Bunge la Marekani lapitisha sheria kumbana Trump kupigana vita na Iran bila ridhaa yake

Hawa binadamu wanaojiita Wamarekani wana akili za ajabu sana sijapata kuona. Kinachochekesha ni kwamba hiyo sheria ni ya njia moja tu (One way operation) na wala haiwezi kumzuia Iran asishambuliwe.

Mchezo uko hivi: Hiyo sheria inamzuia Marekani asifanye shambulio dhidi ya Iran (Offensive Warfare) lakini haimnyang'anyi Marekani haki yake ya kujilindi kipindi atakposhambuliwa na Iran au atakapohisi kwamba anashambuliwa na Iran (Right to self-defense) ambayo iko kwenye Ibara ya 51 ya Hati Idhini ya Umoja wa Mataifa (United Nations).

Upande mwingine hii sheria imemgusa Marekani tu lakini haijawagusa washirika wake wa kimkakati (Strategic Partners) ambao wanaweza kusababisha songombingo na Iran na kumlazimisha Marekani aingie kwenye mgogoro.

Hivi leo unadhani Israel au Saudi Arabia wakianzisha songombingo na Iran, unadhani Marekani ataacha kuingilia kweli ?? Lazima ataingilia na akiingilia lazima ile kwake, vivyo hivyo asipoingilia lazima ile kwake. Democrats na Republicans wote ni maswahiba wakubwa wa Israel.........

Naomba nikupe mfano hai kabisa: Mwaka 1914 kuelekea 1916 Wamarekani walikataa katakata kujihusisha na vita ya kwanza ya dunia na walifanya hivihivi. Lakini waliingia kwenye ile vita chini ya mgongo wa kujilinda dhidi ya Uvamizi wa Mexico na Ujerumani. Soma kuhusu The Zimmerman Telegram.

Mfano mwingine ni kwamba Security Commitments ambazo zimejengwa kupitia mifumo ya kujihami inalifanya bunge la Marekani lisiwe na maana yoyote ile. Mfano Ibara ya 5 ya NATO inasema kwamba akivamiwa mwanachama moja basi wote wanaingia vitani. Hapa bunge halihusiki kabisa.

Sasa mkataba wa Marekani na Israel sijui unasemaje kuhusu ulinzi lakini kama Bunge linautambua basi kama Israel atalianzisha na Iran moja kwa moja Marekani lazima ataingia vitani tu.....

Hakuna ambiguity wala cha ajabu hapo, Congress hata siku moja haiwezi kuweka zuio dhidi ya Self Defense!
Hata Sisi Tanzania na ubovu wa katiba yetu lakini bado inamnyima haki hata raisi wa nchi kuwazuia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupambana na adui aliyeikalia nchi yetu kimabavu,na inamnyima mtu yeyeote kusaini mkataba wa kukubali nchi hii kushindwa vita au kuitoa Jamhuri ya Muungano kwa adui SEMBUSE CONGRESS?

Walichokifanya ni cha kawaida tu lakini chenye manufaa kwa nchi yao, mambo ambayo allies watafanya wakafanye wao, kama Marekani akitaka kuingia basi itabidi arudi kwa congress waidhinishe
 
Hakuna ambiguity wala cha ajabu hapo, Congress hata siku moja haiwezi kuweka zuio dhidi ya Self Defense!
Hata Sisi Tanzania na ubovu wa katiba yetu lakini bado inamnyima haki hata raisi wa nchi kuwazuia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupambana na adui aliyeikalia nchi yetu kimabavu,na inamnyima mtu yeyeote kusaini mkataba wa kukubali nchi hii kushindwa vita au kuitoa Jamhuri ya Muungano kwa adui SEMBUSE CONGRESS?

Walichokifanya ni cha kawaida tu lakini chenye manufaa kwa nchi yao, mambo ambayo allies watafanya wakafanye wao, kama Marekani akitaka kuingia basi itabidi arudi kwa congress waidhinishe

Hebu twenda taratibu bwana:
Mosi, huu uliopitishwa hapa ni muswada (A bill) na siyo sheria (A legislation). Hivyo wewe unadhani kwa akili ya Wamarekani watakubali huu muswada uwe sheria ?? Kwamba wanaiogopa sana Iran, na kwa lipi labda ?? Vipi kuhusu kura turufu ya Raisi wa Marekani ??

