Uchaguzi 2020 Bungeni: Rais Magufuli amteua Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu, Bunge zima(Wabunge 350) wampigia kura za ndiyo

Yaani hakika nimefurahi mno. Majaliwa ni best PM. Ana busara nyingi, mnyenyekevu na mtendaji.

Hongera sana Mh. Rais kwa kumuamini tena Mh. Majaliwa.

Moja ya wa wasioweza kumsaidia Rais kabisa! Mambo mengi ya serikali yanayoibuliwa na kufanywa na Rais yalipaswa kufanywa na huyu jamaa lakini kila mara yeye yuko nyuma.

Unachokiita ni unyenyekevu hasa ni uoga!
 
Karibu

Spika Ndugai amesoma Katiba kuelezea namna Waziri Mkuu anavyopatikana.

Chanzo: ITV
========

Mpambe wa Rais tayari kawasili kwenye ukumbi wa bunge akisindikizwa na askari wa bunge akiwa amebeba bahasha yenye jina la waziri mkuu ajae.

Baada ya spika Ndugai kuipokea amempa kazi katibu wa bunge kuifungua na spika Ndugai anaweka sahihi kukiri kuipokea na kumrudishia mpambe wa Rais.

Rais John Magufuli kwa mujibu wa katiba amemteua mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa kuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, zoezi litakalofuata ni wabunge kumpigia kura kumthibitisha kuwa waziri mkuu wa Tanzania.

Wabunge 350 wamepiga kura, hakuna kura ya hapana pia hamna iliyoharibika hivyo wabunge wote 350 sawa na asilimia 100 wamempigia kura za ndiyo na rasmi kuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

=====


Je, Kassim Majaliwa ni nani?

Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye anaendelea na wadhifa wa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa muhula wa pili, alizaliwa tarehe 22 Desemba mwaka 1960 yaani miaka 60 iliyopita.

Kitaaluma ni Mwalimu aliyepata elimu yake ya Ualimu katika chuo cha ualimu cha Mtwara mwaka 1991-1993, na baadae kujiendeleza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Stockholm nchini Sweden.

Kutoka mwaka 1984 mpaka 2006 amehudumu katika nafasi mbalimbali kama mwalimu na kiongozi wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT). Mwaka 2006 Majaliwa aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya na kisha akajitosa kwenye siasa za ushindani mwaka 2010 alipogombea na kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ruangwa mkoani Lindi.

Baadaye aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa serikali ya awamu ya nne.

Bw Majaliwa ameidhinishwa kuwa Waziri Mkuu na Bunge baada ya jina lake kuwasilishwa bungeni na mpambe wa rais John Magufuli na kupigiwa kura ya ndiyo na wabunge wote 350 waliokuwepo ukumbini. Anatarajiwa kula kiapo hivi karibuni ili kuanza rasmi majukumu yake.

Majaliwa alikuwa Waziri Mkuu katika kipindi chote cha miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Magufuli uliokamilika mwezi uliopita. Endapo atadumu katika wadhifa huo kwa kipindi chote cha pili cha rais Magufuli atakuwa Waziri Mkuu wa pili kuhudumu kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo. Fredrick Sumaye, ndiye mtu pekee mpaka sasa aliyehudumu kwa miaka 10 mfululizo kama Waziri Mkuu wa Tanzania kutoka mwaka 1995 mpaka 2005 chini ya rais mstaafu hayati Benjamin Mkapa.

Majaliwa alikuwa Waziri Mkuu katika kipindi chote cha miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Magufuli uliokamilika mwezi uliopita.

Uteuzi wa Majaliwa hii leo haukusthua wengi kama alivyoteuliwa mara ya kwanza miaka mitano iliyopita. Wachambuzi wengi walitarajia Majaliwa kurejea katika nafasi yake, mosi kutokana na kauli ya rais Magufuli na pili kutokana na utendaji wake. Mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais Magufuli alizungumza wakati wa tukio la kuapishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, kwamba viongozi wa serikali hawatakiwi kuwa na hofu ya nafasi zao kwa sababu mafanikio yaliyopatikana katika miaka mitano iliyopita yalitokana na ufanisi wao pia.

Ingawa alisema kutakuwa na mabadiliko makubwa katika baraza jipya la mawaziri, ni vigumu kutenganisha mafanikio ya utawala wa Awamu ya Tano na utendaji wa Waziri Mkuu. Katika mawaziri wote wa serikali ya Rais Magufuli, Majaliwa - kama kiranja wa mawaziri wengine, ndiye pekee ambaye nafasi yake inafungamanishwa moja kwa moja na Rais katika utendaji.

Bw Majaliwa anatokea kusini mwa Tanzania eneo ambalo mtu wa mwisho kutoka ukanda huo kuwa waziri mkuu alikuwa Mzee Rashid Kawawa aliyekuwa Waziri Mkuu miaka ya mwanzoni ya uhuru. Yeye nimtu wa 11 kuwa Waziri Mkuu tangu Tanganyika ilipopata uhuru ambapo Waziri Mkuu wa kwanza alikuwa Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Majukumu ya Waziri Mkuu

Waziri Mkuu kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania atakuwa na madaraka juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa kila siku wa kazi na shughuli za Serikali, atakuwa na madaraka ya kuongoza shughuli za serikali Bungeni.

Atakuwa na madaraka ya kutekeleza au kusababisha utekelezaji wa jambo lolote au mambo yoyote ambayo rais ataagiza yatekelezwe.

Pia Waziri Mkuu atakuwa na madaraka ya kumshauri rais kuhusu uteuzi wa Mawaziri.

Anayo madaraka ya kumshauri rais kuhusu uteuzi wa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri.

Waziri Mkuu huyu ni mpenzi wa mchezo wa mpira wa miguu, na pia amesomea ualimu wa mpira. Katika kipindi cha mwaka 2010-2015 alikuwa Kocha wa timu ya soka inayoundwa na wabunge.


Alifanya kazi kubwa kuzuia uhuru wa Watanzania na kuhakikisha hana mpinzani hata kwenye jimbo lake. Vilevile ameshirikiana na usalama wa taifa kuhakikisha Tanzania inatoka kwenye demokrasia na kuingia kkwenye mfumo mpya wa kisasa wa Chama kimoja kama China. Amefanikiwa kuhakikisha wapinzani wote wenye nguvu wamefungiliwa kesi na kupigwa na polisi pale ambako wamejaribu kuhoji serikali. Mpaka sasa kuna wabunge 8 tu wa upinzani na kazi kubwa na kuongeza kura kila mahali na kuweka mipango kuhakikisha CCM inashinda kila mahali hata zile sehemu ambazo wananchi hawakuchagua CCM. Ushahidi wa kura za ubunge kutokulingana ni kuonyesha wazi mipango ya majaliwa hata sehemu nyingine kuta za raisi zimezidi kura zote zilizopigwa kwa ubunge. Kuna Mbunge wa CUF wa Temeke kapata kura sifuri yaani hata yeye hajajipigia kura! Haya ni mafanikio makubwa sana. Hongera sana Majaliwa na Hongera sana CCM
 
Moja ya wa wasioweza kumsaidia Rais kabisa! Mambo mengi ya serikali yanayoibuliwa na kufanywa na Rais yalipaswa kufanywa na huyu jamaa lakini kila mara yeye yuko nyuma.

Unachokiita ni unyenyekevu hasa ni uoga!
Hakuna kitu kizuri kama kumuelewa boss wako. Ndiyo maana amemteua tena.
 
Ha
Karibu

Spika Ndugai amesoma Katiba kuelezea namna Waziri Mkuu anavyopatikana.

Chanzo: ITV
========

Mpambe wa Rais tayari kawasili kwenye ukumbi wa bunge akisindikizwa na askari wa bunge akiwa amebeba bahasha yenye jina la waziri mkuu ajae.

Baada ya spika Ndugai kuipokea amempa kazi katibu wa bunge kuifungua na spika Ndugai anaweka sahihi kukiri kuipokea na kumrudishia mpambe wa Rais.

Rais John Magufuli kwa mujibu wa katiba amemteua mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa kuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, zoezi litakalofuata ni wabunge kumpigia kura kumthibitisha kuwa waziri mkuu wa Tanzania.

Wabunge 350 wamepiga kura, hakuna kura ya hapana pia hamna iliyoharibika hivyo wabunge wote 350 sawa na asilimia 100 wamempigia kura za ndiyo na rasmi kuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

=====


Je, Kassim Majaliwa ni nani?

Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye anaendelea na wadhifa wa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa muhula wa pili, alizaliwa tarehe 22 Desemba mwaka 1960 yaani miaka 60 iliyopita.

Kitaaluma ni Mwalimu aliyepata elimu yake ya Ualimu katika chuo cha ualimu cha Mtwara mwaka 1991-1993, na baadae kujiendeleza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Stockholm nchini Sweden.

Kutoka mwaka 1984 mpaka 2006 amehudumu katika nafasi mbalimbali kama mwalimu na kiongozi wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT). Mwaka 2006 Majaliwa aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya na kisha akajitosa kwenye siasa za ushindani mwaka 2010 alipogombea na kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ruangwa mkoani Lindi.

Baadaye aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa serikali ya awamu ya nne.

Bw Majaliwa ameidhinishwa kuwa Waziri Mkuu na Bunge baada ya jina lake kuwasilishwa bungeni na mpambe wa rais John Magufuli na kupigiwa kura ya ndiyo na wabunge wote 350 waliokuwepo ukumbini. Anatarajiwa kula kiapo hivi karibuni ili kuanza rasmi majukumu yake.

Majaliwa alikuwa Waziri Mkuu katika kipindi chote cha miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Magufuli uliokamilika mwezi uliopita. Endapo atadumu katika wadhifa huo kwa kipindi chote cha pili cha rais Magufuli atakuwa Waziri Mkuu wa pili kuhudumu kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo. Fredrick Sumaye, ndiye mtu pekee mpaka sasa aliyehudumu kwa miaka 10 mfululizo kama Waziri Mkuu wa Tanzania kutoka mwaka 1995 mpaka 2005 chini ya rais mstaafu hayati Benjamin Mkapa.

Majaliwa alikuwa Waziri Mkuu katika kipindi chote cha miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Magufuli uliokamilika mwezi uliopita.

Uteuzi wa Majaliwa hii leo haukusthua wengi kama alivyoteuliwa mara ya kwanza miaka mitano iliyopita. Wachambuzi wengi walitarajia Majaliwa kurejea katika nafasi yake, mosi kutokana na kauli ya rais Magufuli na pili kutokana na utendaji wake. Mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais Magufuli alizungumza wakati wa tukio la kuapishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, kwamba viongozi wa serikali hawatakiwi kuwa na hofu ya nafasi zao kwa sababu mafanikio yaliyopatikana katika miaka mitano iliyopita yalitokana na ufanisi wao pia.

Ingawa alisema kutakuwa na mabadiliko makubwa katika baraza jipya la mawaziri, ni vigumu kutenganisha mafanikio ya utawala wa Awamu ya Tano na utendaji wa Waziri Mkuu. Katika mawaziri wote wa serikali ya Rais Magufuli, Majaliwa - kama kiranja wa mawaziri wengine, ndiye pekee ambaye nafasi yake inafungamanishwa moja kwa moja na Rais katika utendaji.

Bw Majaliwa anatokea kusini mwa Tanzania eneo ambalo mtu wa mwisho kutoka ukanda huo kuwa waziri mkuu alikuwa Mzee Rashid Kawawa aliyekuwa Waziri Mkuu miaka ya mwanzoni ya uhuru. Yeye nimtu wa 11 kuwa Waziri Mkuu tangu Tanganyika ilipopata uhuru ambapo Waziri Mkuu wa kwanza alikuwa Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Majukumu ya Waziri Mkuu

Waziri Mkuu kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania atakuwa na madaraka juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa kila siku wa kazi na shughuli za Serikali, atakuwa na madaraka ya kuongoza shughuli za serikali Bungeni.

Atakuwa na madaraka ya kutekeleza au kusababisha utekelezaji wa jambo lolote au mambo yoyote ambayo rais ataagiza yatekelezwe.

Pia Waziri Mkuu atakuwa na madaraka ya kumshauri rais kuhusu uteuzi wa Mawaziri.

Anayo madaraka ya kumshauri rais kuhusu uteuzi wa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri.

Waziri Mkuu huyu ni mpenzi wa mchezo wa mpira wa miguu, na pia amesomea ualimu wa mpira. Katika kipindi cha mwaka 2010-2015 alikuwa Kocha wa timu ya soka inayoundwa na wabunge.
Hapo kwenye majukumu ya Waziri Mkuu, ongeza na jukumu la kusema uongo tena hadharani
 
Back
Top Bottom