Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Haijapata kutokea tangu Tanzania ijitawale kuwa na Spika mbabe, jeuri na mkorofi kama Supukali Job Ndugai. Kitendo cha kumkataa CAG Assad ni dharau, matusi na kejeli kwa mamlaka za Uteuzi wa CAG ambaye ni Rais wa JMT Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Spika Job na Nduagi na Bunge lote wameonesha dharau ya hali ya juu kwa Mhe. Rais kwa kumkataa Prof. Assad kisa ati alisema Bunge ni dhaifu. Ukitazama hili sakata lililoanzishwa na Spika Nduagi kwa jicho la tatu unaweza kubaini kwamba hapa kuna agenda imejificha.
Agenda hiyo yawezekana ikawa ni kutokana na CAG kuibua madudu ya matumizi ya hovyo ya Fedha za Watanzania kama vile matibanu ya Spika Ndugai lakini pia taarifa ya upotevu wa Fedha au kukosa maelezo ya kina jinsi Tshs. 1,5T zilivyo yeyuka na Serikali kushindwa kutoa ufafanuzi wa kina.
Kama Rais hataingilia kati kuhusu sakata hili ili kunusuru Heshima ya Bunge la Tanzania basi tunaweza kusema anachofanya Spika Job Ndugai ni maelekezo toka Juu. Ni wakti wa Prof. Assad kufungasha virago na kutafuta maisha mengine. Hii itakuwa ni udhihirisho mwingine wa Tanzania kupoteza Utawala wa Sheria.
Inasikitisha.
Spika Job na Nduagi na Bunge lote wameonesha dharau ya hali ya juu kwa Mhe. Rais kwa kumkataa Prof. Assad kisa ati alisema Bunge ni dhaifu. Ukitazama hili sakata lililoanzishwa na Spika Nduagi kwa jicho la tatu unaweza kubaini kwamba hapa kuna agenda imejificha.
Agenda hiyo yawezekana ikawa ni kutokana na CAG kuibua madudu ya matumizi ya hovyo ya Fedha za Watanzania kama vile matibanu ya Spika Ndugai lakini pia taarifa ya upotevu wa Fedha au kukosa maelezo ya kina jinsi Tshs. 1,5T zilivyo yeyuka na Serikali kushindwa kutoa ufafanuzi wa kina.
Kama Rais hataingilia kati kuhusu sakata hili ili kunusuru Heshima ya Bunge la Tanzania basi tunaweza kusema anachofanya Spika Job Ndugai ni maelekezo toka Juu. Ni wakti wa Prof. Assad kufungasha virago na kutafuta maisha mengine. Hii itakuwa ni udhihirisho mwingine wa Tanzania kupoteza Utawala wa Sheria.
Inasikitisha.