Pili, unaposema hakuna utata una maana gani labda, maana natumaini wewe utakuwa siyo mgeni na falsafa ya Ulinzi wa kujihami (Self-Defense) ya nchi ya Marekani. Wao wanaamini hadi kujihami ili kuzuia shambulio (Pre-emptive strike/Anticipatory Self-Defense) kama walivyofanya kule Iraq mwaka 2003.

Kwenye sheria zao kuna kesi inaitwa The Caroline's Case ya mwaka 1837 ambayo imeweka wazi kabisa falsafa ya kujihami ya Marekani inaruhusu Pre-emptive Strike/Anticipatory Self-Defense. Wewe utasemaje hichi ni kitu cha kawaida ??

Leo Raisi Trump akisema anafanya Self-Defense through A Pre-emptive Strike kwasababu nchi iko hatarini unadhani hilo bunge litamzuia ?? Bado huoni kwamba wanachokiamini hawa mabwana ni maajabu ya dunia tu ??

Tuanzie hapa kwanza: Naomba nieleweshwe.......
 
Hebu twenda taratibu bwana:
Mosi, huu uliopitishwa hapa ni muswada (A bill) na siyo sheria (A legislation). Hivyo wewe unadhani kwa akili ya Wamarekani watakubali huu muswada uwe sheria ?? Kwamba wanaiogopa sana Iran ?? Vipi kuhusu kura turufu ya Raisi wa Marekani ??

Pili, unaposema hakuna utata una maana gani labda, maana natumaini wewe utakuwa siyo mgeni na falsafa ya Ulinzi wa kujihami (Self-Defense) nchini Marekani. Wao wanaamini hadi kujihami ili kuzuia shambulio (Pre-emptive strike) kama walivyofanya kule Iraq mwaka 2003, kwenye sheria zao kuna kesi inaitwa The Caroline's Case ambayo imeweka wazi kabisa falsafa ya kujihami ya Marekani.

Sasa Raisi Trump akisema anafanya Self-Defense through A Pre-emptive Strike kwasababu nchi iko hatarini unadhani hilo bunge litamzuia ?? Bado huoni kwamba wanachokiamini hawa mabwana ni maajabu tu ??

Tuanzie hapa kwanza: Naomba nieleweshwe.......

Ipo sheria kule marekani inampa raisi window wa kuamuru mashambulizi kadha wa kadha bila kupitia congress kwa mfano Bill clinton aliitumia alipopiga kiwanda cha dawa Sudan au Obama aliposhiriki kusapoti vita ya NATO Libya, Lakini inapokua large Scale war ambayo itatumia Matrilion ya Dollar, ambayo Askari maelfu ya Wamarekani wanawekwa kwenye risk ya kifo na ambayo kuna uwezekano wa kutumia miaka na miaka, lazima President apate authorization na hii bill inakazia hilo ili Trump asije akajifanya kumanouvre kujidai anainvoke ile sheria niliyoitaja awali!.

HataTrump anajua,kuipiga Iran siyo operesheni ya upiga site mbili tatu halafu ukadhani umemaliza kazi, Kuipiga Irani ni lazima iwe full fledged war tena ikibidi kufanya regime change, ukiwaacha Maayatollah kwenye mamlaka ni kazi bure. Sasa vita ya hivyo siyo lelemama kwa taifa lenye nguvu kama Iran
 
Ipo sheria kule marekani inampa raisi window wa kuamuru mashambulizi kadha wa kadha bila kupitia congress kwa mfano Bill clinton aliitumia alipopiga kiwanda cha dawa Sudan au Obama aliposhiriki kusapoti vita ya NATO Libya, Lakini inapokua large Scale war ambayo itatumia Matrilion ya Dollar, ambayo Askari maelfu ya Wamarekani wanawekwa kwenye risk ya kifo na ambayo kuna uwezekano wa kutumia miaka na miaka, lazima President apate authorization na hii bill inakazia hilo ili Trump asije akajifanya kumanouvre kujidai anainvoke ile sheria niliyoitaja awali!.

HataTrump anajua,kuipiga Iran siyo operesheni ya upiga site mbili tatu halafu ukadhani umemaliza kazi, Kuipiga Irani ni lazima iwe full fledged war tena ikibidi kufanya regime change, ukiwaacha Maayatollah kwenye mamlaka ni kazi bure. Sasa vita ya hivyo siyo lelemama kwa taifa lenye nguvu kama Iran
Hujajibu swali, unachofanya ni kuzunguka mbuyu. Halafu naomba tukubaliane kwanza kwamba hii unayoisema kuwa ni sheria (A legislation) siyo sheria bali ni Muswada (A Bill) ambao unategemewa kupitishwa: Hivyo unaweza pitishwa au usipitishwe.

Narudi kwenye hoja yangu: The War Powers Act ya 1973 inatoa masharti mawili ili Marekani ipigane vita. Sharti la kwanza ili Raisi atume vikosi nje ya nchi ni lazima alitaarifu Bunge masaa 48 kabla. Ile sheria ya mwaka 2001 ilimrahisishia Raisi wa Marekani kadhia ya kwenda kila saa bungeni maana nchi ilikuwa iko vitani na magaidi.

Sharti la pili, linampa Raisi wa Marekani mwanya wa kupigana vita wakati wa dharura bila ruhusa ya Bunge la Marekani pindi Marekani yenyewe, Majimbo yake ya nje au Vikosi vyake vya kijeshi vilivyo ndani au nje ya nchi vitashambuliwa. Hapa ndipo tatizo langu mimi linapoanzia:

Hivi Marekani ana vikosi vingapi nje ya mipaka yake hasa kule Mashariki ya kati ?? Afghanistani tu anakopakana na Iran ana wanajeshi siyo chini ya 14000.

And hypothetically speaking, leo hii huo muswada upitishwe halafu vikosi vya Marekani vishambuliwa kule Mashariki ya kati unadhani Donald Trump ataenda tena kwenye bunge wakati anaruhusiwa kisheria kutofanya hivyo ?? Nini kitamzuia kutumia hati ya dharura ili kulikwepa Bunge na kuwatangazia vita Iran ??

Wewe huoni kwamba haya ni maajabu ya dunia na hawa wabunge wanajisumbua kupaka rangi upepo ??
 
Kilichopitishwa na The House ni 'muswada' ambao huenda ukampa zuio Rais Trump kufanya maamuzi ya uvamizi wa kijeshi kwa Irani mpaka kwa ridhaa ya Congress ya Marekani.

Lakini kuna Exception katika huo muswada ambapo haumzuii Trump kufanya maamuzi ya kuingia vitani kama Self Defence katika nyakati za dharura hasa pale ambapo nchi, milki zake ama U.S. Armed Forces (ndani na nje ya nchi) ziko Under Attack.

Lakini mpaka hapo bado kuna uwezekano kwa Trump kuingia vitani kwa kigezo hicho hicho cha Self Defence kama watangulizi wake walipokuwa wakitumia kigezo cha ile Sheria ya 2001 baada ya September 11 ya Authorization for Use of Military Force (AUMF) na ndio maana The House walipigia kura kuing'oa hii sheria mwezi jana lakini ikashindikana.

Tuendelee kusubiri matokeo ya huo muswada.
 
Kama nimesoma vizuri kuna sehemu wanasema hawako tayari kuruhusu serikali yao inaingiza taifa lao ktk "long decade war" bila idhini ya congress.

Ina maana wanajua Iran sio nyanya, wakianza vita itachukua zaidi ya muongo mmoja na kulitia taifa lao hasara kubwa.
Kabisa. Wanajua kwamba haitakua vita ya kitoto na itachukua muda mrefu na gharama kubwa. Hivo wamembana hivo ili akiomba ifhini kwao wakatae.
 
Haha haha haha haha

Ina maana hizi ndege F35 na F22 zime kuwa kwerea au kunguru weusi...
Mkuu baada ya Yule Mwanga (mchawi)
RQ-4 Global Hawk kupigwa pigo moja tu!
Pameacha maswali mengi sana juu ya hatima ya hao F-35 na ndege wengine! Mahesabu yamekuwa magum Sana!
Labda wa mtafute jiwe maana alisha onyeshaga dalili za kujuwa kufanya mahesabu magum! Baada ya kufanya hesabu na kujuwa hesabu ya samaki watao taga na vifaranga watakao anguliwa! Na wanao tarajiwa KUJAMIANA kwenye kina kirefu cha maji!
 
Ha ha ha aa nimeipenda hii.
Moscow blamed for disruption of GPS systems at Ben Gurion Airport
Israeli officials say interference caused by Russian military in Syria; una badilishiwa locations unajikuta badala ya kutuwa Dar unatuwa International Airport of Democratic National of CHATO inabidi ukaangaliye wanyama tu Sasa utafanyaje!
 
Iran Hana uwezo wa kucheza na vikwazo vya Marekani. Vikwazo vya kiuchumi vya Marekani vimeathiri uchumi wa nchi nyingi Duniani. Urusi imeteteleka kiuchumi baada ya vikwazo vya Rais Barack Obama kupitisha. Ukumbuke Urusi ndio nchi ya pili kivita, ndio nchi kubwa kuliko zote duniani , Urusi ndio nchi yenye rasilimali yaani natural resources kuliko nchi nyingine yeyote ile duniani , ukumbuke Urusi ilikuwa nchi ya 8 Kwa uchumi duniani baada ya vikwazo ikateremka mpaka ya 12. Tuje Venezuela kumbuka miaka ya nyuma Venezuela ilikuepo G20 Ila sasa imepotea Duniani, Kumbuka Venezuela ndio inaongoza kwa kuwa na mafuta mengi zaidi kuliko nchi zote duniani kupitia hata zile za Mashariki ya Kati. Kumbuka uchumi wa Marekani ni mkubwa kuzidi nchi zote za Ulaya zikiungana, zikiungana Ulaya ndio zinakuwa nchi za pili kwa uchumi duniani, uchumi wa Marekani ni mkubwa kuzidi nchi zote za kiislam au kiarabu zikiungana, uchumi wa Marekani ni mkubwa. Nchi za Afrika ndio nasikini hata uingereza ina uchumi mkubwa kuzidi ule wa nchi za Afrika zikiungana. Marekani ndio biggest market na consumer wa vitu vingi duniani mfano mafuta ndio mnunuzi mkubwa. Vikwazo vya Marekani vinayumbisha uchumi wa Iran . Vikwazo vikiendelea Iran lazima itetereke na kupoteza uchumi inaoushikilia sasa ambao umeshaanza kuporomoka. Iran haijawahi kuwekewa vikwazo vikubwa kama vya Trump katika historia yake. Iran akitegemea Ulaya itamsapoti aendelee kuuza mafuta imeshindikana. Kila siku analia na kutishia ataongeza urutubishaji wa uranium. Hata hiyo technology ya uranium Iran aliuziwa na Marekani. Iran anaisoma namba . North Korea vikwazo vimeifanya iwe masikini kabisa, kumbuka Zimbabwe ilikuwa miongoni mwa top 5 richest countries in Africa Leo iko wapi. Marekani bado ni superpower. Marekani is superpower labda ujio wa Mchina ni challenge kubwa Kwa US lakini gap la uchumi na China ni kubwa Marekani ipo mbali zaidi kiuchumi kuzidi China
Tukiachana na hilo bunge la Us kupitisha sheria hio ukweli mchungu Iran wako sawa haswaaa, na wamejipanga kabisa, alaf kitu kinachowaogopesha zaidi hao wabunge wa Us ni kuwa hawajui Iran itajibu kivipi, maana vitisho vya maneno tu vya Iran vimeshusha petrol dollars thamani, kiukweli Dunia ya sasa ukiwa na silaha hatari, alaf anga lako ukijua kulifunga hautoguswa na nchi yyte mpaka Dunia itamaliza, kubwa utakachofanyiwa ni vikwazo, na vikwazo ukijua kucheza navyo ndio unawamaliza kabisa aaa, Hongera sana Iran
 
The House of Representatives has adopted the 2020 military spending bill, but with an amendment that blocks war on Iran without congressional approval – backed by President Donald Trump’s outspoken critics and supporters alike.
A bipartisan amendment to bar the executive branch from offensive action against Iran without explicit authorization from Congress was adopted with a 250-170 vote, with 27 Republicans joining the Democrats in support, and seven Democrats crossing the aisle in opposition.

The amendment was proposed by otherwise unlikely allies: Rep. Ro Khanna (D-California) of the Progressive Caucus, and Rep. Matt Gaetz (R-Florida) of the Freedom Caucus, one of the most prominent Trump supporters in the House.

“What Ro and I are proposing is not to lay our arms down and make victims or targets out of our service members,” Gaetz told Fox News prior to the vote, flanked by Khanna. “We do not believe that any president should be able to lurch into a decades-long war in the absence of approval by Congress.”



Waamerika wanajitambua, kwani hii ndiyo njia bora ya kuwabana viongozi wehu wasijeleta madhara kwa nchi kutokana na maamuzi yao ya hovyo.
 
Mfano mwingine ni kwamba Security Commitments ambazo zimejengwa kupitia mifumo ya kujihami inalifanya bunge la Marekani lisiwe na maana yoyote ile. Mfano Ibara ya 5 ya NATO inasema kwamba akivamiwa mwanachama moja basi wote wanaingia vitani. Hapa bunge halihusiki kabisa.
Asante sana Mkuu kwa ufafanuzi. Lakini mara kadhaa nimesikia viongozi wa Marekani wanasema sheria za nchi yao ziko juu ya sheria zote ulimwenguni(exceptional)...ikiwemo na zile zinazowekwa na UN...sasa kama hao jamaa wanaamini hivyo...unadhani wanajari sana habari za NATO?
 
Asante sana Mkuu kwa ufafanuzi. Lakini mara kadhaa nimesikia viongozi wa Marekani wanasema sheria za nchi yao ziko juu ya sheria zote ulimwenguni(exceptional)...ikiwemo na zile zinazowekwa na UN...sasa kama hao jamaa wanaamini hivyo...unadhani wanajari sana habari za NATO?
In Law (De jure) hakuna taifa lililo juu ya sheria hapa duniani: In Fact (De facto) mataifa makubwa na yenye nguvu yako juu ya sheria. Hapa tunarudi kwenye ule msemo wa George Orwell kwenye The Animal Farm kwamba "All animals are equal but some are more equal than the others"

Mataifa makubwa huwa hufuata sheria za kimataifa pale ambapo yanaona kwamba yananufaika. Hili siyo kwa Marekani tu, hata siku Uchina akija kuwa ndiyo namba moja kuna mambo hatayafuata kabisa..
 
Tukiachana na hilo bunge la Us kupitisha sheria hio ukweli mchungu Iran wako sawa haswaaa, na wamejipanga kabisa, alaf kitu kinachowaogopesha zaidi hao wabunge wa Us ni kuwa hawajui Iran itajibu kivipi, maana vitisho vya maneno tu vya Iran vimeshusha petrol dollars thamani, kiukweli Dunia ya sasa ukiwa na silaha hatari, alaf anga lako ukijua kulifunga hautoguswa na nchi yyte mpaka Dunia itamaliza, kubwa utakachofanyiwa ni vikwazo, na vikwazo ukijua kucheza navyo ndio unawamaliza kabisa aaa, Hongera sana Iran
Kweli mkuu Kwa hali ilivyo Siku hizi hauhitaji kuwa na nuclear kujilinda ni Air defense system Bora kama S300,S400,S500 nk.
 
Hawa binadamu wanaojiita Wamarekani wana akili za ajabu sana sijapata kuona. Kinachochekesha ni kwamba hiyo sheria ni ya njia moja tu (One way operation) na wala haiwezi kumzuia Iran asishambuliwe.

Mchezo uko hivi: Hiyo sheria inamzuia Marekani asifanye shambulio dhidi ya Iran (Offensive Warfare) lakini haimnyang'anyi Marekani haki yake ya kujilindi kipindi atakposhambuliwa na Iran au atakapohisi kwamba anashambuliwa na Iran (Right to self-defense) ambayo iko kwenye Ibara ya 51 ya Hati Idhini ya Umoja wa Mataifa (United Nations).

Upande mwingine hii sheria imemgusa Marekani tu lakini haijawagusa washirika wake wa kimkakati (Strategic Partners) ambao wanaweza kusababisha songombingo na Iran na kumlazimisha Marekani aingie kwenye mgogoro.

Hivi leo unadhani Israel au Saudi Arabia wakianzisha songombingo na Iran, unadhani Marekani ataacha kuingilia kweli ?? Lazima ataingilia na akiingilia lazima ile kwake, vivyo hivyo asipoingilia lazima ile kwake. Democrats na Republicans wote ni maswahiba wakubwa wa Israel.........

Naomba nikupe mfano hai kabisa: Mwaka 1914 kuelekea 1916 Wamarekani walikataa katakata kujihusisha na vita ya kwanza ya dunia na walifanya hivihivi. Lakini waliingia kwenye ile vita chini ya mgongo wa kujilinda dhidi ya Uvamizi wa Mexico na Ujerumani. Soma kuhusu The Zimmerman Telegram.

Mfano mwingine ni kwamba Security Commitments ambazo zimejengwa kupitia mifumo ya kujihami inalifanya bunge la Marekani lisiwe na maana yoyote ile. Mfano Ibara ya 5 ya NATO inasema kwamba akivamiwa mwanachama moja basi wote wanaingia vitani. Hapa bunge halihusiki kabisa.

Sasa mkataba wa Marekani na Israel sijui unasemaje kuhusu ulinzi lakini kama Bunge linautambua basi kama Israel atalianzisha na Iran moja kwa moja Marekani lazima ataingia vitani tu.....

NB: Yote tisa, hii sheria bado haijapita, na sidhani kama itapita kwasababu kumbana Raisi wa Marekani siyo rahisi maana ana VETO Power ya kuipinga. Iran asifanye makosa ya kuwaamini wazungu, itakula kwake. Hawa binadamu wenye macho ya bluu a nywele za khaki siyo wema kabisa.
Iran haina time nao wala haiitaji huruma ya mtu wao wacha wajitekenye wacheke wenyewe Iran inachofanya ni kuwa tayari kwa lolote na kuwa tayari kuilinda nchi yao that's all
 
Kwa kifungu gani cha sheria ya US inasema ivyo?? Usjekua unaongea nchi ya jiwe ww?? Maana jiwe anaweza kujiamulia vyovyote vile anavyojiskia bila ya kufata katiba ya nchi, ilimradi jecha atangaze fisi

Rejea George Bush aliivamia Iraq bila Congress approval, google it utaona hiyo habari.
 
The House of Representatives has adopted the 2020 military spending bill, but with an amendment that blocks war on Iran without congressional approval – backed by President Donald Trump’s outspoken critics and supporters alike.
A bipartisan amendment to bar the executive branch from offensive action against Iran without explicit authorization from Congress was adopted with a 250-170 vote, with 27 Republicans joining the Democrats in support, and seven Democrats crossing the aisle in opposition.

The amendment was proposed by otherwise unlikely allies: Rep. Ro Khanna (D-California) of the Progressive Caucus, and Rep. Matt Gaetz (R-Florida) of the Freedom Caucus, one of the most prominent Trump supporters in the House.

“What Ro and I are proposing is not to lay our arms down and make victims or targets out of our service members,” Gaetz told Fox News prior to the vote, flanked by Khanna. “We do not believe that any president should be able to lurch into a decades-long war in the absence of approval by Congress.”

Ila rais ana option nyengne yakuingia vitan bila bunge ila mpaka hapa inaonesha how jmaaa wanamuhofia sanaaa tehran
 
Tukiachana na hilo bunge la Us kupitisha sheria hio ukweli mchungu Iran wako sawa haswaaa, na wamejipanga kabisa, alaf kitu kinachowaogopesha zaidi hao wabunge wa Us ni kuwa hawajui Iran itajibu kivipi, maana vitisho vya maneno tu vya Iran vimeshusha petrol dollars thamani, kiukweli Dunia ya sasa ukiwa na silaha hatari, alaf anga lako ukijua kulifunga hautoguswa na nchi yyte mpaka Dunia itamaliza, kubwa utakachofanyiwa ni vikwazo, na vikwazo ukijua kucheza navyo ndio unawamaliza kabisa aaa, Hongera sana Iran
Braza agisa kinywaji chochote kisicho nakilevi ukunyweee
 
Back
Top Bottom