Bunge lasitisha Shughuli zake ili kujadili bei ndogo ya Mahindi nchini

Bunge limesitisha kwa muda shughuli zake za leo ili kujadili changamoto ya bei duni inayowakumba wakulima wa mahindi nchini. Wabunge wameeleza kutoridhishwa na bei ndogo ya mahindi, bei ghali ya mbolea hivyo wameitaka Serikali kuiongeza hela NFRA ili inunue mahindi kwa wakulima.

Waziri wa Kilimo, Prof. Adolph Mkenda amekiri uwepo wa tatizo la bei ndogo ya mahindi. Ameeleza kuwa Serikali inachukua hatua za haraka kushughulikia suala hilo ambapo ameahidi kuwa kabla ya Bunge kuhitimishwa hapo kesho Serikali itatoa tamko bungeni kuhusu hatua ilizochukua.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameeleza kuwa Serikali imesikia kilio na Serikali na kupitia NFRA ilianza kununua mahindi kwa wakulima lakini imegundua kuwa uzalishaji wa mwaka huu ni mkubwa na Serikali imefanya mazungumzo na mataifa jirani ili kununua mahindi hapa nchini.
Mahindi ni Nishati.

Hili halina maswali liko dhahiri.

Kilimo cha Mahindi ni Kilimo kisichokoma-Hili Ndilo zao letu la Msingi.

Tatizo ninaloliona katika hili zao ni hivi:

1.Kwanza kabisa ni nini BEP(Break Even Point)Ya Kilimo cha Mahindi kwa Ekari moja?

2.Kwa ni nini tunadhani Tsh 50000 kwa gunia ni bei ndogo?

3 Hayo Mahindi yako wapi?
Kwa nani?

Hii ni sawa na kufuga ndege walioko kwenye Miti huko shambani halafu unajihesabia kwamba ni Mali ya familia-Simply kwa sababu wamekaa juu ya mti wa nyumbani.


Tizama:

FWP walitoa takwimu za Post Harvest Losses kuwa ni mpaka 40%...

Hapa ndipo ilipo economic intelligence...

Serikali Itafute suluhisho l UHIFADHI WA MAHINDI KWA KUWEKEZA KWENYE MODERN SILOS-?integrated.

Silos nyingi kwa kila Mkoa..

Na hizo ziitwe FOOD BANKS-THEN BIASHARA IANZIE HAPO.

YAKO NA MENGINE MENGI BUT LET US START FROM THIS ANGLE.
 
Bunge limesitisha kwa muda shughuli zake za leo ili kujadili changamoto ya bei duni inayowakumba wakulima wa mahindi nchini. Wabunge wameeleza kutoridhishwa na bei ndogo ya mahindi, bei ghali ya mbolea hivyo wameitaka Serikali kuiongeza hela NFRA ili inunue mahindi kwa wakulima.

Waziri wa Kilimo, Prof. Adolph Mkenda amekiri uwepo wa tatizo la bei ndogo ya mahindi. Ameeleza kuwa Serikali inachukua hatua za haraka kushughulikia suala hilo ambapo ameahidi kuwa kabla ya Bunge kuhitimishwa hapo kesho Serikali itatoa tamko bungeni kuhusu hatua ilizochukua.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameeleza kuwa Serikali imesikia kilio na Serikali na kupitia NFRA ilianza kununua mahindi kwa wakulima lakini imegundua kuwa uzalishaji wa mwaka huu ni mkubwa na Serikali imefanya mazungumzo na mataifa jirani ili kununua mahindi hapa nchini.
Bunge la wapumbavu n wajinga ndio wamejaa humo
 
Wanafanya FUTUHI tu ,sijawai kuona faida ya bunge la ndugai...hawatetei wananchi hata kidogo wapo kimaslahi.
 
Nchi za SADC ni walaji wakuu wa mahindi. Kutokana na Globalisation wakazi wengi wa nchi hizi wanaishi Ulaya, Marekani na Australia. Hawa ni wateja wazuri wa unga wa mahindi.

Kampuni ya Iwisa ya South Africa imefanikiwa kupeleka unga wa Iwisa nchi zote nilizotaja hapoejuu. Waganda pia wanasafirisha unga wa Maganjo kwenda Sweden.

Wasomi wetu mnakwama wapi?
Sio tatizo la wasomi. Jaribu kufanya biashara ya kusafirisha mazao nje ndipo utakapoifahamu serikali ya Tz. ikoje kiuhalisia.
 
Bunge limesitisha kwa muda shughuli zake za leo ili kujadili changamoto ya bei duni inayowakumba wakulima wa mahindi nchini. Wabunge wameeleza kutoridhishwa na bei ndogo ya mahindi, bei ghali ya mbolea hivyo wameitaka Serikali kuiongeza hela NFRA ili inunue mahindi kwa wakulima.

Waziri wa Kilimo, Prof. Adolph Mkenda amekiri uwepo wa tatizo la bei ndogo ya mahindi. Ameeleza kuwa Serikali inachukua hatua za haraka kushughulikia suala hilo ambapo ameahidi kuwa kabla ya Bunge kuhitimishwa hapo kesho Serikali itatoa tamko bungeni kuhusu hatua ilizochukua.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameeleza kuwa Serikali imesikia kilio na Serikali na kupitia NFRA ilianza kununua mahindi kwa wakulima lakini imegundua kuwa uzalishaji wa mwaka huu ni mkubwa na Serikali imefanya mazungumzo na mataifa jirani ili kununua mahindi hapa nchini.
Yani bado hatuna suluhisho tu. Nilidhani mwanangu hatoona hizi changanoto, zitaishia kwangu. Sasa naona wajukuu pia watazishuhudia hizi seleka. Loh!
 
Serikali ifungue mipaka ya soko la nje ili tukauze huko. Hakuna haja ya kujadili Mambo ya kizembe hivyo. kwani hawajui tatizo? Au wanataka waunde kamati za kijinga
Mkuu mipaka mbona iko wazi yote?kwa sasa soko kubwa liko kenya, sasa arusha mahindi yako kibao, mtu ataacha kuyachukua hapo, karibu aende rukwa, songea, katavi, songwe, kuyafuata?ni ngumu sana!!hapo hadi ukanda huo yapungue sana ndio wataanza kuyafuata huko mbali.
 
Toka mwanzo nilisema, pesa waliyopewa NFRA ni matusi kwa wakulima wa nchi hii!! Wakulima wanadhoofishwa na pia tunaiweka nchi hatarini kwa kukumbwa na janga la njaa endapo mvua hazitakuwa nzuri msimu ujao wa kilimo! Pesa za Tozo baadhi zipelekwe NFRA maana kilimo ni uti wa mgongo wa nchi yetu, waongezewe pesa!!!
Acha watie akili tu, kwani hii ni mala ya kwanza kutokea hiii hali??toka 2016 serikali ilipoanza kuipa NRFA, pesa kidogo toka uwezo wa kununua MT 300, 000, hadi MT 80, 000 tu kwa mwaka, ndipo tatizo lilipoanzia, kwani serikali imekuwa ikinunua kiwango kidogo sana cha mahindi, na hali hii kuna mwaka nadhani 2017 au 18, unga ulifikia tsh.2000@kilo, kwani maghara hayakuwa na chakula cha kutosha!!miaka yote ya nyuma walikuwa lazima wanunua kuanzia tani 300, 000!!akaja meko zikawa ni tani 80, 000!!na kwa sasa serikali haina uwezo wa kununua mahindi yote, we subiria kauli ya waziri mkuu leo!!!juzi katibu mkuu wa ccm, alipotoa maelekezo yale , waziri alimjibu nini?kuwa hakuna pesa tena, ya kuongeza.
Wakulima wa nchi hii ni wakuonea huruma tu.
 
Acha watie akili tu, kwani hii ni mala ya kwanza kutokea hiii hali??toka 2016 serikali ilipoanza kuipa NRFA, pesa kidogo toka uwezo wa kununua MT 300, 000, hadi MT 80, 000 tu kwa mwaka, ndipo tatizo lilipoanzia, kwani serikali imekuwa ikinunua kiwango kidogo sana cha mahindi, na hali hii kuna mwaka nadhani 2017 au 18, unga ulifikia tsh.2000@kilo, kwani maghara hayakuwa na chakula cha kutosha!!miaka yote ya nyuma walikuwa lazima wanunua kuanzia tani 300, 000!!akaja meko zikawa ni tani 80, 000!!na kwa sasa serikali haina uwezo wa kununua mahindi yote, we subiria kauli ya waziri mkuu leo!!!juzi katibu mkuu wa ccm, alipotoa maelekezo yale , waziri alimjibu nini?kuwa hakuna pesa tena, ya kuongeza.
Wakulima wa nchi hii ni wakuonea huruma tu.
Itakuwa ni aibu mwakani kilo ya unga itakapofika 3,000/= kwa kilo kwa ukisefu wa akiba ya mahindi, wakati mwaka huu uzalishaji umekuwa mkubwa, ni kiasi cha kununua tu na kuhifadhi!!!
 
Soko liko nje. Nchi ifunguliwe kwelikweli wakulima/wafanya biashara wajiconnect na masoko ya nje kama umasikini wa kutupwa utaendelea kuwepo nchini. Hii kuendekeza umachinga badala ya kuvutia vijana kwenye kilimo inaua nchi.

Kenya sasa ndio imekuwa dalali mkuu wa Tanzania. Mazao yanakimbiziwa Kenya ndio yawe exported. Viongozi Tz wamekalia talalila za kisiasa huku wanawawekea kauzibe wanaotaka kujiendeleza kimataifa kupitia kilimo.
umenichekesha wewe. jaribu kuomba kibali cha kufanya biashara ya mazao nje ya nchi. ndio utajua urasimu ni nini?. utatembea wewe kutafuta vibali mpaka mahindi yatakutana na ya mavuno ya mwakani hujapata kibali
 
Uliona hivyo jua mahindi yao ndo yamedoda wanataka serikali iyanunue, Bunge halijawahi tetea wananchi.
 
Mbona mafuta ya kila yapo juu hawajadili!? Ukiona hivyo ujue mahindi yao hayauziki!!! Fisi hao
 
Tanzania kuendelea kwa akili hizi hata miaka 10,000 haiwezekani.

Miaka zaidi ya 60 ya uhuru bunge linajadili kuuza mahindi kama mahindi badala ya kuuza bidhaa zitokanazo na mahindi kweli......!

Hakika hata huko shuleni tunafundishana ujinga ujinga tu.
Bunge bila wapinzani ni mavi
 
Acha watie akili tu, kwani hii ni mala ya kwanza kutokea hiii hali??toka 2016 serikali ilipoanza kuipa NRFA, pesa kidogo toka uwezo wa kununua MT 300, 000, hadi MT 80, 000 tu kwa mwaka, ndipo tatizo lilipoanzia, kwani serikali imekuwa ikinunua kiwango kidogo sana cha mahindi, na hali hii kuna mwaka nadhani 2017 au 18, unga ulifikia tsh.2000@kilo, kwani maghara hayakuwa na chakula cha kutosha!!miaka yote ya nyuma walikuwa lazima wanunua kuanzia tani 300, 000!!akaja meko zikawa ni tani 80, 000!!na kwa sasa serikali haina uwezo wa kununua mahindi yote, we subiria kauli ya waziri mkuu leo!!!juzi katibu mkuu wa ccm, alipotoa maelekezo yale , waziri alimjibu nini?kuwa hakuna pesa tena, ya kuongeza.
Wakulima wa nchi hii ni wakuonea huruma tu.
Ni wa ccm usiwaonee huruma acha wasote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom