Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Willium Lukuvi
akifuatilia mjadala wa Bajeti Bungeni mjini Dodoma jana
Mbunge wa Ilemela (Chadema) Highnes Kiwia ambaye aliiponda bajeti hiyo na kuipongeza bajeti iliyotolewa na wapinzani akisema ndiyo iliyopaswa kutekelezeka.
"Bajeti mbadala ilipaswa kusomwa na positive mind kwani ikisomwa na negative mind sio tu msomaji ataona giza, bali atatumbukia gizani," alisema Kiwia na kuongeza:
"Sisi tunachofanya sio kubeza mafanikio, ila tunasema mafaniko yaliyopo hayaendani na wingi wa rasilimali tulizonazo, hatusemi hakuna kilichofanyika. Nyerere alisema, ili kuwa na maendeleo tunahitaji viti vitatu; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora hakutaja fedha.
"Alisema (Nyerere) hatuwaondoi wakoloni kwa sababu tunachukia rangi zao, ni matendo yao. Sasa mkoloni wa leo ni ufisadi. hakuna namna Tanzania tukaondokana na umaskini kama hatuwezi kuondoa ufisadi."
Mbunge huyo ambaye ametishia kuikwamisha bajeti hiyo aligeukia sekta ya umeme akimtaka waziri Ngeleja kuongeza kasi ya utendaji wake ili huduma hiyo iwafikie watu wengi zaidi kuliko ilivyo sasa. "Namwambia ndugu yangu, Ngeleja, watu hawataki mahesabu ya Megawati, wanataka umeme," alisema.
Mwananchi