MENGELENI KWETU
JF-Expert Member
- May 8, 2013
- 9,548
- 24,159
Salute sanaaa Mkuu..Mwaka 2002, nilikuwa jijini Santiago kikazi. Nilijumuika na watu wengi toka pande mbalimbali za Dunia. Mmoja wa niliyejumuika naye alikuwa ni ofisa mmoja wa kutoka Indonesia. Wakati huo Indonesia ilikuwa haijapita muda mrefu tangu wamchague Waziri Mkuu.
Wakati huo, kwenye hoteli ile kulikuwa na King Hassan wa Jordan, na George Bush aliondoka siku mimi nilipoingia. Ni hoteli ambayo wakubwa wa Dunia walipenda kufikia, na gharama yake haikuwa haba.
Wakati fulani wa maongezi, nikiwa nimesimama na yule ofisa wa Indonesia, afisa wa juu wa Serikali ya Canada, akamwambia yule afisa wa kutoka Indonesia, 'this time you have a got a very good Prime Minister', yule Muindonesia akasema, 'you are right'. Kisha yule afisa wa juu wa Canada, akasema, 'but I assure you, he is not as good as this genteman's President, President Benjamin William Mkapa.
Last week Benjamin Mkapa was in Toronto, he addresed like the President of Africa. He spoke on behalf of Africa. We were expecting such a speech from Thabo Mbeki, but it was Benjamin Mkapa who made it. He is an exceptional leader. He has made what even the First World Presidents cannot. Can you imagine, lowering inflation from 30% down to 4%, that had never happened anywhere but Benjamin has done it. Unfortunately, I do not think the Africans understand the greatness of Benjamin. Had it been in any American or European countries - he would be in success records'.
Nilimjua Mkapa kwa mbali sana. Niliijua kazi aliyoifanya Mkapa, hasa kwenye uchumi wa nchi yetu lakini sikufikiria kuwa alichokifanya kilikuwa ni cha pekee sana Duniani.
Ni Mkapa ndiye aliyesimamia sera ya uwekezaji. Kuna watu wajati wa uhai wake wamekuwa kuhusu uwekezaji kwenye sekta ya madini, na kuashiria kuwa aliuza rasilimali za Taifa kwa mabeberu. Lakini kwa dhamira ya moyo wangu kabisa, na kwa kumheshimu Mungu aliyeniumba, nina hakika Rais Mkapa alikuwa mzalendo wa kweli wa nchi yetu. Uwekezaji kwenye sekta ya madini, haukuwa na rushwa yoyote wala dhamira yoyote ya kuangamiza Taifa.
Naikumbuka hotuba aliyoitoa Mkapa pale Bulyanhulu, mbele ya Watanzania na Balozi wa Kudumu wa Marekani, Andrewa Young, 'to make an investor come to Tanzania, not to South America, Asia or even Kenya, where there is electricty, good roads, assured communication facilities, instead come to Tanzania where all the necessary enabling infrastructure is missing, there is a price to pay, and my government has accepted it".
Mkapa wakati huo alikuwa akigangaika kupata hrla ya kuendeshea Serikali. Wakati Mkapa anaingia madarakani, hata mishahara ya wafanyakazi wa umma ilikuwa inakosekana. Mwezi wa 7, mfanyakazi analipwa mshahara wa mwezi wa 5 au 6. Mkapa aliondoka madarakani wafanyakazi wote wa umma wakilipwa kwa wakati.
Ukitaka kumjua kiongozi mzuri, uone atafanya nini wakati nchi ikiwa katika matatizo. Mkapa aliweza kuonesha uwezo wake wa kuitoa nchi kwenye dimbwi la dhiki kubwa. Mkapa hakuwahi kuhangaikia sifa bali alihangaikia mafanikio ya nchi.
Ni bahati mbaya sana watanzania huwa tunavutika na kushawishika kwa vitu vidogo vidogo, huku makubwa tukiyapa umuhimu mdogo.
Sina nia ya kumlaumu mtu lakini kama kuna kitu ambacho mpaka leo huwa najiuliza, sipati jibu, ni mtazamo wa Serikali ya awamu ya 5 kuamini kuwa hakuna makubwa yaliyowahi kufanyika awamu zilizopita. Wanataka kuwaaminisha watu kuwa mambo makubwa, mazuri na ya ajabu yamefanyika awamu hii. Lakini kwa hakika misingi muhimu ya uchumi wa kisasa kwa Tanzania, iliwekwa na Mkapa.
Mkapa aliuchukua uongozi wa nchi, hazina ikiwa ina zero balance. Akaondoka akiwa ameacha $5 billion. Ni Mkapa ndiye aliyejenga taasisi imara za utawala, uongozi na za kusimamia uchumi. Ni Mkapa ndiye aliyeifanya sekta binafsi kuwa mhimili wa uchumi. Ni Mkapa aliyeingia madarakani $1 = TZS 800; akaishusha mpaka $1 = 500. Mwinyi aliipandisha $1 = TZS 5 mpaka $1=TZS 800.
Hakuna mtawala mwingine yeyote aliyeweza kupandisha thamani ya shilingi dhidi ya sarafu nyingine kubwa za Dunia kama alivyofanya Mkapa.
Niliwahi kukutana na kiongozi mmoja aliyehudumu kipindi cha Mkapa, Kikwete na Magufuli - alisema, 'katika awamu zote, ni kipindi cha Makapa pekee, ukitaka kufanya maamuzi unaangalia sheria, kanuni na miongozo. Huna haja ya kumwuliza mkubwa wako. Leo ukijifanya kuangalia sherua na kanuni bila kujitahidi mkubwa anataka nini, umeebda na maji".
Yale maelezo ya Mkanada na huyu afisa kiongozi wa Serikali, yanadhihirisha kuwa Mkapa alikuwa Kiongozi. Kiongozi hutengeneza mifumo. Mifumo huwatengeneza viongozi wengi na kuwapa moyo wa kujiamini katika kutenda kazi zao.
Watawala badala ya kujenga mifumo, huyajenga majina yao. Hawapendi kujenga mifumo kwa sababu mifumo hutoa nafasi ya watu wengine kuonesha umahiri wao. Watawala hupenda wasifiwe wao tu. Hawataki kujenga mifumo ambayo huwajenga watu wengi, na kuyainua majina yao.
Mpendwa ndugu yetu Rais Mstaafu Mkapa, umeimaliza safari yako. Umeziacha nyayo zako Duniani. Wapo watakaopenda kuzifuta lakini hawataweza kwa sababu nyayo zako zimechapwa kwenye miamba kwa kutumia wino usiofutika.
Mazuri ya Mkapa, ni zawadi ya Mungu kwetu tunaoebdelea kuishi.
Kwa watawala waliopo sasa na wajao, wasiyanene mazuri ya Mkapa kama hadithi bali waweke dhamira ya kuyaiga na kuyaishi. Watakapoyaishi watakuwa wanamuenzi Mungu ambaye hugawa karama fulani kwa kila mwanadamu ili zikijumuika pamoja zimtunze, zimjenge na zimlinde mwanadamu.
Makala nzuri sana.