ZIPO hisia kuwa imefikia wakati wa kuchambua na kunyambua ni nini hasa wabunge wa Bunge linaloitwa la Taifa wawe wanazungumza wanapokuwa wanalipwa posho nono wakati wa vikao muhimu vya kitaifa.
Mtu ana haki ya kuzungumza lolote lile analotaka mahala popote hapa nchini. Lakini sivyo, au sivyo inavyotakiwa katika Bunge la Taifa. Bunge la Taifa linatakiwa lizungumzie masuala muhimu na mazito ya kiuchumi, kijamii, kitamaduni, kiteknolojia na kisiasa katika ngazi ya taifa na sio mkoa, wilaya au tarafa au jimbo eti!
Hali iliyopo hivi sasa inahitaji REDET au wajanja wengine wale kwa kulishauri NCHI juu ya mustakabali wa kile kinachostahili kufanywa na wabunge wabunge la taifa. Inavyoonekana kuna masuala ya Uwakilishi kwa vikundi vya washikadau mbalimbali-basi tuangalie wa kuwa na uwezekano wa bunge linaloweza kutumia masaa kadhaa kuzungumzia posho na maslahi ya watu. Hii sio nchi ya kijamaa tena jamani au sio au ndio? Vipi? Unashangaa? Hata wao wenyewe hawajui ni wajamaa au ni watu gani?
Sembuse iwe mimi?
Kama kuna masuala ya Kimkoa mkoa, jamani, wabunge wa mkoa husika labda mkichanganyikana na mangi meza kadhaa na wawakilishi wengine muwe na bunge lenu myazungumzie huko. Jamani ambulensi wilayani kwenu au jenereta kwenye shule wilayani kwenu hili ni jambo la kuzungumziwa na Bunge la taifa. Au kwa akili yetu hatujui kuwa MUDA ni RASILIMALI pia. Na muda tofauri na rasilimali nyingine haina salio?
Ili kuwatanabaisha na wanaobabaika katika kutofautisha lipi lizungumzwe na Bunge la Taifa na yepi yazungumzwe na Mabunge ya Mkoa au Bunge la Uwakilishi kutokana na shughuli au kazi watu wanazofanya nawapeni mifano hii hapa chini:
Mshauri sikiliza hoja hizi toka bungeni kisha tupe ushauri zinafaa mahala hapo:
HOJA 1
Spika: Mheshimiwa Mbunge wa Njaakali yeye ana maswali mawili Kwa Naibu, Naibu Waziri, karibu mheshimiwa.
Mbunge Njaakali: Hospitali ya Jimbo langu wanakula wali mara moja tu, je, Wizara husika ina mpango gani wa kuongeza siku za wali na ikiwezekana pilau na briani?
Mshauri: Hii ni hoja iliyotakiwa kutolewa katika Bunge la Mkoa [kama lingekuwepo na sio Bunge la Taifa-tena taifa la nchi mbili zisizounganika sawasawa!]
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
HOJA 2
Mbunge 1: Askari hawalipwi mishahara [kama yetu?] sasa hawa watu wanatulinda basi wapande mabasi bure!
Mbunge 2: Nauli hizi zinawatosha kabisa wenye daladala wao kazi yao ni uroho tu ndio maana wanadai zaidi.
Mbunge 3: Madaktari na manesi wanadai rushwa kwa kuwa mishahara yao ni kidunchu! Waongezewe mshahara angalau uwe nusu ya mshahara wangu!
Mbunge 4: Walimu ndio baba na mama zetu kiakili. Tusipowaangalia nani atawaangalia?
Mbunge 5: Sera ya vijana basi iboreshwe iwe hivi au vile vijana wapate ajira jamani eee! Na kina mama wawe na Baraza la Kinamama eee? Na Wazee wawe na Baraza la Wazee heee? Na watoto wawe na Jumuiya ya Watoto eeehe!
Watu wote, yaani, makundi yote wawe na mabaraza yao eeee! Maana ndio demokrasia eehhe! Sasa kila chama kikiwa na Baraza lake la hawa au wale kweli hatutaendaga upandege wa Burundi na Rwanda eee?
Mshauri: Hoja hizi ingelifaa kutolewa katika Bunge la Wawakilishi ambapo wabunge wake wangelikuwa wakichaguliwa kutokana na tarafu au kazi zao. Kungekuwa na walimu, madaktari, wanajeshi, polisi, maprofesa, wahandisi, wenye mabasi ya mikoani, wenye ndege, wenye meli na mashua, wakulima, wenye daladala, vibarua na wanaojiajiri.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
HOJA 3
Mbunge 1: Mkongo wa taifa lazima uwepo ili kuhakikisha maendeleo yetu hayakwamishwi na mitapanyo ya njia za kutoa na kupokea mawasiliano.
Mbunge 2: Mapato yanayotokana na Migodi ya madini ichangie maendeleo ya pale ilipo na ya taifa zima kwa ujumla.
Mbunge 3: Tuna uwezo wa kuwa na shule bora za msingi na sekondari hasa kwenye mikoa ya mipakani pamoja na vyuo vya taaluma mbalimbali na taasisi hizo zikavutia takriban wanafunzi 200,000 kwa mwaka kutoka nje.
Ruksa kuajiri walimu toka nje ili waongeze ubora wa elimu yetu na walimu wetu wakasome tena nje ili wapande na ikiwezekana wapate kazi nchi za nje watutumie fedha za kuwalipa hawa wa kigeni hapa nchini.
Mkitaka kufanya jambo eti sawa na nchi zingine za Kiafrika zinavyofanya basi hamna ushindani na mtaishia papo hapo wanapoishia wao kama sio chini zaidi!
Mbunge 4: Ndugu Waziri wa Afya kama hospitali zako zikiendeshwa vyema nina hakika zaidi ya kupokea Wakomoro na Washelishlei hata na sisi tutaweza kutibiwa papa hapa nchini.
La muhimu ni kuhakikisha tunajipinda tutengeneze mashine zetu wenyewe na kuajiri madaktari wanaolipwa vyema toka ndani na nchi ya nje. Hili halina tofauti na kuwekeza maana mawaziri na wabunge toka nchi nyingine za Kiafrika watakaokuja kutibiwa hapa watalipa kiasi cha kutosha kurudisha gharama zote za uwekezaji. Tufungueni macho jamani haya ndio majibu sahihi kwa utandawazi.
Mshauri: Wallahi, hizi ni hoja
za kitaifa kwa hiyo zinafaa kuwepo kwenye bunge la Taifa na sio mabunge ya mikoa au yale ya uwakilishi.
Wenye akili watanielewa, wababaishaji katu hawatakaa wanielewe! Wana-jamii nanyi toeni HOJA ZENU. NAOMBA KUTOA HOJA!
Mtu ana haki ya kuzungumza lolote lile analotaka mahala popote hapa nchini. Lakini sivyo, au sivyo inavyotakiwa katika Bunge la Taifa. Bunge la Taifa linatakiwa lizungumzie masuala muhimu na mazito ya kiuchumi, kijamii, kitamaduni, kiteknolojia na kisiasa katika ngazi ya taifa na sio mkoa, wilaya au tarafa au jimbo eti!
Hali iliyopo hivi sasa inahitaji REDET au wajanja wengine wale kwa kulishauri NCHI juu ya mustakabali wa kile kinachostahili kufanywa na wabunge wabunge la taifa. Inavyoonekana kuna masuala ya Uwakilishi kwa vikundi vya washikadau mbalimbali-basi tuangalie wa kuwa na uwezekano wa bunge linaloweza kutumia masaa kadhaa kuzungumzia posho na maslahi ya watu. Hii sio nchi ya kijamaa tena jamani au sio au ndio? Vipi? Unashangaa? Hata wao wenyewe hawajui ni wajamaa au ni watu gani?
Sembuse iwe mimi?
Kama kuna masuala ya Kimkoa mkoa, jamani, wabunge wa mkoa husika labda mkichanganyikana na mangi meza kadhaa na wawakilishi wengine muwe na bunge lenu myazungumzie huko. Jamani ambulensi wilayani kwenu au jenereta kwenye shule wilayani kwenu hili ni jambo la kuzungumziwa na Bunge la taifa. Au kwa akili yetu hatujui kuwa MUDA ni RASILIMALI pia. Na muda tofauri na rasilimali nyingine haina salio?
Ili kuwatanabaisha na wanaobabaika katika kutofautisha lipi lizungumzwe na Bunge la Taifa na yepi yazungumzwe na Mabunge ya Mkoa au Bunge la Uwakilishi kutokana na shughuli au kazi watu wanazofanya nawapeni mifano hii hapa chini:
Mshauri sikiliza hoja hizi toka bungeni kisha tupe ushauri zinafaa mahala hapo:
HOJA 1
Spika: Mheshimiwa Mbunge wa Njaakali yeye ana maswali mawili Kwa Naibu, Naibu Waziri, karibu mheshimiwa.
Mbunge Njaakali: Hospitali ya Jimbo langu wanakula wali mara moja tu, je, Wizara husika ina mpango gani wa kuongeza siku za wali na ikiwezekana pilau na briani?
Mshauri: Hii ni hoja iliyotakiwa kutolewa katika Bunge la Mkoa [kama lingekuwepo na sio Bunge la Taifa-tena taifa la nchi mbili zisizounganika sawasawa!]
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
HOJA 2
Mbunge 1: Askari hawalipwi mishahara [kama yetu?] sasa hawa watu wanatulinda basi wapande mabasi bure!
Mbunge 2: Nauli hizi zinawatosha kabisa wenye daladala wao kazi yao ni uroho tu ndio maana wanadai zaidi.
Mbunge 3: Madaktari na manesi wanadai rushwa kwa kuwa mishahara yao ni kidunchu! Waongezewe mshahara angalau uwe nusu ya mshahara wangu!
Mbunge 4: Walimu ndio baba na mama zetu kiakili. Tusipowaangalia nani atawaangalia?
Mbunge 5: Sera ya vijana basi iboreshwe iwe hivi au vile vijana wapate ajira jamani eee! Na kina mama wawe na Baraza la Kinamama eee? Na Wazee wawe na Baraza la Wazee heee? Na watoto wawe na Jumuiya ya Watoto eeehe!
Watu wote, yaani, makundi yote wawe na mabaraza yao eeee! Maana ndio demokrasia eehhe! Sasa kila chama kikiwa na Baraza lake la hawa au wale kweli hatutaendaga upandege wa Burundi na Rwanda eee?
Mshauri: Hoja hizi ingelifaa kutolewa katika Bunge la Wawakilishi ambapo wabunge wake wangelikuwa wakichaguliwa kutokana na tarafu au kazi zao. Kungekuwa na walimu, madaktari, wanajeshi, polisi, maprofesa, wahandisi, wenye mabasi ya mikoani, wenye ndege, wenye meli na mashua, wakulima, wenye daladala, vibarua na wanaojiajiri.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
HOJA 3
Mbunge 1: Mkongo wa taifa lazima uwepo ili kuhakikisha maendeleo yetu hayakwamishwi na mitapanyo ya njia za kutoa na kupokea mawasiliano.
Mbunge 2: Mapato yanayotokana na Migodi ya madini ichangie maendeleo ya pale ilipo na ya taifa zima kwa ujumla.
Mbunge 3: Tuna uwezo wa kuwa na shule bora za msingi na sekondari hasa kwenye mikoa ya mipakani pamoja na vyuo vya taaluma mbalimbali na taasisi hizo zikavutia takriban wanafunzi 200,000 kwa mwaka kutoka nje.
Ruksa kuajiri walimu toka nje ili waongeze ubora wa elimu yetu na walimu wetu wakasome tena nje ili wapande na ikiwezekana wapate kazi nchi za nje watutumie fedha za kuwalipa hawa wa kigeni hapa nchini.
Mkitaka kufanya jambo eti sawa na nchi zingine za Kiafrika zinavyofanya basi hamna ushindani na mtaishia papo hapo wanapoishia wao kama sio chini zaidi!
Mbunge 4: Ndugu Waziri wa Afya kama hospitali zako zikiendeshwa vyema nina hakika zaidi ya kupokea Wakomoro na Washelishlei hata na sisi tutaweza kutibiwa papa hapa nchini.
La muhimu ni kuhakikisha tunajipinda tutengeneze mashine zetu wenyewe na kuajiri madaktari wanaolipwa vyema toka ndani na nchi ya nje. Hili halina tofauti na kuwekeza maana mawaziri na wabunge toka nchi nyingine za Kiafrika watakaokuja kutibiwa hapa watalipa kiasi cha kutosha kurudisha gharama zote za uwekezaji. Tufungueni macho jamani haya ndio majibu sahihi kwa utandawazi.
Mshauri: Wallahi, hizi ni hoja
za kitaifa kwa hiyo zinafaa kuwepo kwenye bunge la Taifa na sio mabunge ya mikoa au yale ya uwakilishi.
Wenye akili watanielewa, wababaishaji katu hawatakaa wanielewe! Wana-jamii nanyi toeni HOJA ZENU. NAOMBA KUTOA HOJA!