PostGE2025 Bunge la Ulaya (EU) lapinga Msaada wa Euro Milioni 156 (Tsh. Bilioni 440+) kwa Tanzania. Wataja Haki za Binadamu na Uchaguzi wa 2025

PostGE2025 Bunge la Ulaya (EU) lapinga Msaada wa Euro Milioni 156 (Tsh. Bilioni 440+) kwa Tanzania. Wataja Haki za Binadamu na Uchaguzi wa 2025

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Tatizo hao unaowashabikia wewe ndiyo wezi mara 1000 wenye lugha laini za kukupumbaza wewe,wanakupa matumaini makubwa yasiyokuwepo, vijana wengi sana wameathirika wakisubiri lissu awe rais wakijua watapata kazi,eti ana majawabu ya ajiri zao 😂😂😂
Kwani hao Akina Lissu unaposema ni wezi wakubwa , ni lini waliwahi shika serikali wakaiba hizo hela emb' tuambie ni wapi waliiba ktk serikali waliyo iongoza.
 
Kwa hiyo leo mnawaita jamaa wa upinde. Ila jana mlipokuwa mnapokea misaada yao walikuwa wqshirika wa kimaendeleo. Kweli Ujinga haina mipaka.

Rasilimali zinasaidia nchi katika maendeleo, Tanzania ya sasa inapiga hatua kila mwaka haijasimama, maendeleo yapo kila sector na yanaendelea kupigwa kila siku!
Wingi wa rasilimali tulizonazo, kasi ya maendeleo iliyopo haiendani hata kidogo na hali mbaya wa maendeleo ya wananchi walio wengi. Shule karibia zote za umma bado watoto wanakaa chini zungukia kidogo shule za Dar na mikoani utaona. Tatizo la maji ni zaidi , Afya madawa hakuna, Haya ndiyo maendeleo ya msingi ambayo kwa sasa yalipaswa kuwa yameisha au karibu na mwisha na sivyo ilivyo sasa.
 
Mwafrika ana asili ya ujinga sana vikwazo hivi pia vitaenda kumkandamiza yeye binafsi lakini atafurahia kama #ZUZU!
Kwa ukubwa wa mwenyezi mungu huenda yeye mshangiliaji ndiyo vikamkaba mara 50!
-Wengine tukiona ya aina hii huwa tunamfikiria mtu wa chini,elewa rais aumii wala hakuna kiongozi ataumia,ni miradi itachelewa kufanyika,infact #UZUZU_MBAYA_SANA.
Poor thinking. Akili za kidikteta na kinyonyaji ndi zipo hivi unavyowaza.

Hujali katika uongozi wako unaacha alama gani. Ukifikiria hapo, utaamua tofauti.

Kwa akili zako miradi na uchumi ukiyumba utawasingizia wazungu tu.
 
Wingi wa rasilimali tulizonazo, kasi ya maendeleo iliyopo haiendani hata kidogo na hali mbaya wa maendeleo ya wananchi walio wengi. Shule karibia zote za umma bado watoto wanakaa chini zungukia kidogo shule za Dar na mikoani utaona. Tatizo la maji ni zaidi , Afya madawa hakuna, Haya ndiyo maendeleo ya msingi ambayo kwa sasa yalipaswa kuwa yameisha au karibu na mwisha na sivyo ilivyo sasa.
So chadema wakiingia watamaliza shida zote miraculous?/ (Jinsi walivyo wezi wenye uchu mkali)
 
Kwa hiyo leo mnawaita jamaa wa upinde. Ila jana mlipokuwa mnapokea misaada yao walikuwa wqshirika wa kimaendeleo. Kweli Ujinga haina mipaka.
Naona kila mwana chadema suala hili limempendeza sana,idiot!
 
Na mfaransa ajongelea Nairobi hapo.

Nasikia wataanza kutengeneza tule tu-umbu tudogo tule.
Yes ni kweli Dunia ya sasa sio ya kutengeneza maadui ni kujenga urafiki na Nchi nyingi ili kizazi kijacho kiwe kwenye mazingira mazuri naona wao wamejiangalia wao na kizazi chetu pekee..
 
Russia hana misaada,elewa kwanza hili,
Russian ana miradi ya kiubia tu,mgawane 50/50.
Russian hana akili za kinyonyaji kama wale jamaa wa 🌈
Russia na wale Mabeberu wote sawa tu Russia mjanja mjanja sana akiona Nchi inateteleka uhusiano na Nchi za jumuiya ya Ulaya yeye na Mchina ndio wanatia miguu mrusi ni rafiki wa Tanzania toka enzi za Mwalimu JK Nyerere ndio waliojenga Chuo cha MUST Mbeya huko ila ndio wale wale bhana..
 
Pamoja na kuwa Mzoga wa nguruwe wenye mvundo; maandishi kama haya ni sawa na ya chizi asiyetambua lolote linaloendelea hapo anapoozea.
Tanzania kuwa na umoja dhidi ya Samia Mhalifu ndilo linalokwenda kuwamaliza waovu nyie; siyo kinyume chake.

Hata mizoga wenzio wengi hilo wamekwishalitambua; umebaki tu wewe na wenzie wachache.

Kawaida huwa sijibishani na mzoga, nimeona tu mara moja hii nikukumbushe.
Your nonsense mayhem are useless gentleman, as our beautiful nation Tanzanians is going to be more powerful, united and stronger than before 🐒
 
Makusanyo ya TRA kwa mwezi kiasi gani?
Kinachokusanywa na TRA kinaishia kutumika ndani ya mwezi husika kwa kulipa mishahara.

Ukitegemea makusanyo ya TRA pekee unaweza usijenge hata kilomita moja ya lami kwa mwaka.

Unapaswa kipewa elimu ya uchumi ili ujue kwanini mataifa ya Afrika yanahitaji na kuhaha kila uchwao kushobokea misaada na mikopo kutoka nje.
 
Ndio, ambayo TRA wanakusanya kwa wiki moja!!
Huna elimu ya uchumi kabisa.

Unadhani ingekuwa makusanyo ya TRA pekee ndiyo yanaleta maendeleo ya nchi, kungekuwa na ulazima wa viongozi wa Kiafrika kuhaha huko nje kutafuta fedha za misaada na mikopo?

Hayo makusanyo unayosema wakati mwingine ni exaggeration tu siasa inachukua nafasi.

Hayo makusanyo unayodai yanaushia kwenye mishahara na government expenditure tu. Sasa shughuli za maendeleo zitafanyikaje?
 
Katika familia, baba ukifanya ujinga wako huko kazini kwako ukakosa mshahara na hivyo watoto kukosa chakula cha kuweka mezani kutibu njaa zao, haya ndiyo yatakuwa matokeo;

1. Watoto ni kweli watakosa chakula na wanaweza kufa kwa njaa

2. Watalalamika na kukulaumu sana baba ni kwanini umeshindwa kuwapa chakula. Hawatafikiria wala kujali sababu utakazotoa kujitetea. Wao wanachotaka kuona ni chakula, wale washibe...

3. Watalia sana huku wakikulaumu na kukulaani kuwa wewe ni baba mbaya, usiyewajali na usiyejua wajibu wako.

4. Wakati mwingine, wanaweza kutamani wapate baba mwingine anayejali na kuwapatia mahitaji yao

##Hiyo👆🏻👆🏻ndiyo scenario inayoikabili serikali hii haramu chini ya CCM na Samia muuaji wa ndugu zetu. Ni kweli kabisa kuwa, tukikosa misaada hii yeye na watoto wake watakuwa wanakula na kushiba hadi kusaza na kumwaga.

##Lakini itamsaidia nini yeye kuwa ameshiba katikati ya mamilioni ya masikini walio na njaa ambao anatamba kuwa anawaongoza, yeye ni Rais wao? Does it make any sense? Hiyo amani ya nafsi yake ataitoa wapi ktk mazingira ya namna hii..?

##Ni kweli kuna maumivu kwa wananchi kwa misaada hii kukosekana lakini katikati ya maumivu hayo, raia/wananchi wataichukia sana serikali kwa kuwa ndiyo chanzo cha magumu na matatizo yao kwa kuwa itakuwa imeshindwa kutekeleza wajibu wake wa kuhudumia wananchi..!!

##Inaweza kusababisha chaos na vurugu (maandamano, migomo, zomeazomea ya viongozi, mauji, uhalifu kuongezeka na maovu mengine). Haya yanapozidi ktk taifa, basi huwa ni ishara ya wazi ya kushindwa kwa serikali iliyopo madarakani..!!

##Tatizo na changamoto hizi zikiwa extreme, serikali iliyoko madarakani inaweza kuanguka hata kabla ya uchaguzi mwingine kuwadia..!

THEREFORE: Think twice before you argue this sensitive issues
BRIGHT HUMAN SEARCH FOR SURVIVAL AND ALWAYS SUCCEED BY 100%.
 
Tatizo akili mbovu tu but tulitakiwa kama nchi hizo Hela sio za Sisi kupagawa wala kushangaa na pia tungekuwa na akili vizuri hizo pesa tungezikataa tu kitambo Sana. Siku zote ukisaidiwa Jua Tu kuna kitu utarudisha au utauza aidha Mali au utu wako...Msaada ni Deni na siyo sifa, MaCCM hayana akili.
Ila na sisi tumezidi kuwa omba omba;

Yaani hivyo ndio vipesa vya kutuendesha namna hiyo.

Hata wao itakuwa wanatucheka baada ya hii kura yao.

Tanzania hatupaswi kabisa kulilia vijipesa kama hivyo.
 
Ila na sisi tumezidi kuwa omba omba;

Yaani hivyo ndio vipesa vya kutuendesha namna hiyo.

Hata wao itakuwa wanatucheka baada ya hii kura yao.

Tanzania hatupaswi kabisa kulilia vijipesa kama hivyo.
Tunapaswa kulilia kiasi gani ili V8 zisikose mafuta na wabunge wasikose posho?
 
Tunapaswa kulilia kiasi gani ili V8 zisikose mafuta na wabunge wasikose posho?
Hizo ni bei za nyumba tu huko ulaya.

Ukiacha ushabiki pembeni na ukatumia akili basi utajua kama nchi hatupaswi kutikiswa na fedha ndogo kama hiyo ya kununulia nyumba.
 
Hizo ni bei za nyumba tu huko ulaya.

Ukiacha ushabiki pembeni na ukatumia akili basi utajua kama nchi hatupaswi kutikiswa na fedha ndogo kama hiyo ya kununulia nyumba.
Achana na ulaya, zungumzia Tanganyika yako, V8 na wabunge na mishahara inaweza hudumiwa na pesa za makusanyo na miradi ya maendeleo isiwe affected?
 
Mwafrika ana asili ya ujinga sana vikwazo hivi pia vitaenda kumkandamiza yeye binafsi lakini atafurahia kama #ZUZU!
Kwa ukubwa wa mwenyezi mungu huenda yeye mshangiliaji ndiyo vikamkaba mara 50!
-Wengine tukiona ya aina hii huwa tunamfikiria mtu wa chini,elewa rais aumii wala hakuna kiongozi ataumia,ni miradi itachelewa kufanyika,infact #UZUZU_MBAYA_SANA.
🥹
 
Bunge la Ulaya limepitisha azimio la kusimamisha msaada wa maendeleo wa takriban Euro 156M (zaidi ya TZS bilioni 440) kutokana na masuala ya ukiukwaji wa haki za binadamu, kukosekana kwa utawala bora, kukandamizwa kwa demokrasia na uhuru wa maoni.

Uamuzi huu ulitangazwa jana Mei 03, 2026, ambapo Kamati ya Maendeleo wabunge 81 waliunga mkono na mmoja kupinga. Katika bunge kubwa (plenary) wabunge 539 waliunga mkono Tanzania kunyimwa pesa hizo, huku wabunge 27 wakiwa neutral na hakuna mbunge hata mmoja aliyepinga.

Sababu zilizotolewa na Umoja wa Ulaya kuinyima pesa TZ:

1. Mauaji ya raia Oktoba 29 na kukosekana kwa uwajibikaji.

2. Kufungwa kwa kiongozi wa upinzani Tundu Lissu na ukandamizaji wa demokrasia.

3. Ukandamizaji wa uhuru wa habari na uhuru wa kutoa maoni.

4. Matukio ya watu kutekwa na kupotea.

5. Kamati ya Ulinzi na Mambo ya Nje ya Bunge la Tanzania kukataa kushirikiana na Bunge la Ulaya ili kufanya uchunguzi huru wa mauaji ya Oktoba 29.

Ikumbukwe pesa hizi si mkopo bali ni msaada, na zililenga miradi ya afya, elimu, maji, nishati etc. Kusimamishwa kwake kunamaanisha miradi mingi inayotegemea ufadhili wa Ulaya itakwama.

EU ipo tayari kuleta fedha hizo ikiwa Serikali ya Tanzania itakubali masharti yafuatayo:

1. Kukubali vyombo vya kimataifa kuchunguza mauaji ya Oktoba 29.

2. Serikali imuachie Tundu Lissu na wafungwa wengine wa kisiasa bila masharti yoyote.

3. Serikali iache kufungia/kuvitisha vyombo vya habari na iruhusu uhuru wa maoni.

4. Serikali ikubali kushirikiana na vyombo vya kimataifa kuchunguza matukio ya watu kutekwa na kupotea.

Kama serikali itakubali masharti hayo EU itaondoa zuio la pesa hizo. Lakini kama itakataa, tutapoteza pesa hizo na pia kuna uwezekano wa kupoteza misaada mingine ya Ulaya na hata kukabiliwa na vikwazo vya kiuchumi.

Mwaka 2002 Zimbabwe ilifanya uchaguzi na yakatokea machafuko. Umoja wa Ulaya ulipotaka kuchunguza serikali ilikataa. EU ikaweka masharti kama haya na Zimbabwe ikajikuta katika mdororo mkubwa wa kiuchumi. Thamani ya sarafu iliporomoka, uwekezaji wa kigeni ulipungua, na ikajikuta imetengwa kimataifa. TZ ikishupaza shingo inaweza kuingia kwenye mtego kama huo. Bahati mbaya wananchi ndio waathirika.!

Credit : Godlisten Malisa
 
Back
Top Bottom