Bungeni - Highness Kiwia (Ilemela) atoa semina kwa Wabunge

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,896
10lukuvi.jpg

Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Willium Lukuvi
akifuatilia mjadala wa Bajeti Bungeni mjini Dodoma jana

Mbunge wa Ilemela (Chadema) Highnes Kiwia ambaye aliiponda bajeti hiyo na kuipongeza bajeti iliyotolewa na wapinzani akisema ndiyo iliyopaswa kutekelezeka.

"Bajeti mbadala ilipaswa kusomwa na positive mind kwani ikisomwa na negative mind sio tu msomaji ataona giza, bali atatumbukia gizani," alisema Kiwia na kuongeza:

"Sisi tunachofanya sio kubeza mafanikio, ila tunasema mafaniko yaliyopo hayaendani na wingi wa rasilimali tulizonazo, hatusemi hakuna kilichofanyika. Nyerere alisema, ili kuwa na maendeleo tunahitaji viti vitatu; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora hakutaja fedha.

"Alisema (Nyerere) hatuwaondoi wakoloni kwa sababu tunachukia rangi zao, ni matendo yao. Sasa mkoloni wa leo ni ufisadi. hakuna namna Tanzania tukaondokana na umaskini kama hatuwezi kuondoa ufisadi."

Mbunge huyo ambaye ametishia kuikwamisha bajeti hiyo aligeukia sekta ya umeme akimtaka waziri Ngeleja kuongeza kasi ya utendaji wake ili huduma hiyo iwafikie watu wengi zaidi kuliko ilivyo sasa. "Namwambia ndugu yangu, Ngeleja, watu hawataki mahesabu ya Megawati, wanataka umeme," alisema.


Mwananchi
 
Rais Kikwete huko Malasya amesema afrika nchi nyingi afrika ni maskini sababu ya kukosa pesa za misaada ili kuendeshea miradi ya maendeleo. Anapingana na itikadi za hayati Nyerere kwamba ili tuendelee tunahitaji watu ardhi, siasa safi na uongozi bora kama alivyowakumbusha wabunge mheshimiwa Mbunge wa Ilemela. Ina maana Rais wetu anachojua maendeleo huletwa na pesa? Walioanza kuendelea walipata wapi pesa? Watu, ardhi, siasa safi na uongozo bora ndio msingi wa maendeleo, eti tunahitaji pesa ili tuendelee na pesa zinaishia mifukoni mwa viongozi wa serikali maana yake kukosa uongozi bora.
 
kobe akinyamaza anatunga sheria, huyu jamaa amekuwa kimya mda mpaka nikasahau jina lake tofauti na mwenzake wenje. safi sna timu ya CDM
 
Mkuu hawa jamaa wa CDM ni Noma woote leo nimemshuhudia na Mh. Machemli ni hatari kwa wazembe na ni wajasiri full data and focused
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Hiyo ndiyo inavyotakiwa,wabunge wengi waipongeza bajeti wakati kwenye majimbo yao kuna matatizo yanayowakabiri
 
Rais Kikwete huko Malasya amesema afrika nchi nyingi afrika ni maskini sababu ya kukosa pesa za misaada ili kuendeshea miradi ya maendeleo. Anapingana na itikadi za hayati Nyerere kwamba ili tuendelee tunahitaji watu ardhi, siasa safi na uongozi bora kama alivyowakumbusha wabunge mheshimiwa Mbunge wa Ilemela. Ina maana Rais wetu anachojua maendeleo huletwa na pesa? Walioanza kuendelea walipata wapi pesa? Watu, ardhi, siasa safi na uongozo bora ndio msingi wa maendeleo, eti tunahitaji pesa ili tuendelee na pesa zinaishia mifukoni mwa viongozi wa serikali maana yake kukosa uongozi bora.
Hizo pesa za misaada hata wakimmwagia kama mvua kama uongozi wake hautabadilisha mienendo yao hakutakuwa na maendeleo yeyote. Pesa si msingi wa Maendeleo!
 
10lukuvi.jpg

Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Willium Lukuvi
akifuatilia mjadala wa Bajeti Bungeni mjini Dodoma jana

Mbunge wa Ilemela (Chadema) Highnes Kiwia ambaye aliiponda bajeti hiyo na kuipongeza bajeti iliyotolewa na wapinzani akisema ndiyo iliyopaswa kutekelezeka.

