Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,794
- 71,214
Wakuu jamvini, Nimekuwa nafuatilia mijadala ya Bunge letu la Budget kwa muda sasa ila sasa nimechoka kabisa.
Kilicho nichosha ni hii tabia ya baadhi ya wabunge wengi (hasa wa CCM) kutumia muda wao wote kujadili mstari kwa mstari wa maoni ya Upinzani katika kila Budget iletwayo na Wizara.
Nijuavyo mimi maoni ya kambi ya upinzani sio lazima yafuatwe na serikali iliyoko madarakani hivyo kama yana makosa serikali inayaweka pembeni na bado inakuwa haijavunja sheria yeyote.
Sasa najiuliza kwa nini wabunge wa CCM na baadhi wa CUF wanatunisha Misuli na kutumia nguvu nyingi ku crash maoni ya Chadema na watoa maoni hayo wakati siyo yatakayo endesha serikali 2012/2013?
Wanapoteza muda wao kisha wanaishia na kusema "Mhe Spika naona waziri asilisahau jimbo langu linakabiliwa na umasikini"
Najiuliza tena Hili Linaashiria nini?
Kilicho nichosha ni hii tabia ya baadhi ya wabunge wengi (hasa wa CCM) kutumia muda wao wote kujadili mstari kwa mstari wa maoni ya Upinzani katika kila Budget iletwayo na Wizara.
Nijuavyo mimi maoni ya kambi ya upinzani sio lazima yafuatwe na serikali iliyoko madarakani hivyo kama yana makosa serikali inayaweka pembeni na bado inakuwa haijavunja sheria yeyote.
Sasa najiuliza kwa nini wabunge wa CCM na baadhi wa CUF wanatunisha Misuli na kutumia nguvu nyingi ku crash maoni ya Chadema na watoa maoni hayo wakati siyo yatakayo endesha serikali 2012/2013?
Wanapoteza muda wao kisha wanaishia na kusema "Mhe Spika naona waziri asilisahau jimbo langu linakabiliwa na umasikini"
Najiuliza tena Hili Linaashiria nini?