Bunge la Jamhuri ya Muungano limepitisha muswada wa sheria unaotamka kuwa kukutwa na bangi, mirungi sasa ni kosa la jinai

Kuanzia leo wateja zangu wote,, wengine mpo humu, skanka mzigo mpya huo ila imepanda bei,, mana sasa ishakuwa jinai,, nadhani tumeelewana, sio tena uje uanze kuleta songi songi, mahakamani napanda peke yangu, uji ntaenda kuunywa peke yangu,, yani majani haya sijui kwa nini serikali ya nchi hii ina chuki nayo, wakati haya ni majani kama majani mengine
20210822_120312.jpg
 
Kuanzia leo wateja zangu wote,, wengine mpo humu, skanka mzigo mpya huo ila imepanda bei,, mana sasa ishakuwa jinai,, nadhani tumeelewana, sio tena uje uanze kuleta songi songi, mahakamani napanda peke yangu, uji ntaenda kuunywa peke yangu,, yani majani haya sijui kwa nini serikali ya nchi hii ina chuki nayo, wakati haya ni majani kama majani mengine
View attachment 1929705
Dah
 
Huu ni miongoni mwa muswada mbovu sana kupitishwa.
Muswada huu unainyima nchi fursa ya kupata mapato ambayo yangetokana na kilimo na uuzaji wa bidaa hizo pendwa duniani.
na Pili tunaongeza mzigo kwa Mahakama kuu bila sababu za msingi. Maana yake sasa hata yale mateja ya pale River Side na Ubungo Terminal n.k yanatakiwa kesi zao za misokoto njaa itolewe uamuzi Mahakama kuu.
unaangalia mapato tu bali huangalii athari .
dunderhead
 
Daaah hili bunge la Ndugai sasa imedhamiria kuwajaza vijana magereza..Arusha mirungi inaliwa balaa sasa sisi wote si tutapotelea jela jamani kwa kesi ya mirungi ambayo ni jinai!!
 
Kwakua wanasema bange ina madhara basi wangeruhusu sahivi tuivute yote iishe ili watoto wetu wasiikute ikaja kuwadhuru na wao.
 
Tumekua Nchi ya hovyo sana kutunga sheria za kukandamiza Wananchi kila kukicha bila kufikiri madhara kwa Wananchi wako hiyo bangi sasa hivi Nchi nyingi zinapata kipato Zambia,Zimbabwe,SA na Swaziland...Mungu atusaidie kwa kweli huyu Spika kila kukicha anatamani ziwepo sheria za Watanzania kuwa jela kwanza bila hata kosa ndio furaha yake wakati Nchi za wenzetu wanafikiri jinsi ya kupunguza misongamano wao wanatamani kuongeza tumepata aina fulani ya Viongozi wakatili sana kwa Wananchi wao..
 
Wanaacha mambo ya msingi wanaelekeza nguvu kwenye mambo ya kipumbavu

Lingekuwa ni bunge la wananchi lingeangazia kuhusu rushwa, uvunjifu wa haki za binadamu na utawala wa sheria katika kila engo
Kila siku hoja zao za hovyo hovyo tuu wakitoka kidogo ni kumjibu Gwajima na kamati yao Dunia ipo kwenye janga la ugonjwa wao hilo hawalijui ili kuhadili jinsi ya kwenda na mazingira haya maana biashara imeshuka hata wao waweke kodi rafiki kwa Wananchi ndio kwanza wanakija na Tozo pana watu hapo si bora hata Bunge lisiwepo Nchi itaenda vizuri tu..
 
Hapa wamechemka mirungi haina lolote baya sijawahi kusikia mtu kala mirungi kaenda kufanya uhalifu ni starehe kama wanaokula tambuu tu bado walevi wa pombe hatari sana kuliko wala mirungi maana mlevi anaweza kulewa akaleta balaa mtaani lakini sio wala mirungi ni starehe tu na watu wanapiga porojo imeisha nadhani waje wathibitishe kitaalamu mirungi ni jinai. Toeni tozo za kijinga huku ruhusu mirungi weka ushuru mkubwa tu serikali itapata sana tu tutajenga mpaka vyoo.
 
Sheria nzuri, Tanzania tumechagua kukataa bangi na mirungi hivyo lazima tuwe na sheria kali kukomesha hilo. Wanaopinga sijui shida iko wapi?
Nataka uniambie tofauti ya mlevi wa pombe, mvuta bangi na mla mirungi na kati ya hawa watatu ni yupi kwako hana madhara katika jamii ikiwa inabidi atumie moja kati ya hayo.
 
Athari zipi? Nchi zinazoruhusu hayo mambo zina faida/hasara ipi?
Hakuna athari zozote zaidi ya hawa walevi waliotujazia kila sehemu mipombe mingine watu wakilewa wanaokotwa kwenye mitaro choka mbaya na afya zinadororoa na kuna walevi wana starehe tu wanakunywa kwa kiwango wako vizuri ila sijawahi kusikia mtu kala mirungi kaokotwa nje huko ni starehe tu na hakuna lolote. Ujinga tu wakiulizwa mtaje athari zake hamna. badala ya kujikita kupigana na madawa ya kulevya kama cocaine yenye athari za wazi kwa vijana mnaongeza mambo hayana ubaya wowote.
 
Nafkir wangefanya kukutwa na mapuli kumi ndio iwe jinai kwa kete mbili au tano watuache tuvute
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom