Bunge la Ujerumani: Serikali ya Tanzania inatakiwa kutafuta mbadala wa mabwawa kuzalisha Nishati ya Umeme

Siwezi k)eza muda kujibu maswali yako. swala lililonileta hapa ni ujerumani against tz coz naelewa tutapunguza kaeneo ka hifadhi na yes kutakua na upotevu wa kiasilimia fulani ka miti na yes percentage chache ya mazingira ila tuna mambo mengi sana tunafanya yanayoharibu mazingira by far kulio hiyo project. So maswala yako ya Norway anzisha uzi mwingine wa maswala ya environmental conservation or else

This proves you don't have a clue to what I have been saying and which in turn you have no idea as to why a foreign country would bother about the welfare of one country in order to preserve own interests. Hata jiwe hana intellectual capacity ya kuelewa hiki nitakachokuambia sasa, nevertheless I will try. Ipo hivi; wanachokifanya Wajerumani ni sawa kwa mtu mwenye jirani ambae ana shamba linaloweza kuwaka moto (wakati yeye ataathirika moto ukianzia kwenye shamba la.jirani yake ambae ni mvivu na mpumbavu) anaamua kumsaidia huyo jirani yake. Kwa akili yako ya ki Magufuli nani anafaidika zaidi?
 
So unamaanisha wanaijua selous vyema kuliko sisi?

Unajua Africa ilikuwa haipo kinchi nchi, Ila Wakoloni ndo wametuchorea mipaka na kutupa mfumo wa nchi. Sasa watu waliokuchorea kuwa nchi yako mwanzo ni hapa mwisho pale somehow wanaifahamu hiyo nchi.
Pia Wana technolojia inayowawezesha kuiona mars na kuichunguza. Hivyo hata kama huku si kwao kuna uwezekano mkubwa kuwa wanapaelewa.
Ila Hapa swala si kupafahamu au la, swala hapa ni kwamba hakuna tutakachopoteza kwa kuwahoji kuwa wao wanaona nini mpaka wapoteze mda kutujadili. raisi anaweza mtuma hata balozi kuwahoji.
Wazungu walipitia hii stage na huenda wanatamani wangerudi nyuma wasahihishe baadhi ya njia walizotumia maana inawezekana industrialization iliambatana na upungufu mkubwa wa kiwango cha oxygen duniani. Na sasa dunia inapoteza uwezo wake wa kujisafisha na hewa chafu. Sijui miaka 10,000 ijayo hali itakuaje kwa vizazi hivyo.
 
Hao ni wapuuzi na mabwabwaishaji kwanza warudishe mjusi wetu.
Baada ya wao kufanikiwa kumaliza vyanzo vyao vyote vya maji na kujipatia umeme wa kutosha(hydroelectric power) ambao ni zaidi ya mara 100 ya umeme utakaozalishwa Rufiji sasa wanataka kutubugudhi.
Watanzania tusipojitambua sasa hatutajitambua milele!!


Germany (357,386 km² )had a hydropower installed capacity in 2016 of 11,258 MW, including 6,806 MW of pumped storage.[1] In the same year, the country generated 21.5 TWh from .hydroelectric plants, representing about 3% of the country's total electricity generation.

The hydropower capacity in Germany is considered mature and the potential already almost completely exploited, with limited room for growth. In recent years, growth in capacity has mainly come from repowering of existing plants.
Hakuna kitu kizuri kaa elimu, na ukosefu wa elimu ndio unakufanya kuandika haya
 
Ujerumani: Mradi wa umeme wa Tanzania wapigiwa kura bungeni

Bunge la Ujerumani limepitisha mswada wa kuitaka serikali ya Ujerumani itafute njia mbadala ya mradi wa Tanzania wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler ili kulinda turathi na asili.

View attachment 998487

Vyama vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani vimeitaka serikali itafute njia nyingine badala ya ile ya mradi wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler kwenye mto rufiji kusini mwa Tanzania Wabunge wa vyama vya CDU/CSU, Kijani na AFD walishiriki katika kupiga kura hiyo lakini chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD, hakikushiriki. Azimio la vyama vya CDU,CSU na SPD pia linatokana na mapendekezo ya kamati ya serikali ya Ujerumani ya ushirikiano wa kiuchumi.

Azimio lililopitishwa bungeni na vyama hiyvo vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani linaitaka serikali kuu isaidie katika masuluhisho ya kukidhi mahitaji ya nishati ya Tanzania bila ya kuathiri mazingira. Katika azimio lao vyama hivyo vimesema mradi huo mkubwa wa kuzalisha nishati ya umeme utavuruga mfumo wa mto mmojawapo mkubwa barani Afrika.

Tanzania inakusudia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia nguvu ya maji kutoka kwenye mto rufiji. Sehemu hiyo ni muhimu kwa shughuli za kilimo za wakaazi. Ikiwa mradi huo utaendelea mbele bonde la Stiegler ambalo limewekwa miongoni mwa turathi za shirika la Umoja wa mataifa la UNESCO litapoteza hadhi yake na huenda likasababisha athari kubwa katika raslimali zilizopo kwenye sehemu hiyo.
Katika ombi lao kwa serikali ya Ujerumani wabunge wa vyama vya CDU,CSU na SPD wamesema sehemu hiyo ya mbuga ya wanyama ya Selous nchini Tanzania ni eneo kubwa kabisa na kongwe la hifadhi ya wanyama pori barani Afrika.

Wabunge hao wamesema mradi huo wa bwawa la nishati utahitaji sehemu kubwa sana itakayotokana na kukatwa kwa miti na hivyo kusababisha athari kubwa katika mazingira, tabia nchi na katika uchumi.

Wabunge wa chama cha upinzani cha FDP wameshauri kujengwa kinu cha nishati kutokana na gesi kwa sababu Tanzania inayo gesi ya kutosha iliyogunduliwa hivi karibuni. Chama hicho cha upinzani cha FDP kilichopinga azimio hilo kimeitaka serikali ya Ujerumani ifanye mazungumzo na serikali ya Tanzania.

Mwandishi/Zainab Aziz/Daniel Pelz/DW Berlin

Mhariri: Yusuf Saumu

CHANZO: Ujerumani: Mradi wa umeme wa Tanzania wapigiwa kura bungeni | DW | 18.01.2019

Kulikoni Wajerumani eti watupangie matumizi ya rasimali zetu..!!
Selous is in TZ not in German!!!
over!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..mimi ningependa u-argue your case bila kuingiza masuala ya Soveregnity.

..nadhani hoja ya sovereugnity huwa inaibuliwa ili kufukia-fukia hoja zinazotakiwa kujibiwa kitaalamu.

..Wajerumani wametu-challenge kuhusu suala la MAZINGIRA ya Selous na bonde la mto Rufiji.

..Sasa unatakiwa uje na counter-argument za jinsi ya kudhibiti hayo madhara waliyosema yatatokea.

..Kwa upande wa Kihansi naona mambo yalifanyika vizuri. Zilitolewa sababu za kimazingira na wataalamu wakaja na mbinu za kujibu hoja na tahadhari zilizotolewa. At the end of the day tulipata mradi wa umeme, na vilevile tulitunza hao viumbe ambao walikuwa ktk hatari ya kutoweka. Everybody "won" in that case.

..Mimi ninachopendekeza ni serekali iweke wazi tahadhari za kimazingira za mradi huu. Pia tupewe alternative/options za sites nyingine zinazofaa kwa uzalishaji umeme. Na zaidi serekali ieleze hatua itakazochukua kudhibiti madhara kwa mazingira.

NB.

..bonde la mto Rufiji linagusa maisha ya WAKULIMA na WAVUVI. Je, tumefikiria mustakabali wa maisha yao?

hivi kati ya Umeme wa maji (HEP) na gesi (TE) upi ni hatari kwa mazingira?
 
This proves you don't have a clue to what I have been saying and which in turn you have no idea as to why a foreign country would bother about the welfare of one country in order to preserve own interests. Hata jiwe hana intellectual capacity ya kuelewa hiki nitakachokuambia sasa, nevertheless I will try. Ipo hivi; wanachokifanya Wajerumani ni sawa kwa mtu mwenye jirani ambae ana shamba linaloweza kuwaka moto (wakati yeye ataathirika moto ukianzia kwenye shamba la.jirani yake ambae ni mvivu na mpumbavu) anaamua kumsaidia huyo jirani yake. Kwa akili yako ya ki Magufuli nani anafaidika zaidi?

Siku zote nachekaga sana hawa watu wanaojifanya zipo sana. Nani amekataa kuwa hakuna percentage yoyote ya uharibifu? swala ni kwamba kuna uranium, mafuta na madini kibao na pia yanaharibu mazingira ila hawapigi kelele, so why umeme wa maji? because it will not benefit them in any case rather than make us less dependent on their loans. Swala lingine ni kua why now? can they pay us the money we already signed a contract with Egypt? you are so dumb to think they give a shit on any of us
 
Unajua Africa ilikuwa haipo kinchi nchi, Ila Wakoloni ndo wametuchorea mipaka na kutupa mfumo wa nchi. Sasa watu waliokuchorea kuwa nchi yako mwanzo ni hapa mwisho pale somehow wanaifahamu hiyo nchi.
Pia Wana technolojia inayowawezesha kuiona mars na kuichunguza. Hivyo hata kama huku si kwao kuna uwezekano mkubwa kuwa wanapaelewa.
Ila Hapa swala si kupafahamu au la, swala hapa ni kwamba hakuna tutakachopoteza kwa kuwahoji kuwa wao wanaona nini mpaka wapoteze mda kutujadili. raisi anaweza mtuma hata balozi kuwahoji.
Wazungu walipitia hii stage na huenda wanatamani wangerudi nyuma wasahihishe baadhi ya njia walizotumia maana inawezekana industrialization iliambatana na upungufu mkubwa wa kiwango cha oxygen duniani. Na sasa dunia inapoteza uwezo wake wa kujisafisha na hewa chafu. Sijui miaka 10,000 ijayo hali itakuaje kwa vizazi hivyo.

Halafu iweje? kumbuka tumeshaingia mkataba wa 6.5t, watailipa au wanataka kutuongezea maumivu? Tena ni unafk mkubwa
 
Tatizo tunafanya mambo kama vichaa bila kuangalia future ya vizazi vijavyo. Inasikitisha kuna watu hawajui umuhimu wa mazingira watu hawajui..... unaweza ukakata miti bongo ukaathiri Ethiopia
Umeona wakilalamika matumizi ya mkaa?
 
Binafsi ningependa sana suala hili lijadiliwe kwa KITAALAMU na kwa UWAZI. Na pia tujiridhishe kwamba hata kama kuna madhara tunachukua tahadhari ya kudhibiti madhara hayo.

Hili ninakubaliana na wewe moja kwa moja, na sio hili tu linaloonyesha udhaifu mkubwa uongozi tulio nao sasa walivyo. Wao wanadhani kutumia mabavu na kutohojiwa na yeyote katika maamuzi yao ndiyo ishara ya nguvu walizonazo! Mimi naona ni kinyume chake.
Wanaounga mkono mradi wa Stieglers gorge wameshikilia suala la UZALENDO pamoja na UHURU wa kujiamulia mambo yetu ya ndani.

Wapo wa namna hii ndio, na nadhani hili ni jambo linalotokea katika mataifa yote duniani bila kujali ngazi yao ya maendeleo.

Kwa Tanzania naweza kusema lilishika kasi sana enzi za Mwalimu Nyerere.
Niseme wazi, hata mimi sipendezewi kabisa, watu wengine wakwamishe mambo ambayo yako kwenye mipango yetu ya kujikwamua, hasa kukwamisha huko kunapofanywa bila ya kuwepo na ushahidi unaoeleweka.

Wao walipokuwa wnafanya ya kwao, hawakukwamishwa na yeyote. Wanapozungumzia uharibifu wa mazingira inatakiwa wawe na 'data' zisizopingika zinazoonyesha uharibifu utakaoletwa na miradi hiyo; na hata ikiwa hivyo, uamzi wa mwisho ni lazima uwe wetu. Tutapima gharama za kuwa na mradi huo na umuhimu wa mradi katika maendeleo ya taifa letu. Hii ni 'sovereign right' ya taifa lolote.
Sasa ni mzalendo gani anayeharibu mazingira? Je, kuwa huru maana yake ni kufanya mambo bila kujali madhara ya kiuchumi na kimazingira?

Kauli kama hii ya 'uzalendo' na 'wanyonge' zinapotumika kisiasa na kujitafutia sifa binafsi, hata hao walliolengwa ziwachochee sidhani kuwa zinafikisha ujumbe unaotakiwa waupate.

Wajerumani kwa kufanya walivyofanya bungeni kwao wameondoa ushawishi wowote ambao wangeweza kuwa nao katika jambo hili na mengine. Sasa hata vyama kama CHADEMA wakiendelea kuomba msaada wataonekana kuwa upande wa wasiotaka tuamue mambo yetu kwa manufaa yetu wenyewe. Lebo ya "Ubepari" na "usaliti" itakuwa imekolezwa zaidi.

Kiufupi ni kwamba, wameuimarisha zaidi mkono wa watawala wetu kuzidi kutukandamiza.
.
 
Siku zote nachekaga sana hawa watu wanaojifanya zipo sana. Nani amekataa kuwa hakuna percentage yoyote ya uharibifu? swala ni kwamba kuna uranium, mafuta na madini kibao na pia yanaharibu mazingira ila hawapigi kelele, so why umeme wa maji? because it will not benefit them in any case rather than make us less dependent on their loans. Swala lingine ni kua why now? can they pay us the money we already signed a contract with Egypt? you are so dumb to think they give a shit on any of us

You are even dumber not to realise what I have been telling you all this time that although they don't care about us THEY STILL CARE ABOUT THEMSELVES.
And to ensure their wellbeing THEY MUST STOP THE IDIOTS YOU who are trying to DO SOMETHING THAT MAY HARM THEM.
 
Acha ujuha, eneo la kuzalisha umeme wa gas 2100MW umejaribu kulifikiria litakua kubwa kiasi gani? na je umefikiria hatari ya gas yenyewe ukilinganisha na maji, acha cost, acha utaalamu + figisu za kukufanya wewe usiwe na umeme wa kutosha


Hizo siku 7 ulizonipa kimihemko zimeisha? Dogo hapa ukija moto utarudi baridi.
 
You are even dumber not to realise what I have been telling you all this time that although they don't care about us THEY STILL CARE ABOUT THEMSELVES.
And to ensure their wellbeing THEY MUST STOP THE IDIOTS YOU who are trying to DO SOMETHING THAT MAY HARM THEM.

And yet support you to do them whenever they appear to benefit them, men you are so clever. I envy you
 
'Treasure.....' Our Top leaders and some politicians wanafahamu na niwanufaika. Msijichoshe ingieni field...
 
hakuna siku nimechukia wazungu kama leo na bahati mbaya sana naishi kwao!! hawa wazungu ni watu wauaji!hawataki kusikia nchi yoyote masikini duniani ikiendelea, mf India inapewa mabilioni ya dola na Marekani ili kufidia India kuaacha matumizi ya hazina kubwa ya Coal iliyogunduliwa huko India miaka ya karibuni na India iliwambia Marekani haya ni madini yetu yako kwetu na tuna haki ya kuyatumia kuzalisha umeme kama nyie Marekani na nchi za ulaya mlivyofanya wakati wa Industrial Revolution era!! Nchi kama Sweden na Norway zinaweza kuipa bongo mabilioni ya dola mkipeleka tu proposal za kulinda mazingira hasa kuhifadhi misitu na kuanzisha misitu mingine! , hivyo hilo si Ujerumani wabunge kukaa na kudiscuss kudidimiza chini uchumi wa koloni lao si jambo la ajabu, kimsingi Ujerumani bado wanaamini Tanzania ni koloni lao na iko chini yao hadi leo hata kama tulipata uhuru feki! Huu ni ukweli mtupu kwa 100% matumizi ya Coal, Natural Gas na Oil katika kuzalisha nishati huleta athari kubwa za mazingira na kuongezeka kwa joto duniani kwa kasi ambayo sayansi imeshindwa kutabiri, sasa wazungu duniani kote wanahaha la kufanya kupunguza athari za uharibifu wa mazingira kwa namna yoyote.Kuna kitu kitaalam kinaitwa Greenhouse Gas effect ( wasomi please google) hii ni mwiba mkali kwa wazungu duniani kote kwasasa na hawawezi kuicontrol sababu si tunataka kuishi kwenye modernity? . Wazungu wanajua ngozi nyeusi ni mtumwa wao, Afrika ina watu wapumbavu wote , viongozi wote wa Afrika ni wapumbavu na Afrika ina shida ya umeme ndo maana ni maskini daima , haiendelei sasa wakiona mna Rais mwenye akili kama Bwana Mkubwa wetu na mmeanza kufanya practically miradi ya kuondokana na tatizo la nishati , vita yake haitakuwa ndogo! wabongo tumuombee kwa Allah bwana mkubwa
Mwenyezi Mungu amlinde na kumpa maisha marefu Raisi wetu John Magufuli
 
Mtapiga sana kelele humu shubahamiti ila selous project ni mission impossible....period

UNESCO has a clear position that dam projects that harm World Heritage sites should not be built. So far no assessment has been carried out for Stiegler’s Gorge hydropower project. Companies who become involved in the project run the risk of significant reputational damage. We are asking investors, banks and those in the construction industry that work on dams to add Stiegler’s Gorge to their risk register

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom