Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,879
- 16,311
Katika tamko lake, Bunge hilo limesema vikosi vya usalama vilitumika si kwa lengo la kulinda wapiga kura, bali kuwatishia, kuwatia mbaroni, kuwatesa na hata kuua baadhi ya wapinzani wa kisiasa. Kwa mujibu wa kauli hiyo, mazingira ya uchaguzi yalitawaliwa na hofu, ukandamizaji na vizuizi vilivyolenga kuzuia ushindani wa haki wa kisiasa.
Bunge la Ulaya limezitaka Umoja wa Ulaya (EU), nchi wanachama wake pamoja na washirika wa kidemokrasia kuchukua hatua madhubuti dhidi ya wahusika wa vitendo hivyo. Hatua zilizopendekezwa ni pamoja na kuweka vikwazo vinavyolengwa, marufuku ya viza, kufungia mali za wahusika, kusimamisha ushirikiano wa kiusalama, na kupitia upya misaada inayodaiwa kuendeleza au kuhimili ukandamizaji.