Bunge la JMT halijavunjwa tayari kihoro kimeshawapata je likivunjwa?

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Sitaki kumumunya maneno naweka wazi kabisa hawa wabunge wa Chadema wamekumbwa na kihoro.
Hii ni kwa sababu 96% hawatarudi bungeni.
Walitaka kutuaminisha kuwa hali ni mbaya sana ya maabukizi ya Covid-19. Baada ya bahati mbaya wabunge watatu kufariki kwa magonjwa mengine .Na wao walidhani huu utakuwa mtaji wa kisiasa kwao na Mwenyekiti wa chama chao ambae ni Mbunge pia.
Lakini ukweli ni kwamba wameshajua wengi wao hawatarudi mjengoni sababu hawkusoma alama za nyakati. Maana walikuwa wamezoe zile siasa za kuendeaha mapambano na serikali iliyopo madarakani. Kwa miaka mitano yote wamepoteza muda wao wakishinda mahakamani badala ya kuwahudumia wapiga kura wao.
Sasa imebaki miezi miwili bunge livunjwe na kihoro kimewashika wanatapatapa hovyo.
Na muda nao unakimbia na tar 31 june bunge linavunjwa mbaya zaidi spika amewaumbua kuwa wengi wao wana madeni sababu walikuwa wanakichangia chama chao.
Ushauri wangu huko walipo karantini waanze kutumia valium ili waweze kupata usingizi maana sidhani kama wanapata usingizi maana kila mbinu wanayoitumia inakwama. Bora hao wawili ambao wameendelea kutimba bungeni na kuwaumbua.
 
Wanaotuhimiza tuendelee kuchapa kazi wao wanachapa kazi kutokea nyumbani, tena nyumbani walikozaliwa na watakakozikwa.

Haya. Tuendelee kuchapa kazi tu.
 
Back
Top Bottom