Bungeni: Upinzania umeibua issue ya Tovuti ya Rais na Ile ya Wananchi

Kasheshe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
4,694
787
Wanabodi,

Leo kuna kivumbi kikubwa sana bungeni, fuatiliani vizuri especially issues za Kubenea, Tovuti ya Rais na ile ya Wananchi.

Watanzania bado... wizara ya habari bajeti yake haiko kwenye tovuti yao... angalia
 
Ndio nawapongeza upinzani kwani haiwezekani akawepo mkurugenzi wa habari ikulu huku hana jipya la kuiweka hata tovuti ya ikulu on air?

Huyu ni bora aitwe mwandishi wa rais kama alivyokuwa Maura mwingira, na sio kuanzisha vyeo bila tija kisa eti alikuwa mtandao...
 
Ndio nawapongeza upinzani kwani haiwezekani akawepo mkurugenzi wa habari ikulu huku hana jipya la kuiweka hata tovuti ya ikulu on air?

Huyu ni bora aitwe mwandishi wa rais kama alivyokuwa Maura mwingira, na sio kuanzisha vyeo bila tija kisa eti alikuwa mtandao...

Tehe...tehe...tehe...

Tanzanianjema
 
Mdau Zitto Kabwe anachangia muda si mrefu... ndani ya dakika 15 zijazo... stay tuned!
 
E-mail yao hii hapa waandikie info@ikulu.go.tz

Mie niko Tayari kutoa Pesa ya Kutengenezea Tovuti ya Ikulu.Watu wa saqqa ni dola 500.Mie nitawapa kama Serikali ikisema haina Pesa ya kutengeneza hiyo Tovuti.Kila siku wana fanya semina bila Mpango wowote na zinagharimu pesa nyingi.Hili hwalioni
 
Zitto: Financing ya TBC and TSN ndio issue kubwa kutoka kwa Mbunge huyu.
 
Zitto: Financing ya TBC and TSN ndio issue kubwa kutoka kwa Mbunge huyu.

Anasema pia kuhusiana na wamiliki wa vyombo vya habari kuwa na nguvu za kuwafukuza kazi waandishi kwa kuwa tuu wanamiliki vyombo hivyo.

Amezungumzia pia kuwa haiwezekani TBC wakawa wanapewa fedeha za umma na wakati huo huo wao wanaenda kushindana na mashirika binafsi kufanya biashara .

Amezungumzia pia kumpongeza Vicky Ntetema kwa kazi nzuri na kuitaka serikali kuwalinda waandishi wa habari.

Amezungumzia pia kuhusiana na wasanii na hati miliki zao kwani wanafanya kazi ila wao hawanufaiki moja kwa moja,ila promoters et all ndio wananufaka.

Na pia alimtaka Spika awatake front bench wawe na nidhamu kwani walikuwa wanazomea wakati akizungumza na jueni kuwa front Bench ni Mawaziri, na Spika aliwaambia hawana haki ya kufanya hivyo.....
 
Anasema pia kuhusiana na wamiliki wa vyombo vya habari kuwa na nguvu za kuwafukuza kazi waandishi kwa kuwa tuu wanamiliki vyombo hivyo.

Amezungumzia pia kuwa haiwezekani TBC wakawa wanapewa fedeha za umma na wakati huo huo wao wanaenda kushindana na mashirika binafsi kufanya biashara .

Amezungumzia pia kumpongeza Vicky Ntetema kwa kazi nzuri na kuitaka serikali kuwalinda waandishi wa habari.

Amezungumzia pia kuhusiana na wasanii na hati miliki zao kwani wanafanya kazi ila wao hawanufaiki moja kwa moja,ila promoters et all ndio wananufaka.

Na pia alimtaka Spika awatake front bench wawe na nidhamu kwani walikuwa wanazomea wakati akizungumza na jueni kuwa front Bench ni Mawaziri, na Spika aliwaambia hawana haki ya kufanya hivyo.....

Hii ni safi sana,TBC wamekuwa na kiburi sana...
Kwa wale mnaotaka E-mail ya salva ni srweyemamu@ikulu.go.tz
 
NI MCHANGO WA KAMBI YA UPINZANI KWENYE HOTUBA YAO NILIYOIPATA PUNDE.

56. Mheshimiwa Spika, tatizo la tovuti hii linafanana sana na ile ya Ikulu ambayo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa haifanyi kazi pamoja na ukweli kuwa hivi sasa kuna Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Ikulu ambaye analipwa fedha za walipa kodi kwa ajili ya kuwapatia wananchi habari mbalimbali .
57. Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani pamoja na kutambua kuwa Tovuti hii ipo chini ya Ofisi ya Rais inatambua pia kuwa jukumu la kuhabarisha umma lipo chini ya wizara ya habari. Hatuoni umuhimu wa Kuwepo na Mkurugenzi wa Habari kama utendaji kazi wake ndio huu , tunashauri kuwa badala ya kuanzisha vyeo ambavyo havina ufanisi katika utendaji basi sasa ni wakati wa kurudisha utamaduni wa hapo awali wa kuwa na mwandishi wa habari wa Rais na huku majukumu mengine yakiwekwa chini ya wizara hii .
 
Last edited:
NI MCHANGO WA KAMBI YA UPINZANI KWENYE HOTUBA YAO NILIYOIPATA PUNDE.

56. Mheshimiwa Spika, tatizo la tovuti hii linafanana sana na ile ya Ikulu ambayo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa haifanyi kazi pamoja na ukweli kuwa hivi sasa kuna Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Ikulu ambaye analipwa fedha za walipa kodi kwa ajili ya kuwapatia wananchi habari mbalimbali .
57. Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani pamoja na kutambua kuwa Tovuti hii ipo chini ya Ofisi ya Rais inatambua pia kuwa jukumu la kuhabarisha umma lipo chini ya wizara ya habari. Hatuoni umuhimu wa Kuwepo na Mkurugenzi wa Habari kama utendaji kazi wake ndio huu , tunashauri kuwa badala ya kuanzisha vyeo ambavyo havina ufanisi katika utendaji basi sasa ni wakati wa kurudisha utamaduni wa hapo awali wa kuwa na mwandishi wa habari wa Rais na huku majukumu mengine yakiwekwa chini ya wizara hii .

Hapa wamempiga Salva kichwani. Huyu kazi imemshinda au mazingira yale hayawezi. Yeye alifikiri ni mchezo kufanya kazi na hawa jamaa waliozoea kuishi kwa mazoea.

Cha kufurahisha ni kwamba nikisoma hapo juu ni kama nasoma JF thread, interesting, our voices are just being heard where they are supposed to be heard, it is amazing!

.....Mkuu Kasheshe, tuelezane bwana naona mwenzangu siku hizi heee...upo huko kabisa, vipi wazee wameamua kukusogeza, wasaidie bwana, mambo yao hayaendi vizuri. Help them to turn things around (LOL & JK).
 
Back
Top Bottom