Bunge linalotegemewa kupitisha Sheria za Nchi lasema limebaini dosari kwenye upitishaji wa sheria ya kumiliki laini zaidi ya 1

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
BUNGE limebaini dosari katika utungaji wa sheria ndogo nchini, ikiwamo sheria inayoweka zuio kwa Mwananchi kuwa na laini ya simu zaidi ya moja

bungee.jpg

Akiwasilisha bungeni jijini hapa jana, taarifa ya Kamati ya Sheria Ndogo kuhusu uchambuzi wa sheria ndogo zilizowasilishwa katika mikutano ya 18 na 19 ya Bunge, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, William Ngeleja, alisema miongoni mwa dosari hizo ni sheria ndogo kwenda kinyume cha sheria mama na sheria nyingine za nchi.

Alizitaja baadhi ya sheria hizo kuwa ni pamoja na The Water Supply, Regulations 2019 ambayo inakwenda kinyume cha Sheria ya The Water Supply and Sanitation, 2019 na Sheria Ndogo (Ada na Ushuru) za Halmashauri za Mkinga 2019 inayokwenda kinyume cha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura 290.

Ngeleja alisema dosari ya pili ni sheria ndogo kutozingatia misingi ya uandishi wa sheria, akiwakumbusha waandishi wa sheria kuzingatia kifungu cha 25(2) cha Sheria ya Tafsiri ya Sheria kinachowataka kuzingatia majedwali kuwa sehemu ya sheria.

Mbunge huyo wa Sengerema (CCM) aliitaja dosari ya tatu kuwa ni sheria ndogo kuwa na makosa katika majedwali kwa kurejea kanuni ambazo si sahihi au kurejea kanuni ambazo hazipo.

Alisema dosari ya nne ni sheria ndogo kutoendana na uhalisia wa mambo ukiwamo urahisi katika utekelezwji wake, hali ya uchumi wa walengwa na viwango vya adhabu na faini.

Alisema Sheria ya The Electronic and Postal Communication, Regulations 2020, imeweka masharti yasiyo na uhalisia yenye zuio la mtu kumiliki zaidi ya laini moja ya simu kutoka kampuni moja ya simu.

Vilevile, alisema wamebaini sheria ndogo kukiuka haki za binadamu, akiitolea mfano Sheria ya The Transport Licensing Act (Sura 317) ambayo mtu anaweza kufutiwa leseni bila hata kupewa nafasi ya kusikilizwa.

Alisema kuwa katika mikutano hiyo miwili, kamati yao ilipitia na kuchambua sheria ndogo 2,601.
 
Mwaka wa uchaguzi mtatetea hata nzi. Leo ndo mnaona ubaya wa sheria mnazopitisha kishabiki? Ndugai umeandika historia ya kuwa Spika "Mpuuzi" (Kwa sauti ya Makonda) kuliko watangulizi wako wote.
 
Matapeli hao, uchaguzi umekaribia ndio wanaanza itapeli wao, kelele zote zilizopigwa wakati ule hamkuzijibu leo ndio wamepata majibu yake!.
 
Wameona wana karibia kuridi vijiweni ndio wana wanaongea mambo hivi.. maana wanajua vipanda vya mpesa vitawahusu.
 
Hizi sheria zote waliozitunga na kuzipitisha kwa kura nyingi za ndiyo ni wabunge wa CCM. Wanafurahia maumivu ya Wananchi kwa maslahi yao.Tuwakatae wao na washangiliaji wa utawala huu.

Sheria zinapitishwa kishabiki na baada ya muda mfupi wanasema ni kandamizi zibadilishwe badala ya kuwawajibisha waliozileta na kuzipitisha.

Huu ni uhujumu uchumi kwa kupoteza muda wa bunge na gharama zitokanazo na utekelezaji pamoja na waathirika wa hizi sheria.Wapi tayari kuwapa fidia kwa usumbufu waliosababishiwa?
 
Matapeli hao, uchaguzi umekaribia ndio wanaanza itapeli wao, kelele zote zilizopigwa wakati ule hamkuzijibu leo ndio wamepata majibu yake!.
They're slow learners, huwa wanapinga ushauri na mawazo mbadala ndipo baada ya miaka wanakuja kushtuka kwamba ulikuwa ushauri mujarab.Kumbuka elimu bure walivyopinga,kuhusu uwekezaji kwenye madini,hili LA sheria mbovu ndiyo karata yao.

Wanakataa katiba mpya ila kwa kuja na miswada kwa hati za dharuru wapi mstari wa mbele.Hapo ujue ni aina yao ya kushawishi wapiga kura kwa ajili ya kuwachagua October 2020.
 
They're slow learners, huwa wanapinga ushauri na mawazo mbadala ndipo baada ya miaka wanakuja kushtuka kwamba ulikuwa ushauri mujarab.Kumbuka elimu bure walivyopinga,kuhusu uwekezaji kwenye madini,hili LA sheria mbovu ndiyo karata yao.

Wanakataa katiba mpya ila kwa kuja na miswada kwa hati za dharuru wapi mstari wa mbele.Hapo ujue ni aina yao ya kushawishi wapiga kura kwa ajili ya kuwachagua October 2020.
Hapa humuoni paskali, bia wala kipara kipya. Nzi wa kijani humuoni hapa
 
Hii sheria ili itekelezwe inabidi mitandao yote ya simu iwe na bei sawa za vifurushi vya dakika, ujumbe mfupi na intaneti.

Pia mitandao yote itoe huduma za kiwango sawa, kasi, uhakikanwa huduma bora.

Watu wengi unakuta ana sim card zaidi ya mbili, atakuambia Tigo ana bei nafuu za vifurushi vya dakika, voda siku akiwa na pesa anatumia intaneti yenye kasi, halotel anatumia intaneti ya usiku.

Hayo maisha ya kuhama hama tumeshayazoea kwa sababu mitandao ya simu iko huru kubadilisha badilisha bei za vifurushi wanavyotaka
 
Back
Top Bottom