Dodoma: Mussa Assad(CAG), ahojiwa na Kamati ya Haki, Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge, ripoti kukabidhiwa kwa Spika..

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
V25A7978.JPG

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof Mussa Asad amewasili bungeni, Dodoma kuitikia wito wa kufika katika kamati ya maadili

CAG tayari kwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kuhusu madai ya kudhalilisha Bunge, inadaiwa alisema bunge ni dhaifu.

UPDATES:1115HRS

IMG_20190121_114204.jpg

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad akiwa tayari amefika mbele ya Kamati ya Haki, Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge Muda huu mjini Dodoma kuhojiwa kufuatia kauli za kudhalilisha Bunge akiwa ziarani nchini Marekani.

UPDATES: 1500HRS
IMG_20190121_155620.jpg

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Emmanuel Mwakasaka, amesema kamati yake imemaliza kumhoji Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad na ametoa ushirikiano mkubwa. Hata hivyo, amesema kamati bado inaendelea na uchambuzi na wakikamilisha watalipeleka suala hilo kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Dodoma. Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge leo Jumatatu Januari 21, 2019 saa 8 mchana imemaliza kumhoji Mdhibiri na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kuhusu kauli yake ya “udhaifu wa Bunge.”

Wakati CAG akiondoka saa 8:47 atika viwanja vya bunge, maofisa mbalimbali waliwazuia waandishi wa habari kumhoji chochote.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Emmanuel Mwakasaka amesema atawaeleza waandishi wa habari kilichojiri katika kikao hicho.

CAG Assad aliyeteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, Desemba Mosi mwaka 2014 ameitwa mbele ya kamati hiyo kujieleza kuhusu kauli aliyoitoa wakati alipokuwa akihojiwa na kituo cha televisheni cha idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa (UN) akiwa New York, Marekani alikokuwa akihudhuria mkutano.

Alitumia neno “udhaifu” wa Bunge alipokuwa akieleza sababu za kutofanyiwa kazi kwa ripoti zake ambazo zimekuwa zikibainisha ufisadi.
Prof. Assad(CAG): Nitaitikia wito wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge - JamiiForums
 
Dah..
Naona jamaa katumia hekima sana kwenda.

Cha ajabu eti taarifa zinasema sio Spika aliyemuita, ila ni kamati ya maadili iliyomuagiza Spika amuite kuhojiwa.
Kinachofuata hapo jamaa ni kuibuka mshindi tu, halafu soon Jiwe anaitisha shughuli ya kitaifa anamualika Assad na kumsifia mambo yanakwisha.

Ndugai ajiangalie sana.
Jiwe si mwanasiasa.
Atamharibia sana political carrier yake, na baadaye Ndugai ataonekana kama Spika aliyevurunda Tanzania.
 
Dah..
Naona jamaa katumia hekima sana kwenda.

Cha ajabu eti taarifa zinasema sio Spika aliyemuita, ila ni kamati ya maadili iliyomuagiza Spika amuite kuhojiwa.
Kinachofuata hapo jamaa ni kuibuka mshindi tu, halafu soon Jiwe anaitisha shughuli ya kitaifa anamualika Assad na kumsifia mambo yanakwisha.

Ndugai ajiangalie sana.
Jiwe si mwanasiasa.
Atamharibia sana political carrier yake, na baadaye Ndugai ataonekana kama Spika aliyevurunda Tanzania.
NDUGAI NI SPIKA DHAIFU SANA ALIYEWAHI KUTOKEA TANZANIA ZAIDI YA MAMA MAKINDA
 
hao kamati watajikuta wanaomba kupiga picha na CAG baada ya kumaliza mahojiano

lengo ikiwa kupata kujitapa mbeleni kuwa sehemu muhimu kwa kuiondoa dhuruma kwa watanzani.
 
Back
Top Bottom