"Bajeti mbadala ilipaswa kusomwa na positive mind kwani ikisomwa na negative mind sio tu msomaji ataona giza, bali atatumbukia gizani," alisema Kiwia na kuongeza:

"Sisi tunachofanya sio kubeza mafanikio, ila tunasema mafaniko yaliyopo hayaendani na wingi wa rasilimali tulizonazo, hatusemi hakuna kilichofanyika. Nyerere alisema, ili kuwa na maendeleo tunahitaji viti vitatu; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora hakutaja fedha.

"Alisema (Nyerere) hatuwaondoi wakoloni kwa sababu tunachukia rangi zao, ni matendo yao. Sasa mkoloni wa leo ni ufisadi. hakuna namna Tanzania tukaondokana na umaskini kama hatuwezi kuondoa ufisadi."

Mbunge huyo ambaye ametishia kuikwamisha bajeti hiyo aligeukia sekta ya umeme akimtaka waziri Ngeleja kuongeza kasi ya utendaji wake ili huduma hiyo iwafikie watu wengi zaidi kuliko ilivyo sasa. "Namwambia ndugu yangu, Ngeleja, watu hawataki mahesabu ya Megawati, wanataka umeme," alisema.


Mwananchi

Kwa hili la Tanesco sikubaliani na kiwia kuwa hawana walilofanya. Tanesco ya miaka iliyopita siyo hii ya leo nafikiri bado baadhi ya watu wamebaki na historia, Tanesco ya sasa inafanya kazi zake kwa mpangilio unaoeleweka, sikutarajia hata siku moja kuwa nitakuja kuwasha umeme wa Tanesco ila nataka nikuhakikishie kuwa nilipofanya mchakato wa ufuatiliaji nilishangaa jinsi Tanesco walivyokuwa wanafanya shughuli zao kwa uhakika kiasi cha mtu kama mimi kupata huduma hiyo bila kutoa chochote ndani ya week tatu toka nilipe kiasi cha pesa kilichohitajika, awali nilikuwa natumia jenereta, kwa siku tatu petrol ya sh.10,000/= sasa hivi hiyo elfu kumi napata uniti kama sikosei zaidi ya hamsini ambapo nazitumia kwa zaidi ya week tatu au mwezi kabisa, sasa jamani ni kweli hawajafikia hicho kiwango kinachotakiwa ila kwa sasa wanajitahidi tuwatie moyo matatizo mengine yako nje kabisa ya uwezo wa Tanesco.
 
kobe akinyamaza anatunga sheria, huyu jamaa amekuwa kimya mda mpaka nikasahau jina lake tofauti na mwenzake wenje. safi sna timu ya CDM

Nakubaliana na kinachojilia kauli za wabunge wa Chadema kwamba watu makini wenye mtazamo makini kwa ajili ya kujenga taifa makini. Hoja na kauli zao zinapenya na kunyong'onyeza, ukweli, hali halisi ya maisha na kueleweka hata kwa mtu ye yote. Si hoja ya kisiasa ila ukweli wa hali halisi ya maisha yalivyo. Imefika sasa kila mtu anasema CCM tuiweke kando, wamechoka na tumewachoka, wakae kando wapumzike waone jinsi na wengine wanavyofanya ili wapate kuwanyooshea vidole. Huu ndio mchezo wa siasa wenye kuleta tija kwa taifa.
 
Yani! yani! yani! CDM MP'S wapo tooooo smart! yani! yani! unaenjoy bunge fleve those jamaa wanapokuwa wakipafomu!
 
Yani! yani! yani! CDM MP'S wapo tooooo smart! yani! yani! unaenjoy bunge fleve those jamaa wanapokuwa wakipafomu!

Well said wanapafomu wakimaliza miaka yao mitano wanalipwa viinua mgongo vya maana wanakuja kuwapiga porojo wanarudi tena basi their lives goes on na nyie mnabaki na burudani za maneno. Moral of my comment: "action speak louder than words"
 
Kwa hili la Tanesco sikubaliani na kiwia kuwa hawana walilofanya. Tanesco ya miaka iliyopita siyo hii ya leo nafikiri bado baadhi ya watu wamebaki na historia, Tanesco ya sasa inafanya kazi zake kwa mpangilio unaoeleweka, sikutarajia hata siku moja kuwa nitakuja kuwasha umeme wa Tanesco ila nataka nikuhakikishie kuwa nilipofanya mchakato wa ufuatiliaji nilishangaa jinsi Tanesco walivyokuwa wanafanya shughuli zao kwa uhakika kiasi cha mtu kama mimi kupata huduma hiyo bila kutoa chochote ndani ya week tatu toka nilipe kiasi cha pesa kilichohitajika, awali nilikuwa natumia jenereta, kwa siku tatu petrol ya sh.10,000/= sasa hivi hiyo elfu kumi napata uniti kama sikosei zaidi ya hamsini ambapo nazitumia kwa zaidi ya week tatu au mwezi kabisa, sasa jamani ni kweli hawajafikia hicho kiwango kinachotakiwa ila kwa sasa wanajitahidi tuwatie moyo matatizo mengine yako nje kabisa ya uwezo wa Tanesco.

Anold we una bahati na labda unafahamika. Niliomba kuletewa umeme nikajaza form na ikachukua wiki bila hatua zo zote kuchukuliwa na wakati likizo yangu inakaribia nirudi ninakobangaisha maisha. Fundi akaniambie suala nimwachie yeye anajua namna ya kuwapata, na amini usiamini form nilizojaza hazikutumika na fundi siku hiyo hiyo alirudi na mtaalamu mkadiriaji na kesho yake umeme uliwaka. Mambo bado sana tusitetee hilo. Kuna tofauti na wanaangalia nani na kama sura isiyofahamika au jina geni basi ujue utakutana li red light na bahati yako ulipata green light.
 
Huyu bwana nakumbuka nilikaa naye hapo nyuma kabla ya kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu uliopita pale Arusha aikiwa na muheshimiwa mwenzake ambaye sasa hivi ni mbunge wa Arusha mjini muheshimiwa GodBless Lema kwakweli alinipa hamasa kubwa sana wakati akiniambia anajikita katika kugombe jimbo la Ilemela Mwanza, amekomaa sana na anauchungu sana wa kuliletea jimbo lake maendeleo. Keep it Up Highness Kiwia kwa kutuonyesha vijana kua nasi tunaweza.

Highness-Kiwia-240x300.jpg
 
Well said wanapafomu wakimaliza miaka yao mitano wanalipwa viinua mgongo vya maana wanakuja kuwapiga porojo wanarudi tena basi their lives goes on na nyie mnabaki na burudani za maneno. Moral of my comment: "action speak louder than words"

I agree with u, but not all MPs. Wanachopigania kufa na kupona Chadema kinaeleweka na kila mmoja hata mwanakijiji anaelewe, ya yale yanayopiganiwa na MPs wa CCM kinaeleweka ulaji tofauti na uwajibikaji. So sera ziko wazi pande zote mbili na hata kushinda kwa wingi wa kura dhidi ya haki inayodaiwa ni ishara tosha ya kuiongezea nguvu bendera ya Chadema kupepea. Chama cha magamba wangekuwa na miwani ya kuona mbali wangeshukuru kutekeleza sera ya Chadema kiwani atakayefahamika mtekelezaji serikali yao lakini wamevaa miwani kizai hawaoni mbali na zaidi ya kuona kiza mbele yao na hivo CCM nam iwani yao ya kiza kufifisha rays za energy ya Chadema hali inayowageukia kukzidi kuwapotezea mwelekeo wa gari wanaloendesha kutumbukia mtaroni.
 
Well said wanapafomu wakimaliza miaka yao mitano wanalipwa viinua mgongo vya maana wanakuja kuwapiga porojo wanarudi tena basi their lives goes on na nyie mnabaki na burudani za maneno. Moral of my comment: "action speak louder than words"

Actions gani unataka Shossi? Wakiitisha maandamano wanaambiwa wanachochea fujo na kuhatarisha amani, wanatupwa lumande na kubambikwa kesi...wakisema fungeni milango bungeni tuchapane makofi ili watu wawe serious wanaambiwa 'wahuni'...wakisema bungeni sio sehemu ya kuuza sura wanaombewa miongozo ya spika eti wanatumia lugha za 'mtaani'...wakirudisha mpambano bungeni wanaambiwa longo longo 'actions speak louder! Wafanyaje sasa?
 
Hizo pesa za misaada hata wakimmwagia kama mvua kama uongozi wake hautabadilisha mienendo yao hakutakuwa na maendeleo yeyote. Pesa si msingi wa Maendeleo!
nikweli kabisa, kwani wamepewa mingapi na hatuoni chochote
 
Back
Top Bottom