Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sasa linatawala nchi

President Elect

JF-Expert Member
Aug 9, 2011
693
212
Baada ya Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuchukua maamuzi magumu, hususan dhidi ya vitendo dhahiri vya ubadhirifu na uporaji wa raslimali za nchi yetu, hatimaye bunge letu tukufu limeanza kushika hatamu za utawala.

Leo asubuhi, naibu spika ameitisha kikao cha kamati ya uongozi ya bunge, ili kuamua juu ya hoja ya kusitisha shughuli za serikali bungeni.

Serikali ijirekebishe haraka, la sivyo itaanguka polepole!

Kashfa ya D. Jairo inahusika, bunge limedhalilishwa sana!
 
kontena 2 za meno ya tembo zakamatwa zanzibar zikiwa kwenye magunia ya dagaa.kweli serikali hakuna
 
Zainabu Vullu: Luhanjo amekiuka katiba.

Ole Sendeka: Luhanjo ameingilia uhuru wa bunge. Iundwe kamati teule ya bunge kuchunguza ya Jairo na Luhanjo.

Naibu spika ameridhia! Haiwezekani Luhanjo amdharau Waziri mkuu na bunge likae kimya!
 
Mambo Ya Bungeni yanaleta matumaini. Bwana Luhanjo naye pamoja na kujisifia uzoefu wa utendaji kazini, Inasikitisha kwa kulikoroga. Tuwape jina gani hawa ? inaumaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Ndugai, ndugu yangu yuko hoi: alipelekewa vimemo tisa ndani ya dakika nne. Alisoma kimoja tu akaendelea na hoja zake kuhitimisha hoja ya Zitto na Sendeka: SASA AMEITWA PEMBENI KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI HAIJAANZA HADI SASA..... Sijui kama atalala leo.
 
Dhana ya utawala bora imekiukwa kwa kiasi kikubwa sana.
.

Imekiukwa vipi MKUU,! bunge lilikubali serikali ichunguze, majibu ya uchunguzi yanatoka wewe unasema siyo utawala bora?!, kama hawakutaka majibu ya nje ya bunge kwanini walitaka vyombo kusiaka vichunguze?!, BTW, umeona hitimisho la mjadala wa hoja ya Jairo?!. Mkono ameomba mwongozo-amefungwa mdomo. Alikuwa anauliza kwamba je ni halali bunge kutoa hukumu bila kumsikiliza mtuhumiwa?!. Hapa wenye mawazo kama yako imekula kwenu .
 
N

ionavyo mimi kitendo alichokifanya Katibu Mkuu Kiongozi Bwana Philemon Luhanjo ni dharau. Ni dharau kwa Waziri Mkuu; Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni; ambaye kwa uchungu mkubwa, akiwa na dhamira safi uamuzi wake ulikuwa kumtimua kazi Bw. Jairo hata kama alikuwa na nia njema lakini nje ya utaratibu. Sote tunakumbuka sauti na maneno aliyotumia Waziri Mkuu siku ile bungeni akikiri kuwa ni kwa sababu tu mamlaka ya uteuzi ya makatibu wakuu anayo Rais. Pinda alionyeshwa kukerwa. Sote tunaamini kuwa Waziri Mkuu alipata taarifa za kiinteligensia mara baada ya kuipata taarifa ya Bw. Jairo, na kwa uamuzi wake alidhirika kuwa kuna ndivyo sivyo katika hilo. Lililotokea baada ya kukerwa huku ni hadithi nyingine. Ni dharau kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Suala hili lilianzia kwa wabunge ndani ya Bunge, hoja na udhibitisho ulikuwapo inakuwaje liishie kwa Waandishi wa Habari, na wabunge pamoja na Waziri Mkuu wasikilise maamuzi katika vyombo vya habari? Taarifa hizi zingerudishwa bungeni pale zilipoanzia. Huku ni kuonyesha kuwa chombo hiki cha kutunga sheria hakina ukakika na kinachoongelewa ndani ya bunge hilo na kuingia ndani ya hansard. Ni dharau kwa Mheshimiwa Shelukindo aliyeibua barua ya Bw. Jairo bungeni na wabunge wote waliomuunga mkono. Ni dharau ya wazi kwa wananchi wao. Ni dharau kwa wananchi ambao wanawakilishwa na wabunge. Mbwembwe alizoonyesha Katibu Mkuu Kiongozi kuwa yeye ndo mwenye dhamana ya nidhamu kwa makatibu wakuu na kumpa Bw. Jairo likizo ya malipo ilhali wananchi wakijua kuwa huyu kwa namna moja au nyingine ametumia vibaya fedha za wananchi. Wananchi wanaoshindia mlo mmoja, hakuna huduma za afya; zipo hospitali bila dawa; madarasa bila vitabu wala waalimu. Leo Wizara moja inachangisha; hata hizo milioni mita tano kwa ajili ya kupitisha bajeti. Ni dharau kwao.
 
Dah nilikuwa na hasira sana na maamuzi ya CAG na Luhanjo, sasa atleast Bunge limenifanya niwe na subira!
 
Wabunge na hasa wa CCM wajiulize ni kwanini watendaji wa serikali wanawadharau... Kama hawana jibu,basi waendelee kuzomea na kugonga meza na kupitisha miswaada ya hovyo kwa kura zao za ndiooo...!
 
Binafsi bado sijapata pa kupumulia kwa hakika!! Filamu ya jairo inaendelea, kinachofuata ni vikao vya wabunge wa magamba kupeana vitisho. Natamani niwe macho usiku na mchana mpaka siku magamba wanaondoka madarakani. Waingie wengine na sarakasi mpya...Loh!
 
Baada ya Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuchukua maamuzi magumu, hususan dhidi ya vitendo dhahiri vya ubadhirifu na uporaji wa raslimali za nchi yetu, hatimaye bunge letu tukufu limeanza kushika hatamu za utawala.

Leo asubuhi, naibu spika ameitisha kikao cha kamati ya uongozi ya bunge, ili kuamua juu ya hoja ya kusitisha shughuli za serikali bungeni.

Serikali ijirekebishe haraka, la sivyo itaanguka polepole!

Kashfa ya D. Jairo inahusika, bunge limedhalilishwa sana!

Hata hilo bunge halina chochote. Ili mradi wabunge wa magamba ndiyo wengi humo ndani usitegemee zaidi ya Ndiyooooooooooo, siyoooooooooooooooo ambazo hazina tija kwa maendeleo ya nchi hii zaidi ya kulindana, kuuza nchi kwa masilahi yao, kuendelea kuwaona watanganyika ni mazuzu.
 
Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza mheshimiwa Ndugai kwa kutumia busara kukubali hoja ya Mheshimiwa Zito na vile kukubali iundwe kamati ya kuangalia suala hilo kwa undani.Lakini tukirudi nyuma,yeye mwenyewe naibu spika kwa maneno yake amesema,''Bunge haliwezi kuona Waziri mkuu amedharauliwa kiasi hiki likakaa kimya.''TAFSIRI YAKE NI KWAMBA,NI KWELI WAZIRI MKUU NA BUNGE KWA UJUMLA WAMEDHARAULIWA.Sasa mheshimiwa Pinda anasubiri nini?Naamini Watanzania wote watamuunga mkono kama hatasubiri ripoti ya tume.akachukua uamuzi wa kujiuzulu,atabaki na heshima yake na heshima kwa bunge na Watanzania wote kwa ujumla!

Jipumzikie mzee Pinda,serikali yenyewe hii ya kisanii,wakati wewe ni mchapa kazi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom