Bunge libadili Sheria ya makosa ya jinai, mtu anekamatwa nyumbani/ mtaani ni lazima mjumbe wa nyumba kumi na Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wawepo

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
15,522
22,457
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwepo na hali ya sintofahamu pale ambapo watu wapotea tu mitaani na vitongojini na baadae kuja kupatikana wakiwa hoi na taabani.

Wananchi hawa hukutwa maeneo hatarishi kama misituni na pembezoni mwa barabara huku wakiwa na majeraha makubwa kwenye miili yao na huenda majeraha hayo ni ya kudumu.

Natoa pendekezo kwa serikali kupitia wizara ya mambo ya ndani na bunge kubadilisha sheria ya makosa ya jinai ili kuwapa nafasi wale wanokamatwa au kutekwa na polisi waweze kueleza wapi wapelekwa.

Yaani wa kifupi ni kwamba polisi/ wasojulikana na watu wa aina hiyo ni lazima watoe taarifa kwa mjumbe wa nyumba 10 pamoja na mwenyekiti wa serikali ya mtaa kuhusu kutaka kumkamata mtu yoyote waneona kwamba amevunja sheria.

Sheria hii pia izuie vyombo vya dola kuwasaka, kuwawinda na kuwkamata watu mitaani hovyo kwa kuwafunga vitambaa machoni na kuwapeleka kusikojulikana bila kibali maalum cha kamanda wa polisi wa Wilaya.

Sheria hii itamke kwamba watu wakamatwe rasmi majumbani ,au maofisini ambako wapo mashahidi.

Hiyo itasaidia uweka kumbukumbu sawa endapo kutatokea mtu kapotea kitaa na vitongojini.

Copy kwa waziri wa Mambo ya Ndani mheshimiwa Masauni.
 
Ushauri wako ni wa msingi sana. Iwapo polisi watamkamata mtu bila kuujulisha uongozi waitwe watekaji na wafunguliwe kesi ya kuteka. Maana watekaji na polisi wote wanavaa nguo za kiraia wanatuchanganya. Kwa hiyo hata kama mtu anatekwa raia wema wanashindwa kutoa taarifa kwa wakati wakidhani ni polisi kumbe watu wabaya.
 
Ushauri wako ni wa msingi sana. Iwapo polisi watamkamata mtu bila kuujulisha uongozi waitwe watekaji na wafunguliwe kesi ya kuteka. Maana watekaji na polisi wote wanavaa nguo za kiraia wanatuchanganya. Kwa hiyo hata kama mtu anatekwa raia wema wanashindwa kutoa taarifa kwa wakati wakidhani ni polisi kumbe watu wabaya.
Hoja, ili kukabiliana na utekaji swali fikirishi watajuaje kama siyo polisi jibu sikuhizi kuna polisi kata tunaomba washilrikishwe
 
Hoja, ili kukabiliana na utekaji swali fikirishi watajuaje kama siyo polisi jibu sikuhizi kuna polisi kata tunaomba washilrikishwe
Uko sawa kabisa, lakini polisi kata aweza kutokea sehemu ingine.

Ila mjumbe wa nyumba 10 ndie shahidi namba moja baada ya familia.

Mw/kiti wa serikali ya mtaa ni shahidi namba mbili.

Lakini polis kata aweza kuandikisha maelezo katika dawati lao la polisi kata.
 
Ushauri wako ni wa msingi sana. Iwapo polisi watamkamata mtu bila kuujulisha uongozi waitwe watekaji na wafunguliwe kesi ya kuteka. Maana watekaji na polisi wote wanavaa nguo za kiraia wanatuchanganya. Kwa hiyo hata kama mtu anatekwa raia wema wanashindwa kutoa taarifa kwa wakati wakidhani ni polisi kumbe watu wabaya.
Mkuu nakubaliana na wewe ..

Wanaokuja kuteka au kukamata wanavaa kiraia ...

Tena wakiwa polisi au sio polisi wote wana silaha ...

Wakiwa ni polisi au sio polisi wote wana magari

Wakiwa polisi au sio polisi wanapendelea usiku kuanzia SAA 4 usiku

Ila kwa kumalizia ...UPANDE WANGU WANAOTEKA AKILI YANGU INANIAMBIA WENGI WANAOFANYA HIVYO LAZIMA WANA UHUSIANO NA VYOMBO VYA DOLA
 
Wazo zuri, japo kwa mijini watatafutwa wenyeviti wa mchongo
Hapo ndipo wananchi lazima wawafahamu wajumbe wao wa nyumba 10 na mwenyekiti wa serikali ya mtaa kwa majina na wanapoishi.
 
Hii iende sambamba na kuondoa au kufanyia marekebisho sheria ya ugadi. Sheria inatoa mwanya kwa uonevu wote kufanyika kwa kisingizio cha ugaidi.!
 
Wazo lako ni zuri, ila kama ni polisi kweli na kesi inahusu mambo mengine. Ila kama kesi inahusu haya mambo ya siasa hawatafanya hivyo. Na ikiwa ni watekaji ndiyo kabisa, huyo masauni mwenyewe, juzi kasema yeye ndiyo mwenye polisi. Hapo tusitegemee miujiza.
 
Hii iende sambamba na kuondoa au kufanyia marekebisho sheria ya ugadi. Sheria inatoa mwanya kwa uonevu wote kufanyika kwa kisingizio cha ugaidi.!
Sawasawa.

Kawaida mtuhumiwa wa ugaidi au mwingine polisi wana masaa 24 kumhoji na kumfungulia mashtaka.

Sheria ibadilishwe kuwazuia polisi na wasojulikana kukaa na mtu wakimhoji na kumtesa kwa zaidi ya masaa 24.

Polisi wakitaka kuendelea kuhoji mtuhumiwa zaidi ya masaa 24 ni lazima waombe kibali cha mahakama na jaji aruhusu, la sivyo mtuhumiwa aachiwe kwa dhamana.
 
Uko sawa kabisa, lakini polisi kata aweza kutokea sehemu ingine.

Ila mjumbe wa nyumba 10 ndie shahidi namba moja baada ya familia.

Mw/kiti wa serikali ya mtaa ni shahidi namba mbili.

Lakini polis kata aweza kuandikisha maelezo katika dawati lao la polisi kata.
Mjumbe wa nyumba 10 ni cheo cha CCM
 
Mjumbe wa nyumba 10 ni kiongozi rasmi wa serikali??
Ndio kwani ni kiongozi wa ngazi ya kaya.

Kwani umesahau kuna Kaya, Shina, Kijiji, Kata, Tarafa, Wilaya hadi mkoa?

Huyo ni shahidi namba moja.

Mie mjumbe wangu wa nyumba kumi aitwa mzee Kizuguto.

Na mwenyekiti wa serikali yangu ya mtaa aitwa mzee Akilimali.
 
Uko sawa kabisa, lakini polisi kata aweza kutokea sehemu ingine.

Ila mjumbe wa nyumba 10 ndie shahidi namba moja baada ya familia.

Mw/kiti wa serikali ya mtaa ni shahidi namba mbili.

Lakini polis kata aweza kuandikisha maelezo katika dawati lao la polisi kata.
Polisi kata wanajulikana yaani wewe usipo mfahamu mwenyekiti wa mtaa atamfahamu halafu hawa polisi kata wana weledi wa kutosha
 
Mjumbe wa nyumba 10 ni cheo cha CCM
Sheria yaweza kubadilishwa ili mjumbe wa nyumba kumi achaguliwe kwa kura katika nyumba hizo kumi na watambulike kisheria na kiserikali kama wawakilishi wake wa kujitolea.
 
Uko sawa kabisa, lakini polisi kata aweza kutokea sehemu ingine.

Ila mjumbe wa nyumba 10 ndie shahidi namba moja baada ya familia.

Mw/kiti wa serikali ya mtaa ni shahidi namba mbili.

Lakini polis kata aweza kuandikisha maelezo katika dawati lao la polisi kata.
Mjunbe wa nyumba 10 ni shahidi sawa lakini hawezi kuwatambua watekaj,labda kama hujauelewa uzi huu nakushauri usome vizuri
 
Wazo lako ni zuri, ila kama ni polisi kweli na kesi inahusu mambo mengine. Ila kama kesi inahusu haya mambo ya siasa hawatafanya hivyo. Na ikiwa ni watekaji ndiyo kabisa, huyo masauni mwenyewe, juzi kasema yeye ndiyo mwwnye polisi. Hapo tusitegemee miujiza.
Masauni kongea kitabaka zaidi na kwa kutofahamu mipaka ya kazi zake.

Waziri mwenye dhamana kama hiyo hawezi kutamka maneno kama hayo hadharani.

Ni kukiuka haki za biandamu pale serikali inapotumia njia za kinazi kukamata watu mitaani au kuwateka bila mtu yoyote kutaarifiwa.
 
Masauni kongea kitabaka zaidi na kwa kutofahamu mipaka ya kazi zake.

Wazroi mwenye dhamana kama hiyo hawezi kutamka maneno kama hayo hadharani.

Ni kukiuka haki za biandamu pale serikali inapotumia njia za kinazi kukamata watu mitaani au kuwateka bila mtu yoyote kutaarifiwa.
Hii hali isipo dhibitiwa Sasa huko mbeleni watu watafanya yao yaani Sheria mkononi
 
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwepo na hali ya sintofahamu pale ambapo watu wapotea tu mitaani na vitongojini na baadae kuja kupatikana wakiwa hoi na taabani.

Wananchi hawa hukutwa maeneo hatarishi kama misituni na pembezoni mwa barabara huku wakiwa na majeraha makubwa kwenye miili yao na huenda majeraha hayo ni ya kudumu.

Natoa pendekezo kwa serikali kupitia wizara ya mambo ya ndani na bunge kubadilisha sheria ya makosa ya jinai ili kuwapa nafasi wale wanokamatwa au kutekwa na polisi waweze kueleza wapi wapelekwa.

Yaani wa kifupi ni kwamba polisi/ wasojulikana na watu wa aina hiyo ni lazima watoe taarifa kwa mjumbe wa nyumba 10 pamoja na mwenyekiti wa serikali ya mtaa kuhusu kutaka kumkamata mtu yoyote waneona kwamba amevunja sheria.

Sheria hii pia izuie vyombo vya dola kuwasaka, kuwawinda na kuwkamata watu mitaani hovyo kwa kuwafunga vitambaa machoni na kuwapeleka kusikojulikana bila kibali maalum cha kamanda wa polisi wa Wilaya.

Sheria hii itamke kwamba watu wakamatwe rasmi majumbani ,au maofisini ambako wapo mashahidi.

Hiyo itasaidia uweka kumbukumbu sawa endapo kutatokea mtu kapotea kitaa na vitongojini.

Copy kwa waziri wa Mambo ya Ndani mheshimiwa Masauni.

INASIKITISHA WALLAH.
 
Back
Top Bottom