Bungeni: Wabunge wa CCM na hoja ya Upigaji kura wa Bajeti.

residentura

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
6,969
9,516
Wakuu,nimeona wabunge wa CCM wakiomba muongozo wa kwa nini wabunge waliopiga kura ya Hapana kwa bajeti wasinyimwe pesa ya hiyo bajeti na wasiruhusiwe kuhoji maswala yoyote yahusuyo maendeleo yanayotokana na bajeti hii waliyoikataa.
Je,hii ni haki na halali kisheria?
 
CCM hawajui maana ya uchaguzi au kupiga kura. Kwao kupiga kura ni kusema 'ndiyo'. Hawajui kwamba 'hapana' ni sehemu ya kupiga kura. Ila siyo kosa lao maana utafiti wa Twaweza, ambao CCM wamekubaliana nao 100%, unasema hicho chama kinaungwa mkono na wenye elimu duni na vikongwe.
 
Wakuu,nimeona wabunge wa CCM wakiomba muongozo wa kwa nini wabunge waliopiga kura ya Hapana kwa bajeti wasinyimwe pesa ya hiyo bajeti na wasiruhusiwe kuhoji maswala yoyote yahusuyo maendeleo yanayotokana na bajeti hii waliyoikataa.
Je,hii ni haki na halali kisheria?
ccm kila mtu anajitahidi kufanana na jpm, hata wale tuliowaona kama wana hekima kidogo
 
Hata hivyo wametoa hoja tu si sheria.. so wapinzani bado wanahaki ya kusema hapana au ndio..
 
Wakuu,nimeona wabunge wa CCM wakiomba muongozo wa kwa nini wabunge waliopiga kura ya Hapana kwa bajeti wasinyimwe pesa ya hiyo bajeti na wasiruhusiwe kuhoji maswala yoyote yahusuyo maendeleo yanayotokana na bajeti hii waliyoikataa.
Je,hii ni haki na halali kisheria?

Kwa nini kabla ya upigaji kura ilisemwa aina tatu za kura - ndiyo, kutokupiga au hapana - kama wanadhani wote ni lazima wapitishe bajeti? Naona kama ni mwelekeo mpya wa demokrasia Tanzania, ambayo haina hapana isipokuwa ndiyo tu!
 
Hujui % ya wabunge wa CCM ni vichwa maji wao ni kuongea pumba na kupitisha ndioo kila kitu
 
CCM hawajui maana ya uchaguzi au kupiga kura. Kwao kupiga kura ni kusema 'ndiyo'. Hawajui kwamba 'hapana' ni sehemu ya kupiga kura. Ila siyo kosa lao maana utafiti wa Twaweza, ambao CCM wamekubaliana nao 100%, unasema hicho chama kinaungwa mkono na wenye elimu duni na vikongwe.
Mbona huko CHADEMA mnamwambia MBOWE Ndiooooo kwa kila kitu mkitoka nje, mnajipa UJASIRI KOKO
 
Wakuu,nimeona wabunge wa CCM wakiomba muongozo wa kwa nini wabunge waliopiga kura ya Hapana kwa bajeti wasinyimwe pesa ya hiyo bajeti na wasiruhusiwe kuhoji maswala yoyote yahusuyo maendeleo yanayotokana na bajeti hii waliyoikataa.
Je,hii ni haki na halali kisheria?

Kwa yale niliyosikia yakisemwa, wakitoka hapo watakuja pia kwa Rais kwamba wasiomchagua wasipate maendeleo. Ukianza na sehemu moja lazima uendelee na kwingine na hivyo tutakuwa taifa la ndiyo for everything bila kuhoji.
 
Kwa ccm wako sawa maana wenzetu hawa wamelelewa kwenye mazingira ya kukubali tu yaan ilee ya ndiyooooooo...tunawabia madini ndioooooo..tunaiba gesi..ccm ndiooooooo...tunabeba wanyama hai. Ccm ndiooooooo...katiba feki. Ccm..ndiooooo. wazee wa ndio ni kawaida sana kuwashangaa wenzao wanavyosema hapana. CCM KWA HILI WAKO SAWA
 
Mbona huko CHADEMA mnamwambia MBOWE Ndiooooo kwa kila kitu mkitoka nje, mnajipa UJASIRI KOKO
Mbowe hana madhara kwa taifa acha ujinga. Ruhusa ata nyie kumwambia magu ndiooooooo miaka yote pale lumumba wala hatutajal
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom