Bunge Uganda lazuia uanzishwaji wa wilaya mpya kuepuka gharama

omujubi

JF-Expert Member
Dec 6, 2011
4,325
2,498
Wanajf, nimekutana na hii habari na naona kwa kiasi kikubwa sana inafanana na kilichotokea hapa kwetu. Kwa wale wananofuatilia mustakabali wanchi tunaweza kuangalia hii hali. Msijali hii tafsiri isiyo rasmi.

Wabunge jana walizuia uundwaji wa wilaya mpya 25 zilizopendekezwa mpaka serikali ionyeshe uhalali wake na ni jinsi gani inajipanga kupata pesa za kuziendesha. Wabunge walio katika kamati za Utumishi wa umma na Serikali za mitaa jana walikutana na waziri wa Serikali za mitaa Adolf Mwesige na kuzuia uundwaji wa maeneo mapya ya utawala bila ya kuainisha ni jinsi gani serikali imejipanga kuziendesha (kipesa).

Wawakilishi hao wa wananchi pia wameitaka Serikali kutoa taarifa juu ya ni jinsi gani inaendeleza wilaya zilizopo. "Tunataka kujua ulingano na uhalali wa kuunda wilaya zaidi wakati hatujui ni jinsi gani pesa za kuziendesha zitapatikana" Mbunge wa IgaraMagharibi Raphael Magyezi (NRM) amesema. "Tunataka mchanganuo kamili wa mgawanyo ya fedha na uthibitisho kuwa hatutengenezi matatizo makubwa kwa nchi hii."


Wabunge wanaitaka serikali kwanza kuonyesha uhalali wa gharama za maeneo hayo mapya ya utawala na kama yanapelekea hasa kwenye ubora wa upelekaji huduma kwa jamii.

My take:
1. Hivi wakati hizi wilaya na mikoa mipya inaanzishwa hapa Tanzania ni nani walishauriana na kukubaliana kufanya
waliyoyafanya? Na bunge letu lina nafasi gani katika hili suala?

2. Je, kwa gharama za kuendesha hizi wilaya na mikoa wakati hospitali za mikoa hazina hata x-ray (sijataja shule na
mengineyo) ni sawa?
3. Je, kama kuna makosa ya kimaamuzi tumeyafanya, hatuwezi tukarudi nyuma kidogo badala ya kuendelea nayo? (maana
wahenga husema "tujifunze kutokana na makosa")

Nawasilisha


Source: http://www.monitor.co.ug/News/Natio...+costs/-/688334/1462620/-/xs3ojj/-/index.html
 
omujubi;4307739 3. Je said:

Makosa ya kimaamuzi tuliyoyafanya ni kuichagua CCM 2010.

Kama kweli tumejifunza kutokana na makosa, basi 2015 ni kui VOTE OUT CCM
 
Makosa ya kimaamuzi tuliyoyafanya ni kuichagua CCM 2010.

Kama kweli tumejifunza kutokana na makosa, basi 2015 ni kui VOTE OUT CCM

Kweli kabisa mkuu hatuna budi kuepuka kufanya kosa hilo tena.
 
Kweli kabisa mkuu hatuna budi kuepuka kufanya kosa hilo tena.
nimesikia watu wengi wakilalamikia wabunge wetu pamoja na bunge lenyewe kuwa walikuwa wapi sheria ya mafao na pensheni ilipopitishwa lakini baadae tumeona hapa kuwa kuna kumbukumbu zinaonyesha kuwa ilipita huko!

Sasa najiuliza haya maamuzi ya kugawa mikoa ni rais ndiye anaamua iweje bila kujadiliwa bungeni?
Na tukichunguza maamuzi mengi yaliyofanyika (ukiondolea lile ambalo cdm waliamua 'kuingia' Magogoni kumuona JK na akakubali kurekebisha) yanaweza kuwa na utata mkubwa kwa mustakabali wa nchi hii.

Na inaelekea huko Uganda wabunge waliopinga ni wa NRM ambacho ndio chama tawala tofauti kabisa na hapa kwetu


 
Hilo ndio bunge la watu, japo sijui katika mambo mengine linawatetea vipi watu wao, lakini kwa hili nawapongeza.

Kwa kwetu huku, uamuzi wa kuanzisha wilaya na mikoa ulikuwa mbaya pia wakibinafsi mno, kwa mfano, unaanzishaje mkoa una wilaya mbili tu (mkoa wa katavi). Na hii yote ni matatizo ya kukosa watu/viongozi ambao wanatumia bongo zao kabla ya kuingiza nchi kwenye matumizi ya fedha ambazo zingepelekwa mahali kwingine kwenye kuleta manufaa zaidi.

Kwa mfano mimi nilifikiria kwamba kwa vile zaidi ya asilimia hamsini ya mapato ya nchi yanatoka Dar ingekuwa ni uamuzi wa busara zaidi kama tungeamua kutumia hela ambazo tunatarajia kuzitumia kwenye wilaya na mikoa mipya kwa kuongezea dar miundo mbinu, kama vile kuanzisha miji mipya nje ya CBD, eg Bunju, kimara, pugu, mbagala, etc, ili dar iwe na easy trafik movements ambayo kwa sasa imekuwa ni tatizo mkubwa kwa dar kama sio taifa kwa ujumla. Safari ya kutoka, mfano, bandarini mpaka tegeta, inaweza kuwa sawa na muda wa safari ya kutoka Dar kwenda Chalinze kama sio Moro.


Kwa maana hiyo muda mwingi kwenye sehemu ambayo ni chanzo kikuu cha uchumi wa nchi unaishia barabarani.

Au vinginevyo tungetumia fedha hizo kuimarisha hata bandari za Tanga na Mtwara, kwa kutumia mapato yatokanayo na hizo bandari tungeweza kufanya hayo tunayoyafanya sasa hivi ya kuanzisha wilaya na mikoa kwa awamu sio kwa mkupuo kiasi hicho.


Mpaka sasa wilaya zilizoanzishwa kabla za hizi za juzi hazina miundo mbinu ya kutosha including rasilimali watu za kutosha, kwa mfano, wilaya ya kishapu, kwa kukosa rasilimali watu, fedha zaidi ya 5bil. zilizotumwa huko na serikali kuu zimeishia mikononi mwa wajanja.
 
Hilo ndio bunge la watu, japo sijui katika mambo mengine linawatetea vipi watu wao, lakini kwa hili nawapongeza.

Kwa kwetu huku, uamuzi wa kuanzisha wilaya na mikoa ulikuwa mbaya pia wakibinafsi mno, kwa mfano, unaanzishaje mkoa una wilaya mbili tu (mkoa wa katavi). Na hii yote ni matatizo ya kukosa watu/viongozi ambao wanatumia bongo zao kabla ya kuingiza nchi kwenye matumizi ya fedha ambazo zingepelekwa mahali kwingine kwenye kuleta manufaa zaidi.

Kwa mfano mimi nilifikiria kwamba kwa vile zaidi ya asilimia hamsini ya mapato ya nchi yanatoka Dar ingekuwa ni uamuzi wa busara zaidi kama tungeamua kutumia hela ambazo tunatarajia kuzitumia kwenye wilaya na mikoa mipya kwa kuongezea dar miundo mbinu, kama vile kuanzisha miji mipya nje ya CBD, eg Bunju, kimara, pugu, mbagala, etc, ili dar iwe na easy trafik movements ambayo kwa sasa imekuwa ni tatizo mkubwa kwa dar kama sio taifa kwa ujumla. Safari ya kutoka, mfano, bandarini mpaka tegeta, inaweza kuwa sawa na muda wa safari ya kutoka Dar kwenda Chalinze kama sio Moro.


Kwa maana hiyo muda mwingi kwenye sehemu ambayo ni chanzo kikuu cha uchumi wa nchi unaishia barabarani.

Au vinginevyo tungetumia fedha hizo kuimarisha hata bandari za Tanga na Mtwara, kwa kutumia mapato yatokanayo na hizo bandari tungeweza kufanya hayo tunayoyafanya sasa hivi ya kuanzisha wilaya na mikoa kwa awamu sio kwa mkupuo kiasi hicho.


Mpaka sasa wilaya zilizoanzishwa kabla za hizi za juzi hazina miundo mbinu ya kutosha including rasilimali watu za kutosha, kwa mfano, wilaya ya kishapu, kwa kukosa rasilimali watu, fedha zaidi ya 5bil. zilizotumwa huko na serikali kuu zimeishia mikononi mwa wajanja.
kinachonitisha zaidi ni jinsi Watanzania tulivyojielekeza kwenye kushibikia maendeleo ya vitu badala ya watu. Wote tuko moved na quantities and not qualities!
Matokeo yeke unaweza kukuta kiongozi wa ngazi ya juu au hata mbunge akitamka bila aibu kuwa "sisi tumeendelea kwa vile tuna wilaya/mikoa mingi zaidi ya Uganda/Kenya"!!

 
huku nchini kwa wendawazimu kila siku wanaanzisha mikoa na wilaya mpya ukiuliza tatizo na shemeji apate nafasi.
 
Back
Top Bottom