Bunge lisitumike kuzima mapambano dhidi ya Madawa ya kulevya kama lilivyozima Operesheni Tokomeza

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwanza napenda kuwapa pole wale wote walioumizwa kwa namna moja ama nyingine kukamatwa kwa baadhi ya wapenzi wetu kutokana na kuhusika kwao na biashara ya Madawa ya kulevya. Kati ya wote wanaotetewa sana nje na ndani ya mitandao ya kijamii, ni kipenzi 'chetu' Wema Isac Sepetu ambaye kwa sura ya kijamii ni mtu mwema, mpole, mcheshi na Mtanashati. Ila waliomkamata wanajua zaidi ya tujuavyo. Tuwe na subira ili vyombo vifanye kazi yake. Wao wanajua zaidi ya tujuavyo. Hata magaidi wanakuwa karibu sana na jamii husika ili wapate hifadhi na watetezi. Ndivyo ilivyo kwa Madawa ya Kulevya.

Pili niwapongeze na kuwatia moyo wale wote walio kwenye mapambano dhidi ya Madawa ya Kulevya. Niwaambie kwamba hii vita si ya kitoto. Si lele mama na si ya kispoti spoti. Tangu siku ya Kwanza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda alipotangaza vita hii, hakika niliona hatari iliyo mbele yake. Nilijua kuwa hii vita itageuzwa kuwa ya Makonda pekee badala ya Watanzania wote kushiriki. Nilijua atasusiwa na atakatishwa tamaa.

Nimpongeze sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuivua vita hiyo kutoka mikononi mwa RC Makonda hadi vyombo vya Dola. Hapa sasa utamu ulipo. Wale wote mnaomshambulia Makonda mnapoteza muda bure. Vita imeshahama kwake na sasa ipo kwa vyombo vya Dola. Nitavishangaa sana vyombo hivyo kama vitarudi nyuma na kuasi Amri ya Amiri Jeshi Mkuu. Nitawashangaa na kuwashangaa.

Miaka kadhaa iliyopita, tulikuwa na Operesheni Tokomeza. Hakika dhamira ilikuwa njema na mapambano yalianza vema. Ila baada ya kuingia bungeni tu, kila kitu kikaharibika. Baada ya muda ikagundulika kuwa kumbe miongoni mwa wabunge walikuwa na maslahi binafsi na Pembe za Ndovu. Operesheni ikafa na ikatokomea kusikojulikana.

Baada ya kuanza kwa vita ya Madawa ya Kulevya, kelele zilianza kupigwa mitandaoni. Ilianza kama mapambano baina ya Team Wema Sepetu dhidi ya Team za Wanaume aliowahi kuwa nao na mahusiano kimapenzi. Team Mondi, Idris Sultan and the like. Hata hivyo, kadri siku zilivyoenda, baadhi ya watu ambao ama aliwahi kuwa nao kimapenzi ama yupo nao wakaanza kutumia madaraka na mamlaka yao kumtetea Wema Sepetu. Imenisikitisha na imenihuzunisha.

Mbaya zaidi ni pale mjadala huu ulipoingia Bungeni. Mashambulizi yameanza dhidi ya Makonda kana kwamba ni yeye pekee ndiye mwenye kiherehere cha kupambana na madawa ya kulevya. Wabunge wanatumia Style ile ile ya Wema Sepetu. Jana Wema amenukuliwa akisema kuwa Makonda hajamkamata Agnes Masogange kwa vile ana mahusiano naye kimapenzi na amempangisha nyumba Makongo. Msukuma na Halima Mdee nao wakaja na swaga zile zile. Kwamba Makonda hajawakamata baadhi ya watu ambao wamemsafirisha kwenda Marekani na Ufaransa. Inachekesha sana. Kinachonisikitisha zaidi ni pale hawa wabunge wanapokosa ujasiri kama wa Amina Chifupa wa kuwataja madealers wa Madawa ya Kulevya. Wanasema tu kuwa wanafahamika lakini hakuna mwenye uthubutu wa kuwataja. Pia wanajenga dhana kuwa akina Wema Sepetu wanaonewa. Ridiculous.

Niwaase sana Wabunge wetu. Kama hamna dhamira njema ya kupambana na Madawa ya Kulevya, ni bora mkakaa pembeni. Waacheni wenye dhamira hiyo wapambane. Kamwe msiligeuze Bunge letu kuwa fimbo ya kuwachapa wale wote wanaoratibu na kusimamia mapambano hayo.

Ninajua uchungu ambao wabunge kama Msukuma na Waziri Nape walionao hasa wakihesabu idadi ya siku ambazo Wema Sepetu amekaa Selo. Ninafahamu jitihada ambazo wamezifanya nje ya Bunge kwa kuwapigia Simu watu wanaoratibu na kuongoza Operesheni hii ili kipenzi chal aachiwe. Ninajua inawauma sana. Ila mkumbuke kuwa mapambano haya hayachagui na hayabagui. Tukiacha baadhi ya watu eti kwa sababu tu wanatuhusu hakika tutakosea sana na tutakwamisha haya mapambano. Tuanze kwanza kusafisha nyumba zetu kabla ya kuhimiza usafi kwa nyumba ya jirani.

Mapambano Dhidi ya Madawa ya Kulevya Hayahepukiki
 
Kwa sasa tumechoka na porojo za madawa ya kulevya! JK alisema hadharani anayo majina ya vigogo wa dawa za kulevya, ni bora wahusika wote wangeanza na orodha yake!!!
 
Kama Mungu angekuwa anabandika sura za wanaume wote tuliotembea nao, naamini kuwa Wema Sepetu asingekuwa na hata kidoti kwenye mwili wake kisicho na picha ya mwanaume. Bora niliamua kuolewa mapema ijapokuwa ndoa ina mitihani yake kuliko haya maisha ya Wema Sepetu
 
Kwa sasa tumechoka na porojo za madawa ya kulevya! JK alisema hadharani anayo majina ya vigogo wa dawa za kulevya, ni bora wahusika wote wangeanza na orodha yake!!!
Kila zama na namna yake ya kudeal na mambo. Naamini Serikali ya awamu hii ni fumua fumua
 
Hivi unaelewa watu walivyoumia kwenye operation tokomeza?....

Unalinganisha kukamata mateja na kuwapeleka central.........

Na operation iliyoongozwa na JWTZ?....

Acha mzaha wewe kwanza watu walibakwa na kudharirishwa sana aisee tumwachie Mungu tu hayo yamepita.......
 
Kitendo cha hao wabunge kukomaa na issue ya masogange kimenisikitisha sana that nonsense, habari yenyewe haina ukweli hata kidogo hakuna cha kupangiwa wala kupangishiwa tunaoujua ukweli tunawacheka sana na uzushi huo hautozuia kamwe mapambano haya ndio kwanza kazi imeanza.

SayNoToNgada

Go Makonda go go go...
 
Kitendo cha hao wabunge kukomaa na issue ya masogange kimenisikitisha sana that nonsense, habari yenyewe haina ukweli hata kidogo hakuna cha kupangiwa wala kupangishiwa tunaoujua ukweli tunawacheka sana na uzushi huo hautozuia kamwe mapambano haya ndio kwanza kazi imeanza.

SayNoToNgada

Go Makonda go go go...
Wema Sepetu amekutwa na Bangi, Msukuma anayepiga kelele ni mdau wa Bangi what do you Expect? Bamba to Bamba.
 
Back
Top Bottom