilipoanza kufanya kazi na sio kabla ya hapo). just mention one.

alafu, hata kama wangekuwa wanapelekwa waafrica tu, kwani what do you lose, kama wamefanya makosa si wapelekwe ili kupunguza uonevu kwenye nchi zetu? au kwasababu wazungu hauwaoni kule basi unaona bora hata waafrica waonewe tu na viongozi wao ili wote tuikose , nani ana lose zaidi kati yako na wazungu?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom