Bunge la Ujerumani: Serikali ya Tanzania inatakiwa kutafuta mbadala wa mabwawa kuzalisha Nishati ya Umeme

Mkuu Joka Kuu, kwenye hili mimi naungana na serikali yetu kuwa Tanzania is a sovereign state, tutaamua mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa au kupangiwa na mataifa ya nje.

Natolea mfano wa mradi wa Kamba Samaki, shrimp farming kwenye Rufiji Delta, ulipitishwa vizuri tuu, lakini kabla ya utekelezaji, mashirika ya kimataifa ya mazingira yakaja na EIA nyingine, tukapigwa stop mradi ukafa. Hoja ya wanamazingira ni kilimo kile kingeathiri uoto wa asili wa mikoko.

Ukiangalia cost benefits na value benefits za mradi na faida za mikoko, mikoko are nothing compared.

Kama ulifuatilia issue ya Kihansi Hydro Electric Project, mradi ulichelewa sana kwa hoja ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwa relocate wakahamishwa, mradi ulipokamilika wakarudishwa. Ukiangalia faida za nchi inayohitaji umeme na faida ya vyura ni nothing compared.

Sasa kwenye Stieglers ni vile vile wanataka kutupangia, kule nyuma waliweza kwa sababu fedha walikuwa wanatoa wao. Kwa Stieglers, watakwama kwa sababu this time around fedha ni zetu.
Hili jambo niliisha lizungumza sana humu

P

..mimi ningependa u-argue your case bila kuingiza masuala ya Soveregnity.

..nadhani hoja ya sovereugnity huwa inaibuliwa ili kufukia-fukia hoja zinazotakiwa kujibiwa kitaalamu.

..Wajerumani wametu-challenge kuhusu suala la MAZINGIRA ya Selous na bonde la mto Rufiji.

..Sasa unatakiwa uje na counter-argument za jinsi ya kudhibiti hayo madhara waliyosema yatatokea.

..Kwa upande wa Kihansi naona mambo yalifanyika vizuri. Zilitolewa sababu za kimazingira na wataalamu wakaja na mbinu za kujibu hoja na tahadhari zilizotolewa. At the end of the day tulipata mradi wa umeme, na vilevile tulitunza hao viumbe ambao walikuwa ktk hatari ya kutoweka. Everybody "won" in that case.

..Mimi ninachopendekeza ni serekali iweke wazi tahadhari za kimazingira za mradi huu. Pia tupewe alternative/options za sites nyingine zinazofaa kwa uzalishaji umeme. Na zaidi serekali ieleze hatua itakazochukua kudhibiti madhara kwa mazingira.

NB.

..bonde la mto Rufiji linagusa maisha ya WAKULIMA na WAVUVI. Je, tumefikiria mustakabali wa maisha yao?
 
Hujajibu swali langu. Umetoa "faida" za kusadikika ambazo hazijafanyiwa feasibility studies kwenye mazingira na teknolojia ya leo bali ya 1968.

Kuna uhusiano gani kati ya kuchimba au kutochimba uranium Tanzania na Norway kuzuia gadgets ambazo sio green certified kusafirishwa nje ya Norway?
Nimekuuliza hivi: Kinachowafanya Norway wazuie vitu ambavyo sio green certified kutoka nchini mwao kwenda nchi nyingine ni kipi (wakati mtu wa kawaida angedhani wataruhusu vitoke ili kupunguza disposal costs)?
Siwezi kupoteza muda kujibu maswali yako. swala lililonileta hapa ni ujerumani against tz coz naelewa tutapunguza kaeneo ka hifadhi na yes kutakua na upotevu wa kiasilimia fulani ka miti na yes percentage chache ya mazingira ila tuna mambo mengi sana tunafanya yanayoharibu mazingira by far kulio hiyo project. So maswala yako ya Norway anzisha uzi mwingine wa maswala ya environmental conservation or else
 
Don't overule hoja za wasiotaka Stigler's gorge electric dam na kuwaona kama wametumwa na mabeberu kwa kuangalia tu unit cost ya watt moja ya umeme wa maji versus vyanzo vingine. Bali zingatia yafuatayo;
1. 34% ya maji yaliyokuwapo wakati upembuzi yakinifu hayapo baada ya Kihansi Project na shughuli za kininadamu

2. Umeme wa hydro hutegemea sana mvua. Kwa hiyo kuna suala la uncertainty. Ndiyo maana hata Mtera na Kihansi hazikukuwa suluhisho Kwa mahitaji ya umeme nchini kama tulivyoahidiwa nyakati zile

3. Umeme cheap kuliko wote duniani na ambao ni environmental friendly ni solar power.

4. Tumewekeza sana kwenye gas, si vyema hizo investment zikabakia white elephants.

4. Kuna chanzo kingine change umeme mikoa ya Singida na Njombe ambacho ni nguvu ya upepo (windmill)

5. TANESCO wamewekeza tens kwenye umeme wa joto ardhi (Geothermal) kwa tafiti zilizofanyika Mbeya.

Kwa maoni yangu bila kujali sababu za wana mazingira wa Ulaya (mabeberu), uamuzi wa kuendelea na Stiglers gorge ulipaswa uzingatie upembuzi yakinifu mpya kabisa ambao unaweka vyanzo tajwa hapo juu kwenye kikapu kimoja dhidi ya Stigler's gorge.

Otherwise tutunze hii post until 2035 kama Mungu atatujalia uhai...Adios Amigos
 
..mimi ningependa u-argue your case bila kuingiza masuala ya Soveregnity.

..nadhani hoja ya sovereugnity huwa inaibuliwa ili kufukia-fukia hoja zinazotakiwa kujibiwa kitaalamu.

..Wajerumani wametu-challenge kuhusu suala la MAZINGIRA ya Selous na bonde la mto Rufiji.

..Sasa unatakiwa uje na counter-argument za jinsi ya kudhibiti hayo madhara waliyosema yatatokea.

..Kwa upande wa Kihansi naona mambo yalifanyika vizuri. Zilitolewa sababu za kimazingira na wataalamu wakaja na mbinu za kujibu hoja na tahadhari zilizotolewa. At the end of the day tulipata mradi wa umeme, na vilevile tulitunza hao viumbe ambao walikuwa ktk hatari ya kutoweka. Everybody "won" in that case.

..Mimi ninachopendekeza ni serekali iweke wazi tahadhari za kimazingira za mradi huu. Pia tupewe alternative/options za sites nyingine zinazofaa kwa uzalishaji umeme. Na zaidi serekali ieleze hatua itakazochukua kudhibiti madhara kwa mazingira.

NB.

..bonde la mto Rufiji linagusa maisha ya WAKULIMA na WAVUVI. Je, tumefikiria mustakabali wa maisha yao?
Don't overule hoja za wasiotaka Stigler's gorge electric dam na kuwaona kama wametumwa na mabeberu kwa kuangalia tu unit cost ya watt moja ya umeme wa maji versus vyanzo vingine. Bali zingatia yafuatayo;
1. 34% ya maji yaliyokuwapo wakati upembuzi yakinifu hayapo baada ya Kihansi Project na shughuli za kininadamu

2. Umeme wa hydro hutegemea sana mvua. Kwa hiyo kuna suala la uncertainty. Ndiyo maana hata Mtera na Kihansi hazikukuwa suluhisho Kwa mahitaji ya umeme nchini kama tulivyoahidiwa nyakati zile

3. Umeme cheap kuliko wote duniani na ambao ni environmental friendly ni solar power.

4. Tumewekeza sana kwenye gas, si vyema hizo investment zikabakia white elephants.

4. Kuna chanzo kingine change umeme mikoa ya Singida na Njombe ambacho ni nguvu ya upepo (windmill)

5. TANESCO wamewekeza tens kwenye umeme wa joto ardhi (Geothermal) kwa tafiti zilizofanyika Mbeya.

Kwa maoni yangu bila kujali sababu za wana mazingira wa Ulaya (mabeberu), uamuzi wa kuendelea na Stiglers gorge ulipaswa uzingatie upembuzi yakinifu mpya kabisa ambao unaweka vyanzo tajwa hapo juu kwenye kikapu kimoja dhidi ya Stigler's gorge.

Otherwise tutunze hii post until 2035 kama Mungu atatujalia uhai.
 
Mr.Haambiliki na wapamba wake muda ndio huwaumbua maana kamwe huwa hawasilikizi mawazo ya watu.

Mpaka sasa ameshavurunda katika mambo mengi na yote ni kutokana na yeye kupuuza ushauri na maoni ya watu.

Huyu ni mtu wa kuharibu tu na kibaya hataki kujifunza na hata kukiri kuwa anakosea.

Tuache muda utakuja kuthibitisha ni nani yuko sahihi kati ya serikali na wataalamu waliofanya Environmental Impact Assessment.
Chizi
 
Hakuna huruma yoyote! Nafikiri kuna maeneo duniani mikataba imeingiwa yasiguswe kwa sababu ya kimazingira na urithi wa dunia.
Bunge kama la ujerumani linapoteza nini sisi tukitaka tuwe na umeme wetu? We need to listern ni nini wanaona ambacho sisi hatujaona na njia mbadala ni ipi maana tunataka umeme.
Raisi yupo sahihi kutaka tuwe na umeme Ila tuchunguze pia sababu kuu haswa ni ipi mpaka bunge kama la ujerumani lijadili mambo ya nchi yetu. Tukiona ni ujinga ujinga tunawapuuza.
Tanzania ipo Duniani, ukitaka kufanya jambo litakaloathiri Dunia lazima wengine wakuangalie.
So unamaanisha wanaijua selous vyema kuliko sisi?
 
..mimi ningependa u-argue your case bila kuingiza masuala ya Soveregnity.

..nadhani hoja ya sovereugnity huwa inaibuliwa ili kufukia-fukia hoja zinazotakiwa kujibiwa kitaalamu.

..Wajerumani wametu-challenge kuhusu suala la MAZINGIRA ya Selous na bonde la mto Rufiji.

..Sasa unatakiwa uje na counter-argument za jinsi ya kudhibiti hayo madhara waliyosema yatatokea.

..Kwa upande wa Kihansi naona mambo yalifanyika vizuri. Zilitolewa sababu za kimazingira na wataalamu wakaja na mbinu za kujibu hoja na tahadhari zilizotolewa. At the end of the day tulipata mradi wa umeme, na vilevile tulitunza hao viumbe ambao walikuwa ktk hatari ya kutoweka. Everybody "won" in that case.

..Mimi ninachopendekeza ni serekali iweke wazi tahadhari za kimazingira za mradi huu. Pia tupewe alternative/options za sites nyingine zinazofaa kwa uzalishaji umeme. Na zaidi serekali ieleze hatua itakazochukua kudhibiti madhara kwa mazingira.

NB.

..bonde la mto Rufiji linagusa maisha ya WAKULIMA na WAVUVI. Je, tumefikiria mustakabali wa maisha yao?
Mimi hoja yangu kubwa ya msingi ni moja tuu, value benefits vs environmental impact, faida za mradi ni kubwa kuliko hasara ya athari za mazingira.

Kwenye mchango wangu mahali nilipangua hoja kwa hoja za WWF.
Hawa WWF wakafie mbali!, kwa sababu uamuzi kuhusu Mradi huu, umeishafikiwa, hivyo uhamasishaji wa mjadala huu ni too little too late!.

Hoja za msingi za WWF ni hizi

  1. Mradi huu utaathiri Selous Game Reserve ambayo ni moja ya World Heritage Sites hivyo ujenzi katika eneo hili utaathiri ecology ya Selous kwa kuathiri mazingira, yatakayoathiri uchumi na maisha ya watu, hoja hii inakuwa defeated na manufaa ya Mradi huo ukilinganisha na athari za Mradi huo, manufaa ni makubwa mara 1000 kuliko athari!.
  2. Eneo litakalotumika ni kilomita za mraba 1,200km2, hivyo kulifanya kuwa bwawa kubwa kuliko yote eneo la Afrika Mashariki, hivyo litakausha maziwa madogo madogo yote ya jirani, litaathiri utalii, na kukomba fertility yote ya Ardhi ya eneo hilo hadi kwenye Delta ya Rufiji Delta, hivyo kuua samaki, na kuathiri uvuvi wa Kamba samaki na kamba koche unaotegemewa ka watu 200,000 wa eneo hili, pia hoja hii inapigwa chini kwa hoja kuwa Tanzania tuna maeneo mengi ambayo ni waste land, what is km za mraba 1,200?. Hao watu 200,000 watakaothiriwa na Mradi huo ni nini ukilinganisha na Wamasai wanaishi ndani ya eneo la hifadhi ya Loliondo ambao hawaruhusiwi kulima, bali wanalishwa bure?. Kwa vile faida za Mradi ni kubwa, serikali inaweza kuwaambia watu hao 200,000 wasilime na badala yake watalishwa bure maisha yao yote, hivyo Mradi uendelee!.
  3. Mradi unaelezwa unakwenda kinyume cha mikataba ya kulinda World Heritage ambayo Tanzania tumesaini, this also is nothing!, Tanzania tumesaini mikataba kibao ya kimataifa ya haki za binaadamu na kila siku serikali inakiuka mikataba hiyo, kama rais Magufuli, ameikanyaga katiba alioapa kuilinda, what are the chances kuheshimu mikataba ya kimataifa kama itatuzuia kupata manufaa, to hell with mikataba ya kimataifa at the expense of development.
  4. Mradi huo utaazuia tani milioni 16.6 za virutubisho vya Ardhi kwa mwaka, hivyo kusababisha mmomonyoko wa Ardhi kwenye Delta ya Rufiji, hii pia sio hoja, kwa ukubwa wa ardhi ya Tanzania, shughuli za kibinaadamu kama uchimbaji wa madini, unaleta athari kubwa zaidi za kimazingira na kusababisha sio tuu mmomonyoko Mkubwa wa Ardhi, bali kutuachia mahandaki mengi na makubwa Zaidi kuliko hizo tani milioni 16.6 kwa mwaka, hivyo Mradi utaendelea!.
  5. Hoja kuwa Mradi huo utaathiri sio tuu Mbuga ya Selous, bali pia Delta ya Rufiji na Bonde la Mto Kilombero, hapa tena tunaangalia faida za Mradi na kulinganisha na athari za kimazingira, then faida za Mradi ni kubwa kuliko athari!, Mradi utaendelea!.
  6. Hawa wazungu na wana mazingira ni watu wa ajabu sana, nakumbuka walivyotucheleweshea Mradi wa Kihasi kwa ajili tuu ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwahamisha vyura hao hao kuwahifadhi nchini Marekani, kisha kuwarudisha ndipo Mradi ukapitishwa!, yaani vyura walikwamisha mradi muhimu, ujinga huu walimfanyia Nyerere na Mwinyi, lakini kwa Magufuli, watagonga mwamba!.
  7. Hata Mradi wa Kamba Samaki kwenye Delta ya Rufiji, ulikwamishwa na wanamazingira kwa hoja kuwa Mradi huo utaathiri hifadhi ya miyombo!, what is miyombo compared to manufaa ya kiuchumi?.
  8. They can just go to hell, kama katiba ya Tanzania imekanywagwa for the expense ya maendeleo, rais Magufuli aliruhusu tuachane na na hizi EIA katika kupushi Tanzania ya Viwanda, hivyo sasa hapa ni kazi tuu, hakuna cha mazingira, world heritage wala cha nini, Tanzania tunataka Umeme wa kutosha kuendeshea Tanzania ya viwanda!
Hoja zote hizo ni katika kulinda kitu kinachoitwa the sovereignty of our nationalism kwamba Tanzania ni ya Watanzania, tuna uhuru wa kupanga mambo yetu kwa manufaa yetu bila kuingiliwa na mtu mwingine yoyote, hivyo hawa WWF, wasituingilie!.

Lakini on the other hand, kiukweli kabisa japo mimi sio mchumi, lakini sera za uchumi za serikali ya Magufuli ni sera za ajabu sana!.
  1. Huu Mradi wa Umeme wa Stglers Gorge ulizungumzwa tangu Enzi za Nyerere na haukutekelezwa kutokana na hixo hizo environmental concerns na mpango wa Tanzania Power System Master Plan (2016 update), umeonyesha Mradi huu ndio the last option kama miradi mingine mikubwa itashindikana, Mradi wa priority ni Umeme wa kutumia gesi, lakini sasa Magufuli kaingia, mara ghafla hatuzungumzii tena Mradi wa Umeme wa gesi, sasa Mradi huu ndio kipaumbele!, kipaumbele for what?.
  2. Japo ni kweli, the cheapest power generation projects ni hydropower projects, lakini Tanzania hatujifunzi tuu, kutokana na global warming na mabadiliko ya tabia nchi, kuendelea kutegemea Umeme wa maji ni very unpredictable, Richmond ilisababishwa na hii over dependency on hydropower, hivyo kulipotokea ukame, kilichotukuta sote tunakijua!, sasa gesi tunayo tena ya kutosha, na Umeme wa gesi, japo ni expensive kuliko hydro ni cheap kuliko diesel generation, kwa nini tusijikite kwenye gesi yenye uhakika, tunataka kuzamisha matrilioni ya Fedha kwenye pata potea nyingine ya kutegemea mvua?.
  3. Maajabu ya uchuni wa Magufuli pia yapo kwenye kuishadadia sana hii SGR, kama tumekuwa na reli mbili ya meter gauge ya Kati na Tazara, zote zina under perform, tumeanzisha bandari kavu ya Isaka ili ipokee mizigo ya Rwanda, Burundi na DRC, lakini haifunction na reli ya kati ipo, tena hadi eneo la ICD ya Rwanda watu wanalima tuu mahindi!, hii SGR italeta miujiza gani?.
  4. Uchumi wa Tanzania unategemea kilimo, hivyo Tanzania ya kweli ya viwanda, ni Tanzania ya agro processing industries, tunahubiri Tanzania ya viwanda, bila kuinua sekta ya kilimo, hivyo viwanda ni malighafi gani ya kuendesha Tanzania ya viwanda kama sekta ya kilimo ni totally neglected, Magufuli yuko bize kununua ndege na kujenga miundombinu, what has ndege, barabara za juu kwa juu, uwanja wa ndege wa Chato, na hii SGR has to do with sekta ya kilimo?.
Mimi bado nasisititiza, Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!.

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT

Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136!

Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi?

Priorities Zetu Nini?. Dola Milioni 300 Zinatosha Kununua Smelter, Jee Tununue Au Tuzitumie Kwa Mahitaji Muhimu Zaidi?.

P
P
 
Awana jema lolote la maana kwenye kuijali Tanzania

Hakuna bara lililojitia kiherehere kwenye kupokea Kyoto Protocol kama la Europe ni wao pekeee ndio waliopokea masharti yote kama yalivyo and more katika awamu zote; Phase I, phase II and phase III za green house gas (GHG) reduction kama zilivyo pendekezwa.

Kujiongezea matatizo zaidi wakachukua na Paris Agreement kama ilivyo as a continental policy measure, matokeo yake kila nchi ndani ya EU inatakiwa kupunguza GHG emission by 40% compared to the levels of 1990 by 2030.

Sasa kama wewe ndio ujerumani uchumi wako upo based na production si changamoto hiyo maana uwezi zalisha bila ya kuchafua mazingira; kwa sasa wanatakiwa kupunguza pengine more 1000 million tonnes of CO2 emission by 2030 kutokana na sera za bara lao (na kuna target kila mwaka usipofikia fines).

Ndipo hapo unajikuta inabidi uanze unafiki wakujifanya unajali sana mazingira ya third world. Hii ni kwa sababu kutokana na makubaliano ya Kyoto protocol nchi zilizotakiwa kupunguza GHG ni zilioendelea, kwa uelewa wa kwamba nchi za third ndio kwanza zinakuwa kiuchumi na zinahitaji kuzalisha ivyo katika safari hiyo zitaongezaGHG zipewe auheni.

Makubaliano ni kwamba namna moja ya kuzisaidia nchi za third word kupunguza uchafuzi wa mazingira au kupunguza vyanzo vyenye kunyonya CO2 (kama misitu ) ni hawa mabeberu kusaidia kuleta maendeleo ya nishati kupitia technology iliyo rafiki wa mazingira.

Again sio kwa sababu wanahuruma la hasha kwenye ‘United Nations Framework Convention on Climate Change’ (UNFCCC) unaruhusiwa kusaidia third world na ukifanya hivyo unapata points ambazo zinakuruhusu wewe kuchafua kwa sababu nchi nyingine imepunguza kwa niaba yako.

Sasa ukimsaidia nchi kama Tanzania kutokata misitu unachukua point zote za hekari ambazo zinaweza kumeza CO2 na ukimkopesha kujenga mitambo ya gas unachukua point zote ambazo angetumia makaa ya mawe (hiyo system inaitwa Cap and trade) lakini ukijenga mwenyewe miradi yenye kulinda mazingira wakati wewe auna penalties zozote za uchafuzi kama wao (wasipofikia malengo kila mwaka ni fine) maana yake ujenzi wako kwao ni opportunity costs.

Ndio ujiulize kuna mtu mwenye akili timamu atakuja kuwekeza kwenye wa umeme wa upepo kwako wakati sio efficient, the answer is ni kwa sababu ina mruhusu yeye kuchafua huko alipo wakati katika kukusaidia anakukopesha na utamlipa kwake ni win-win na kwako ni loose-looose.

Jenga tu Stieglers Gorge wala atuhitaji kujielezea kwa hawa wazee mahesabu

Asante mkuu
 
Unaweza ukatuonyesha post yoyote uliyoonyesha kuwa na shaka na huu uwekezaji wa umeme wa gas wakati nchi nzima ilipokuwa inaimbishwa uchumi wa gas na wanaccm?

Tuache hilo, wakati Magufuli ameanza kutamba kwamba atajenga stiegler gorge alisema mradi huo utagharimu 3t, ila juzi wakati wa kusaini mradi huu tunaambiwa mradi ni sheria 6.5t!! Hapo hupatikana walakini?

Sijamaliza, je kama hiyo 6.5t inaweza kuleta umeme wa 2,100m, iwapo tungeacha kuharibu mazingira na kuzipeleka kwenye gas ambayo mchakato umeshaanza na bomba liko Dar, ungezalisha megawati ngapi? Itumie akili yako ipasavyo sio kulishwa uzalendo uchwara huku unapigwa.

Acha ujuha, eneo la kuzalisha umeme wa gas 2100MW umejaribu kulifikiria litakua kubwa kiasi gani? na je umefikiria hatari ya gas yenyewe ukilinganisha na maji, acha cost, acha utaalamu + figisu za kukufanya wewe usiwe na umeme wa kutosha
 
Acha ujuha, eneo la kuzalisha umeme wa gas 2100MW umejaribu kulifikiria litakua kubwa kiasi gani? na je umefikiria hatari ya gas yenyewe ukilinganisha na maji, acha cost, acha utaalamu + figisu za kukufanya wewe usiwe na umeme wa kutosha
Wanataka set up ya umeme wa gas watutengeze wao alafu hao hao watuuzie umeme!
Hydro electric power ndy inaunafuu kwetu
Syo gas

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninachojiuliza sanasana, Je wana wivu tu, ni mabeberu tu, wanataka kutukwamisha tu, majibu ninayopata kwa harakaharaka yananichanganya zaidi, WIVU, kwa sababu gani?!? maana kimaendeleo bado tuna safari ndefu sana kuwafikia na jibu si STIGLERS GORGE,MABEBERU naona hiyo siasa ilishapitwa na wakati,KUTUKWAMISHA, ili wapate nini!!! maana sioni uchumi wao kuumia kwa lolote hata kama tukijenga STIGLERS kumi na tano. Najiuliza zaidi hivi yale matrilioni ya litre za gesi kule mtwara tumepanga kuyafanyia nini?!?.hebu kama Taifa tukae chini tujiulize kwa makini tutapata nini tutakosa nini tukiamua ama kujenga bwawa ama kuacha kulijenga tuendelee kuwekeza kwenye gesi. wasomi wa nchi hii njooni hapa mtuelimishe msituache tunabishana na kurushiana vijembe wakati nchi ipo kwenye mtihani mgumu. Hivi tukikaa na wajerumani tukwaambia watujengee kinu cha kufua umeme wa Gesi MEGAWAT12000 kwa gharama zao ama angalau wachangie asilimi 80 na umeme utakaozalishwa uwe bei rahisi kwa mlaji wa mwisho wakikubali sioni haja ya kuendelea na stigilaz goji maana bado itabaki kuwa yetu miaka ijayo tunaweza kuendelea nayo tena!!!!. NG'WAMISHAGA MHOLA BAGOSHA!!
Stigler's project tutafanya na bado tutaongeza umeme wa gas mpaka tufikie 10000MW ndio tutaona ahueni. Hakuna nchi ilioendelea kwa misaada, hakunaa (By Dr. John Joseph Pombe Magufuli). Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Raisi wetu Magufuli
 
Mr.Haambiliki na wapamba wake muda ndio huwaumbua maana kamwe huwa hawasilikizi mawazo ya watu.

Mpaka sasa ameshavurunda katika mambo mengi na yote ni kutokana na yeye kupuuza ushauri na maoni ya watu.

Huyu ni mtu wa kuharibu tu na kibaya hataki kujifunza na hata kukiri kuwa anakosea.

Tuache muda utakuja kuthibitisha ni nani yuko sahihi kati ya serikali na wataalamu waliofanya Environmental Impact Assessment.
"Keyboard Warrior"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujerumani: Mradi wa umeme wa Tanzania wapigiwa kura bungeni

Bunge la Ujerumani limepitisha mswada wa kuitaka serikali ya Ujerumani itafute njia mbadala ya mradi wa Tanzania wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler ili kulinda turathi na asili.

View attachment 998487

Vyama vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani vimeitaka serikali itafute njia nyingine badala ya ile ya mradi wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler kwenye mto rufiji kusini mwa Tanzania Wabunge wa vyama vya CDU/CSU, Kijani na AFD walishiriki katika kupiga kura hiyo lakini chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD, hakikushiriki. Azimio la vyama vya CDU,CSU na SPD pia linatokana na mapendekezo ya kamati ya serikali ya Ujerumani ya ushirikiano wa kiuchumi.

Azimio lililopitishwa bungeni na vyama hiyvo vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani linaitaka serikali kuu isaidie katika masuluhisho ya kukidhi mahitaji ya nishati ya Tanzania bila ya kuathiri mazingira. Katika azimio lao vyama hivyo vimesema mradi huo mkubwa wa kuzalisha nishati ya umeme utavuruga mfumo wa mto mmojawapo mkubwa barani Afrika.

Tanzania inakusudia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia nguvu ya maji kutoka kwenye mto rufiji. Sehemu hiyo ni muhimu kwa shughuli za kilimo za wakaazi. Ikiwa mradi huo utaendelea mbele bonde la Stiegler ambalo limewekwa miongoni mwa turathi za shirika la Umoja wa mataifa la UNESCO litapoteza hadhi yake na huenda likasababisha athari kubwa katika raslimali zilizopo kwenye sehemu hiyo.
Katika ombi lao kwa serikali ya Ujerumani wabunge wa vyama vya CDU,CSU na SPD wamesema sehemu hiyo ya mbuga ya wanyama ya Selous nchini Tanzania ni eneo kubwa kabisa na kongwe la hifadhi ya wanyama pori barani Afrika.

Wabunge hao wamesema mradi huo wa bwawa la nishati utahitaji sehemu kubwa sana itakayotokana na kukatwa kwa miti na hivyo kusababisha athari kubwa katika mazingira, tabia nchi na katika uchumi.

Wabunge wa chama cha upinzani cha FDP wameshauri kujengwa kinu cha nishati kutokana na gesi kwa sababu Tanzania inayo gesi ya kutosha iliyogunduliwa hivi karibuni. Chama hicho cha upinzani cha FDP kilichopinga azimio hilo kimeitaka serikali ya Ujerumani ifanye mazungumzo na serikali ya Tanzania.

Mwandishi/Zainab Aziz/Daniel Pelz/DW Berlin

Mhariri: Yusuf Saumu

CHANZO: Ujerumani: Mradi wa umeme wa Tanzania wapigiwa kura bungeni | DW | 18.01.2019

Kulikoni Wajerumani eti watupangie matumizi ya rasimali zetu..!!
Hivi kweli,Africa unaweza kuwaambia USA,Au Ulaya,jinsi ya kupanga mambo yao ya ki uchumi?
USA ilijitoa kwenye mpango wa kupunguza hewa ya ukaa duniani,maana waliona wakijiunga na mpango huo,inabidi baadhi ya viwanda viache kufanya kazi,wakatupilia mbali hizo ishu.
Hata kwenye mambo ya sheria,wao USA ukimshitaki Askari wao,wanakuambia hawaitambui ICC.
Hao wazungu waende zao wakafie mbele,
Wasituletee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom