Bunge Leo laahirishwa Sababu wabunge wa CCM wanaenda kufanya kazi za chama na posho wamechukua

Wanaenda kula kiapo cha kulindana. Baada ya kugundulika na CAG wizi wa kutisha serikali inahaha kujinasua na karata walio nayo ni kutumia watu kama kina msukuma , kibajaji na wengine wa namna hiyo.
Tupo macho na tutafichua kila ufisadi aliobaini CAG ikiwa ni pamoja na posho za bunge zinazolipwa leo kwenye kikao cha ccm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eeeh Mungu teta na wanaoteta nawe na sema na wanaosema nawe. Katika maisha ya mwanadamu siku zote Mungu pekee huwa anatoa majibu sahihi na wakati sahihi. Katika hili la spika na CAG naona Mungu atajidhirisha na uzuri Mungu hachelewi wala hajawahi kuwahi kadri ya mwanadamu atakavyo bali kwa mapenzi ila mwana wa Adam apate kuinuliwa.

Aibu inakuja mda na wakati usiojulikana.

Eeeh Mungu lia na wanaokulilia na ufurahi na wanaofurahi katika kweli ila tu Mungu napiga magoti kwako nikiomba mapenzi yako yatimizwe.

Tumsifu aliye Juu ya viumbe vyote.

Katika viumbe vyote duniania alivyoumba Mungu mwanadamu ndie kaumbika na ndo mwenye majanga zaidi maana husuda,unafiki,fitina, uongo, usaliti, kuabudu sanamu, nk vi Juu yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Posho warudishe wakachukua za ccm ambazo hawajazipeleka nssf , chama cha mafisadi ni noma wameamua kuzipiga posho mchana kweupe .
 
Nafikiri kuna jambo LA maana , Mh Rais anajua umuhimu wa vikao vya bunge hawezi kufanya hivyo bure, tusubiri tusilaumu kabla ya kujua madhumuni ni nini
@bunge_tz limeahirishwa saa 4.45 kisa ni wabunge wa CCM wanakwenda kukutana na Mkt wa chama Ndg @MagufuliJP kumbuka wabunge Leo watajilipa posho zaidi ya mil 90 pesa za walipa kodi watanzania ili hali wanafanya kazi za chama. Haya ni matumizi mabovu ya Pesa zetu

#2020CCMMustGo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nakubaliana na wewe lakini yule ndugai naona kama anatumwa tuu.
bado naamini bwana JOHN POMBE MAGUFULI ana matatizo makubwa sana.
ivi kulikuwa na ulazima gani wa kumpamdisha CDF Jukwaani kuwatisha watu? iv panaulazima wwte wa kumpa DG Wa TISS mike kisa tu kasoma kigonsera?
Kwani hao watu hawapaswi kuongea na Watanzania?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Spika amekurupuka sana suala la CAG.
Lisipochukuliwa kwa umakini litaipotezea CCM na serikali yake heshima ,huku wabunge wa CCM na madiwani wao wakitegemea Mbeleko za kura za bunduki , risasi na mabomu badala ya Karatasi na kalamu.

Kiburi chote cha Ndugai na Wabunge wa CCM ni kutegemea kura za bunduki,risasi ,mabomu na virungu lakini wananchi wanachukizwa sana na tabia yao ya kupuuza maoni ya wananchi huku akiweka mbele maslahi yao.

Kuna tofauti gani na wapinzani waliokataa kufanya kazi na Mh. Rais na kutoka nje wakati wa kulifungua bunge?
Wabunge wa CCM nao wameanza kususia wateule wa Rais ? Huku ni kumhujumu Rais waziwazi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika maisha kuna vitu utofaulu kuvidhibiti,mfano ukweli hata ukiuwa watu wanaibuka wengine wenye nguvu zaidi ya aliyeuwawa.
 
Spika amekurupuka sana suala la CAG.
Lisipochukuliwa kwa umakini litaipotezea CCM na serikali yake heshima ,huku wabunge wa CCM na madiwani wao wakitegemea Mbeleko za kura za bunduki , risasi na mabomu badala ya Karatasi na kalamu.

Kiburi chote cha Ndugai na Wabunge wa CCM ni kutegemea kura za bunduki,risasi ,mabomu na virungu lakini wananchi wanachukizwa sana na tabia yao ya kupuuza maoni ya wananchi huku akiweka mbele maslahi yao.

Kuna tofauti gani na wapinzani waliokataa kufanya kazi na Mh. Rais na kutoka nje wakati wa kulifungua bunge?
Wabunge wa CCM nao wameanza kususia wateule wa Rais ? Huku ni kumhujumu Rais waziwazi.


Sent using Jamii Forums mobile app
Wananchi mngeamka mdai/,tudai katiba mpya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namhurumia sana Prof. Assad. Najihurumia mwenyewe kuwa mtanzania, nawahurumia watanzania tuakavyoteseka chini ya majinamizi ya CCM, Naumia jinsi watanzania tunavyonyanyasika na kodi zetu kuchezewa kijinga hivi.

Ilitakiwa awamu nzima iwajibike wameshindwa kusimamia kodi zetu.
 
Kama CCM ni gari basi kazi kubwa ingekuwa kulegeza tairi ili likifika hapo mbele liingie kwenye korongo tujue moja.
Hakuna adui mkubwa wa nchi hii kama CCM, hili ni genge la watu hatar kuliko kundi la chatu pori.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hawa ni certified gang criminals like mafia au alqaeda,wanapora ushindi wa watu,wanaua, wanateka,wanakwiba kodi zetu,wanatunyonga kwa kutusomesha no.
 
Kwani wakienda huko au wakibakia bungeni kuna tofauti gani?!

Daaah huu ni ukweli mchungu, maana mambo yao yote ya bungeni huwa yanapitishwa na party caucas. Hivyo wakae bungeni au woteke bado kinachopitishwa na chama ndio kinachopitishwa bungeni.
 
Ingekuwa ni wengine wale watoto wa kambo polisi wasingeruhusu wakutane na mwenyekiti wao
 
bunge limeahirishwa saa 4.45 kisa wabunge wa CCM wanakwenda kukutana na Mkt wa chama Dk Magufuli kumbuka kuwa wabunge Leo watajilipa posho zaidi ya mil 90 pesa za walipa kodi watanzania ili hali wanafanya kazi za chama. Haya ni matumizi mabovu ya Pesa zetu.

Haiwezekani wabunge Leo waone vikao vya maslahi ya taifa tena kikao cha Bajeti cha taifa hakina maana yoyote ila kikao cha chama ndio kina maana sana, Leo wabunge wao watajilipa posho bila kuifanyia kazi yoyote,



Sent using Jamii Forums mobile app
Bunge dhaifu .
 
Back
Top Bottom